Lanlady
JF-Expert Member
- Feb 27, 2019
- 1,836
- 6,303
Kama una watoto, waombee, wakumbatie, wakikukosea wasamehe hata bila masharti; huo ndio urithi wako wa pekee!
Kuna watu wanatamani wangepata japo mtoto hata mmoja, lakini kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wao hawajafanikiwa. Na wengine tayari ni wazee.
Watoto ni urithi wa pekee kutoka kwa Muumba wa mbingu na ardhi!
Wape thamani kuliko chochote ulichonacho!
Waambie unawapenda hata kama uliwapata pasipo kutarajia.
Usiwafanye kuchukia maisha waliyonayo. Wasaidie kujitambua,kujikubali na kujithamini hata kama wana kasoro.
Usikubali mtu yeyote aharibu urithi wako. Usiruhusu watoto wako kuitwa majina yasiyofaa.
Hata ikiwa kwa gharama zozote; linda urithi wako. Watoto wako, ndio urithi wako!
Wabarikiwe wote wanaowapa thamani watoto wao na kuwasamehe makosa yao pasipo masharti. Upendo wa dhati husitiri wingi wa makosa. Waombee heri watoto wako!
Kuna watu wanatamani wangepata japo mtoto hata mmoja, lakini kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wao hawajafanikiwa. Na wengine tayari ni wazee.
Watoto ni urithi wa pekee kutoka kwa Muumba wa mbingu na ardhi!
Wape thamani kuliko chochote ulichonacho!
Waambie unawapenda hata kama uliwapata pasipo kutarajia.
Usiwafanye kuchukia maisha waliyonayo. Wasaidie kujitambua,kujikubali na kujithamini hata kama wana kasoro.
Usikubali mtu yeyote aharibu urithi wako. Usiruhusu watoto wako kuitwa majina yasiyofaa.
Hata ikiwa kwa gharama zozote; linda urithi wako. Watoto wako, ndio urithi wako!
Wabarikiwe wote wanaowapa thamani watoto wao na kuwasamehe makosa yao pasipo masharti. Upendo wa dhati husitiri wingi wa makosa. Waombee heri watoto wako!