Humphrey Polepole na USEMI wa 'Mfalme mzee mjinga'

Humphrey Polepole na USEMI wa 'Mfalme mzee mjinga'

mtimawachi

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2020
Posts
2,108
Reaction score
3,155
Habari wanajamvi!
Nimemsikiliza kijana mwenzetu ndugu POLEPOLE katika hoja zake nyingi sana na mwisho hapa juzi akihojiwa.
IKANIBIDI nirudishe nyuma kumbukumbu hadi kipindi cha mchakato katiba mpya ulioongozwa na mzee wetu WARIOBA.

Katika ile tume,POLEPOLE alipewa ''airtime'' sana kupewa mialiko katika mijadala mbalimbali kuhusu rasimu ile.
Hata wanasiasa hasa chadema huyu alikuwa lulu kwao.

Nadhani hata kipenzi chetu MAGUFULI(RIP) alibaini kitu ndani yake akapenda kufanya nae kazi.

NINAAMINI kwa nafasi alizokuwa nazo kama ni fedha(mkwanja)anao na maisha tunayotamani wengi tayari ameshayavuka.

NIKAJIULIZA kama ndivyo nini kinamsumbua/kumuwasha kuzungumzia/kutetea hayo anayoyatetea? Kwanini asikae kimya tu aendelee na maisha yake? Mbona wenzake akina MAKONDA,BASHIRU nk wapo kimya?

LABDA nikiri wazi kwenye kipindi cha juzi katika wanahabari bora na makini kwa Tanzania yetu ni pamoja na yule kijana,lakini kwa kumwalika POLEPOLE nadhani hata yeye aliona kaingia kwenye msitu mwingine.
NIKIMAANISHA kilichoulizwa kilikuwa madini na kilichojibiwa madini.

Kuna usemi niliwahi usikia ''HERI YA KIJANA MDOGO MWENYE BUSARA KULIKO MFALME MZEE MPUMBAVU''

Katika tafakuri yangu nimebaini kuwa POLEPOLE ni kijana SHUJAA na MZALENDO wa kweli.
Na ndio maana anajitokeza hadharani kutoa mitizamo yake hata kama kuna watu wanaumizwa nayo.

ANA MAISHA maisha mazuri lakini kutokana na roho ya kizalendo alonayo anaona hivyo vyote si kitu ila awafungue na wengine bila kujali atafanywa nini.

KINGINE nimejiridhisha pasi na shaka kuwa CHADEMA hakifai kuwa mbadala wa CCM licha ya kuwa sasa NCHI inahitaji msaada wa mawazo mapya na chama kipya na sura mpya.

Namfananisha POLEPOLE na kijana mdogo mwenye busara.

Nawafanisha wale waliohudhuria kule kama wafalme wazee.

Wakati ni sasa vijana tuamke,hawa wazee wamefikia ukomo.

TUMUUNGE mkono POLEPOLE,tupinge kwa dhati matendo yanayoliangamiza taifa.(sio kupingapinga tu au kusifisifia tu.

NASIMAMA NA POLEPOLE.

NB:Kiitikadi mimi ni CCM tena timu MAGUFULI
 
Kwa hayo maelezo yako uliyotoa hapo ukianzia kwenye mchakato wa katiba kisha katika kipindi cha hayati Magufuli na sasa hapo alipo na alivyo huoni kuwa huyo jamaa ni kigeugeu ? ?!!
 
Kwa hayo maelezo yako uliyotoa hapo ukianzia kwenye mchakato wa katiba kisha katika kipindi cha hayati Magufuli na sasa hapo alipo na alivyo huoni kuwa huyo jamaa ni kigeugeu ? ?!!
Ulisikiza mahojiano ya juzi?
 
Hakuna mwenye akili anaweza kumwunga mkono mtu mnafiki kama Polepole.

1) Wakati akiwa mjumbe kwenye tume ya Warioba, alisema nini kuhusu katiba mpya?

2) Aliposhibishwa tumbo na Magufuli alisema nini kuhusu katiba mpya?

3) Alipokuwa mjumbe wa Tume ya Katiba alisema nini kuhusu maDC na maRC?

4) Aliposhibishwa tumbo kwa kupewa uDC, alisema nini kuhusiana na kazi za DC?

Mtunafiki, anayeongea kwa kutegemea siku hiyo tumbo limejaa au lina njaa, naye ni wa kumfikiria kuwa anaweza kutoa mchango wa maana? Polepole ni mnafiki, mwongo, na asiye na chochote anachosimamia.
 
Hana uzalendo wowote huyu. Yani kipindi cha Magufuli alikula matapishi yake yote. Mtu ambaye ni kigeugeu hafai kuitwa mzalendo.

Kipindi cha Magufuli usingemsikia akiongelea katiba ambayo alikuwa akizunguka na kulia kuwa inahitajika kabla ya kuteuliwa.

Polepole ni mchumia tumbo kama wachumia tumbo wengine. Tanzania hakuna mzalendo, inategemea tu kama muda huo mrija unamfikia.
 
Polepole huyu aliyeipigia debe katiba ya Warioba halafu papohapo akalamba matapishi yake na leo ameanzisha darasa la uongozi kwa unafiki? Mkuu unazungumzia huyu au polepole wa Kusadikika? Mkuu naelewa vyema kwamba nazungumza na polepole ila pole, ndio dunia.
 
