Humphrey Polepole na USEMI wa 'Mfalme mzee mjinga'

Mkuu mi natafuta hela kwa jasho langu na kamwe sijawa waza kuiba au kupiga dili.
Na KAMWE siwezi kuwalamba miguu watu eti kisa nipate maslahi kama mfanyavyo.
Hapa nilipo navuna NYANYA zangu.
ILA namzungumzia POLEPOLE kwa kuwa ana kitu cha ziada nimekiona kichwani kwake
 
In short ni kwamba Kwa maisha yale aliyoishi na Magufuli na speech zake za kipindi kile
Ni dhahiri hakuna mtu mnafiki kama POLEPOLE
NI Opportunist flani hivi
Unadhani nini anakosa huyu kijana mpaka aamue kujitoa mhanga hadharani ili akipate?
 
Polepole watatiu tofauti. pole pole wa katiba ni tofauti na polepole wa JPM ambae alisema atuongei wakati wa kula. na saiz ni pole pole aliemaliza kula na ndio maana anaongea
 
Mtu mwenye Rangi za huyo kiumbe unawezaje mwelewa.🦎
 
Tatizo mnaongozwa na chuki na visasi.Mfuatilie vizuri POLEPOLE akiwa kiongozi wa ccm. Alikuwa anakibadili chama taratiibu na alishaanza kufanikiwa.
Hakuna cha kubadili chama wala visasi, naye kaoza tu hana uzalendo wowote. Polepole ni kigeugeu, huwezi kumuamini mtu ambaye leo anasema hivi kesho anasema vile. Eti kwa sasa hatuhitaji katiba wakati mieiz kadhaa nyuma kabla ya kushiba alikuwa anaililia katiba. Mtu kama huyu ni hatari hawezi kuaminika.
 
Polepole watatiu tofauti. pole pole wa katiba ni tofauti na polepole wa JPM ambae alisema atuongei wakati wa kula. na saiz ni pole pole aliemaliza kula na ndio maana anaongea
Vipi kile anachokizungumza,ni sahihi au?
 
Polepole watatiu tofauti. pole pole wa katiba ni tofauti na polepole wa JPM ambae alisema atuongei wakati wa kula. na saiz ni pole pole aliemaliza kula na ndio maana anaongea
Vipi kile anachokizungumza,ni sahihi au?
 
Vipi kuhusu anachokiongea?
 
Huyo kama yeye Mwenyewe ambavyo haeleweki kama ni kijana or Mzee ndivyo mawazo na mitizamo yake isivyoeleweka....

Leo atatuambia katiba Mpya muhimu,ukimpa usemaji wa ccm anageuka katiba Mpya sio muhimu..

Ukimuondoa kwenye usemaji wa ccm anageuka tena anasema katiba Mpya muhimu sasa MTU kama huyo utamwamini VP?
 
Kwa hayo maelezo yako uliyotoa hapo ukianzia kwenye mchakato wa katiba kisha katika kipindi cha hayati Magufuli na sasa hapo alipo na alivyo huoni kuwa huyo jamaa ni kigeugeu ? ?!!
Ccm huwa hawana akili ya kuchanganua mambo?
 
Huna lolote ujualo zaidi ya kupiga siasa mfu hapa jukwaani. Kwa taarifa yako sio Magufuli ama Polepole waliwahi kupambana na ufisadi, wao walikuwa wanapambana na matumizi ya neno fisadi. Walichokifanya ni Magufuli kutokana na kiburi cha madaraka, alikuwa anawakomoa wote waliompuuza kipindi yuko waziri, ama kiongozi yoyote aliyetofautiana naye kisiasa. Usichanganye mapambano ya ufisadi na kukomoa matajiri asiowapenda. Waliochota fedha za escrow walinaswa hadi na CCTV camera za bank, Magufuli aliwagusa au aliishia kuwaonea Kalasinga Seth na Mzee Rugemelila? Mtaje mwanasiasa mwenzake aliyemgusa.

Hilo la katiba mpya kuwa Ukawa walipotoka mchakato ukavurugika, hii inaonyesha ww ni bendera fuata upepo na huna lolote ujualo. Kwa taarifa yako Ukawa walipotoka ccm waliendelea na hilo bunge mpaka mwisho, na wakapitisha katiba pendekezwa baada ya kubadili maoni makubwa ya wananchi. Katiba hiyo pendekezwa ya ccm inangojea kura ya maoni, na ilisimama kupisha uchaguzi mkuu wa 2015. Alipoingia huyo kiongozi muovu aliyeko motoni, akagomea kumalizia huo mchakato kwa kusema sio kipaombele chake. Kwa hiyo usidhani hatujuia lolote kuhusu katiba mpya, na huyo Polepole wakati wa BMK yeye na hiyo tume yake waliishia kutukanwa na kukejeliwa na wabunge wa CCM, huku mama Samia akiwa naibu spika wa bunge lile la kihuni. Kwahiyo siku nyingine ukitaka kuanika ujinga wako, jikite kwenye ukweli huo.
 
Hakuna
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…