Hussein Bashe amekutana na kufanya mazungumzo na Menejimenti ya Benki ya Equity nchini

Hussein Bashe amekutana na kufanya mazungumzo na Menejimenti ya Benki ya Equity nchini

JUMA JUMA

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2013
Posts
790
Reaction score
964
BASHE AENDELEA KUHAMASISHA TAASISI ZA FEDHA KUTOA MIKOPO YA RIBA NA MASHARTI NAFUU KWA WAKULIMA; UJENZI WA MAGHALA NA MIUNDOMBINU YA UMWAGILIAJI BAADA YA KUKUTANA NA MENEJIMENTI YA BENKI YA EQUITY

Dodoma, Tanzania.

Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe amekutana na kufanya mazungumzo na Menejimenti ya Benki ya Equity nchini, ambapo katika mazungumzo hayo ameishauri menejimenti hiyo kuongeza mitaji katika Sekta ya Kilimo hususani katika uwekezaji kwenye ujenzi wa miundombinu ya Umwagiliaji na Maghala.

Mazungumzo hayo ambayo yamefanyika katika Ofisi ya Waziri, Jijini Dodoma huku Ujumbe wa Benki ya Equity ukiongozwa na Bi. Isabela Maganga ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo hapa nchini.

Aidha Bi. Isabela kwa niaba ya benki hiyo amemuahidi Waziri Bashe kuwa wapo tayari kutoa ushirikiano na kusaidia Serikali katika kukuza Sekta ya Kilimo nchini.

Mkurugenzi huyo pia aliongozana na; Raphael Onyango (Mkurugenzi wa wateja wakubwa-makao makuu Kenya) pamoja na Aboubacar Youssoufou- Mkurugenzi wa Mikopo -Makao makuu Kenya).

#Ajenda10/30
#KilimoBiashara

IMG-20220427-WA0448(2).jpg


IMG-20220427-WA0447(2).jpg


IMG-20220427-WA0446(2).jpg
 
aanze kujenga kwanza irrigation scheme kwenye maeneo mbalimbali watu walime mwaka mzima...

Amshauri mama huko aliko,awaombe wanyamwezi waje wafungue kiwanda cha matrekta nafuu akiwaondolea kabisa kodi...huku wakikopesha wakulima matrekta kwa udhamini wa serikali..

Ajiwekee mazao mkakati na kuwadhamini wakulima na kuwasimamia na mavuno serikali inachukua yenyewe na kuwalipa wakulima au inakuwa tayari inasoko mahala kwa niaba ya wakulima..
 
Nilikuwa na mashaka sana kuhusu Bashe na sasa naanza kuamini nilikuwa sahihi kuwa na mashaka naye. Kwa akili ya darasa la NNE B huwezi kuacha Benki ya Kilimo ukakimbili Equity Bank ya Kenya ili kuendeleza kilimo Tanzania!!! Huu ni ulaghai.
Ile dam project ilikuwa na Maana Sana kwa ukame ule wa dodoma!!umwagiliaji wa mazao ungekuza uchumi Sana!!!
 
Kama unataka Equity Bank wafanye Biashara na wakulima pamoja na wafanyabiashara wa kilimo vipi kuhusu Tanzania Agriculture Development Bank wafanye kazi gani?

Vipi hawa National Bank of Commerce wafanye Biashara na Nani?

Huyu National Microfinance Bank akafanye Biashara na nani?

Kuna haja ya kufikiria sana kwa Hawa watendaji wetu wa serikali wanaacha kushirikiana na taasisi zilizojishakama pamoja na wao wanaenda kutafuta source nje Yan n sawa ukiwa unataka kupika ugali unaenda kukopa unga kwa jirani ili hali ndani kwako Kuna unga na mahindi mengi.

Hii nchi haina dira ya maendelelo.
 
Back
Top Bottom