Hii tabia ya wanasiasa kutokuwa na misimamo thabiti ndo inafanya kuaminiwa inakuwa ngumu, anaongea hiki Leo then hujui kesho kama ataamka na msimamo ule ule,sasa kuwashikia mapanga na marungu cc hatuwez kilichobaki tunapeleka kilio chetu kwa karma tu basi.
 
Habari wanajamvi!
Nimemsikiliza kijana mwenzetu ndugu POLEPOLE katika hoja zake nyingi sana na mwisho hapa juzi akihojiwa.
IKANIBIDI nirudishe nyuma kumbukumbu hadi kipindi cha mchakato katiba mpya ulioongozwa na mzee wetu WARIOBA.

Katika ile tume,POLEPOLE alipewa ''airtime'' sana kupewa mialiko katika mijadala mbalimbali kuhusu rasimu ile.
Hata wanasiasa hasa chadema huyu alikuwa lulu kwao.

Nadhani hata kipenzi chetu MAGUFULI(RIP) alibaini kitu ndani yake akapenda kufanya nae kazi.

NINAAMINI kwa nafasi alizokuwa nazo kama ni fedha(mkwanja)anao na maisha tunayotamani wengi tayari ameshayavuka.

NIKAJIULIZA kama ndivyo nini kinamsumbua/kumuwasha kuzungumzia/kutetea hayo anayoyatetea? Kwanini asikae kimya tu aendelee na maisha yake? Mbona wenzake akina MAKONDA,BASHIRU nk wapo kimya?

LABDA nikiri wazi kwenye kipindi cha juzi katika wanahabari bora na makini kwa Tanzania yetu ni pamoja na yule kijana,lakini kwa kumwalika POLEPOLE nadhani hata yeye aliona kaingia kwenye msitu mwingine.
NIKIMAANISHA kilichoulizwa kilikuwa madini na kilichojibiwa madini.

Kuna usemi niliwahi usikia ''HERI YA KIJANA MDOGO MWENYE BUSARA KULIKO MFALME MZEE MPUMBAVU''

Katika tafakuri yangu nimebaini kuwa POLEPOLE ni kijana SHUJAA na MZALENDO wa kweli.
Na ndio maana anajitokeza hadharani kutoa mitizamo yake hata kama kuna watu wanaumizwa nayo.

ANA MAISHA maisha mazuri lakini kutokana na roho ya kizalendo alonayo anaona hivyo vyote si kitu ila awafungue na wengine bila kujali atafanywa nini.

KINGINE nimejiridhisha pasi na shaka kuwa CHADEMA hakifai kuwa mbadala wa CCM licha ya kuwa sasa NCHI inahitaji msaada wa mawazo mapya na chama kipya na sura mpya.

Namfananisha POLEPOLE na kijana mdogo mwenye busara.

Nawafanisha wale waliohudhuria kule kama wafalme wazee.

Wakati ni sasa vijana tuamke,hawa wazee wamefikia ukomo.

TUMUUNGE mkono POLEPOLE,tupinge kwa dhati matendo yanayoliangamiza taifa.(sio kupingapinga tu au kusifisifia tu.

NASIMAMA NA POLEPOLE.

NB:Kiitikadi mimi ni CCM tena timu MAGUFULI
Usichanganye Roho Mbaya na Roho ya Kizalendo. Huyo Polepole ni Roho Mbaya tu ndio inamsumbua.
 
Itoshe kusema tu kuwa polepole ni maskini kama maskini wengine ndo maana anahangaika hovyo hana kitu. Ni uzalendo upi aliouonyesha kwa Taifa labda majivuno ya kutembelea ma V8 aliyokuwa akijivunia kipindi cha mungu mtu.
Narudia tena kipindi chenu kimekwisha kubalini uhalisia uliopo kazi iendelee.
 
Ulisikiza mahojiano ya juzi?
Mimi naona huyu jamaa huwa ana Dance according to the tunes just to satisfy his thirsty, kwenye katiba mpya aliunga mkono sana alipokuwa nje ya system lakini alipoingizwa kwenye system akasema katiba mpya haina umuhimu wowote, ni vipi Unaweza kumuamini MTU wa aina hiyo ?
 
Mimi naona huyu jamaa huwa ana Dance according to the tunes just to satisfy his thirsty, kwenye katiba mpya aliunga mkono sana alipokuwa nje ya system lakini alipoingizwa kwenye system akasema katiba mpya haina umuhimu wowote, ni vipi Unaweza kumuamini MTU wa aina hiyo ?
Lakini yeye alifanikisha mpaka rasimu ikafikishwa bungeni.
KOSA ni la akina Ndugai,Lissu,Lipumba,Mbowe,Zitto,Mnyika,na wabunge (wajumbe wenye vyama )kwa kuendekeza kwao ubishi hadi bunge likavunjika
 
Polepole afanye biashara nyingine, sio lazima Siasa, hata kuuza Mkaa pia mkono utaenda kinywani.
Alikufikishia rasimu ukaishia kutoka nje na kubandika plasta mdomoni,leo hii unadai katiba,mh! nyie watu nyinyi
 
Back
Top Bottom