Hussein Bashe: Serikali haiwezi kudhibiti bei ya Mazao

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Fuatilia yanayojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 15 leo Aprili 28, 2023.

Serikali imesema haiwezi kudhibiti bei ya mazao, bali inapunguza gharama za uzalishaji kwa wakulima pamoja na kuongeza tija kwenye uzalishaji ili wakulima waweze kupata faida baada ya gharama zao kupungua.

Haya yamesemwa na Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe wakati akijibu swali la Esther Edwin Maleko, Mbunge wa Viti Maalum aliyetaka kufahamu namna ni kwa gani Serikali inafanya ili kudhibiti bei ya Kahawa ambayo imekuwa inapanda na kushuka kila siku.

Aidha, Serikali inapanga kuhamasisha matumizi ya kahawa ndani ya Nchi pamoja na kuongeza uwekezaji kwa baadhi ya viwanda, mfano maeneo ya Kagera ambapo uwekezaji kwenye Kiwanda cha TANICA utaongezwa ili kuongeza ubora na kutoa uhakika wa bei nzuri kwa wakulima.

Pia, Waziri Bashe amesisitiza kuwa kuanzia mwaka 2025/26, Tanzania itaacha rasmi kusafirisha nje ya nchi korosho zisizo banguliwa kwa kuwa zote zitabanguliwa kwanza nchini.



GAMBO AKOSOA MFUMO WA UTOAJI LESENI BIASHARA YA VITO
Mbunge Mrisho Gambo amesema “Kuhusu wafanyabishara wa vito, watengenezaji na wauzaji wa bidhaa za sonara Nchini, ukiangalia Sera ya Madini ya Mwaka 2009 inasisitiza Wananchi wote kuongeza thamani ya madini lakini inapishana na matakwa ya Kisheria.”

Amesema ili mtu aweze kufanya biashara ya sonara anatakiwa kuwa na leseni tano, hali ambayo anaona haipo sawa na kudai kuwa ukijumlisha gharama zote za kukata leseni inakuwa ni zaidi ya Tsh. Milioni 13.
 
Hivi huu mtiririko wa namba katika shughuli za Bunge huwekwa kwa kupitia vigezo gani? Mathalani, ni Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 15.

Bunge ni la 12 tokea wakati gani? Mkutano wa 11 tokea lini? Na kikao cha 15 tokea mwanzo wa mwaka ama Bunge la kujadili bajeti lilipoanza kukaa?

Wajuzi wa mambo, tafadharini naombeni kuelimishwa.
 
Fuatilia yanayojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 15 leo Aprili 28, 2023.


Hoja ya dharura iwe matumizi mabaya ya magari ya serikali ...reference ajali ya Naibu Waziri Tamisemi
 
Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo na Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kusini Mhe. David Mwakiposa Kihenzile akiongoza Mkutano wa 11 Kikao cha Nane Bunge la 12 leo tarehe 28 Aprili, 2023

 

Attachments

  • WhatsApp Image 2023-04-19 at 10.09.48.jpeg
    80 KB · Views: 4
Kama serikali haiwezi kudhibiti bei za vyakula aondoke kwenye kiti hicho asilete tabia za watu wa pembe ya africa
 
Nchi ambayo raisi wa nchi anatamka hadharani adha ya kuishi kwa mlo mmoja ugumu wake kauona mwezi wa ramadhani tena anaishi kwenye kiyoyozi na afanyi kazi ya nguvu.

Halafu raia anaekula mlo mmoja kwa siku anashinda kubeba matofali siku nzima au kuchuuza mtaani siku nzima, halafu unasema shida yake umeijua mwezi wa mfungo tu; sijui nchi nyingine lakini uingereza ugomvi wake usingekuwa mdogo kwa kauli hiyo mpaka wanakutoa kwenye hiyo nafasi.

Sitegemei Bashe aelewe magumu ya watu wanaoshindia mlo mmoja, inakera tu anavyojitapa wakati anasema hayo ataacha bei ya chakula ipande ukiwafikiria watu wanaoshindia mlo mmoja kwa sababu ya bei kubwa, halafu watu hao hao mabillioni ya hela zao ndio wanatumia hela zao kununulia ruzuku za mabillioni, hela zao ndio zinatumika kufanyia upuuzi wake wa uwekezaji mashambani.

Halafu anasema awastahili huruma, kwa kujigamba kabisa hadharani. Kiasi kikubwa cha makusanyo ya serikali kinatoka miji mikubwa Arusha, Dar, Mwanza, na town centres nyingine hawa ndio hela zao unazochezea huko mashambani; wakulima awachangii kwenye makusanyo ya serikali kama hao watu unaowaumiza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…