KERO Huu mfereji mitaa ya Mwembeyanga Buza ni mbovu na una harufu kali, kwani Viongozi hawaoni au dharau?

KERO Huu mfereji mitaa ya Mwembeyanga Buza ni mbovu na una harufu kali, kwani Viongozi hawaoni au dharau?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

MeVSMe

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2024
Posts
270
Reaction score
425

Maeneo ya Buza, hususan Mwembeyanga, yamegeuka kuwa kitovu cha changamoto kubwa za kimazingira.

Mtaro wa maji machafu unaoanzia Mwembeyanga hadi karibu na Kituo cha Daladala cha Usalama unasababisha adha kubwa kwa wakazi na wapita njia wa eneo hilo.

PXL_20241115_125735412.jpg

Mtaro huu, ambao kwa kawaida unapaswa kusafirisha maji ya mvua, umekuwa tatizo sugu. Maji yaliyotuama ndani ya mtaro huo yamekuwa yakitoa harufu kali isiyovumilika, hali inayosababisha uvundo kila kona ya eneo hilo.

Tatizo hili limekuwa sugu kutokana na mtaro huo kuwa na miundo mbinu mibovu inayoshindwa kusafirisha maji ipasavyo.

PXL_20241115_125859517.jpg

Eneo hili linapakana na biashara nyingi, hasa za vyakula, jambo linaloongeza hatari ya maambukizi ya magonjwa kutokana na mazingira duni.

Hali hii inawafanya hata wapita njia na abiria wanaopitia Mwembeyanga kulazimika kushika pua ili kukwepa harufu mbaya.

Malalamiko ya Wakazi na Wafanyabiashara
Nilipozungumza na baadhi ya wenyeji wa eneo hili, wakiwemo waendesha bodaboda kutoka Kituo cha Gereji, walionyesha kusikitishwa sana na hali hiyo.

Wanasema harufu kali kutoka kwenye mtaro huo inawakera, lakini hawana namna ya kurekebisha tatizo hilo kwa sababu mamlaka zinazohusika hazijachukua hatua stahiki.

Kwa mujibu wa wakazi hao, maji yanayotoka kwenye mtaro huo ni ya mvua ambazo hunyesha mara kwa mara, lakini hayawezi kupita kwa sababu mtaro umejaa uchafu na ni mbovu.

PXL_20241115_125922188.jpg

Ingawa hivi karibuni kulionekana juhudi za kuchimba na kusafisha mtaro, kazi hiyo ilikatizwa kabla ya kuzaa matunda.

Athari za Kiafya na Mazingira
Harufu inayotokana na maji yaliyotuama kwenye mtaro huu si tu inakera, bali pia ni hatari kwa afya ya watu wanaoishi na kufanya kazi katika eneo hilo.

Biashara za vyakula zinazofanyika karibu na mtaro huo zinaongeza hatari ya kuenea kwa magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu, huku hali ya mazingira ikizidi kuwa mbaya.

Wito kwa Mamlaka Husika
Ni dhahiri kuwa hali ya mtaro wa Mwembeyanga inahitaji kushughulikiwa haraka. Mamlaka za Manispaa ya Temeke zinapaswa kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha mtaro huo unasafishwa na kurekebishwa ili kudhibiti maji yaliyotuama na kuondoa harufu kali.

Afya za wananchi na usitawi wa biashara za eneo hilo vinategemea juhudi za dhati kutoka kwa mamlaka husika.

Bila hatua za haraka, eneo hili linaweza kuwa kitovu cha mlipuko wa magonjwa na changamoto kubwa za kimazingira.

Nihitimishe Kwa kusema Mwembeyanga ni mfano hai wa Changamoto zinazotokana na miundombinu mibovu na ukosefu wa usimamizi thabiti.

Natoa wito kwa mamlaka kuchukua hatua za haraka kurekebisha hali hii na kuhakikisha mazingira rafiki kwa wananchi na wajasiriamali wa eneo hilo.
 
Maeneo ya Buza, hususan Mwembeyanga, yamegeuka kuwa kitovu cha changamoto kubwa za kimazingira.

Mtaro wa maji machafu unaoanzia Mwembeyanga hadi karibu na Kituo cha Daladala cha Usalama unasababisha adha kubwa kwa wakazi na wapita njia wa eneo hilo.

Mtaro huu, ambao kwa kawaida unapaswa kusafirisha maji ya mvua, umekuwa tatizo sugu. Maji yaliyotuama ndani ya mtaro huo yamekuwa yakitoa harufu kali isiyovumilika, hali inayosababisha uvundo kila kona ya eneo hilo.

Tatizo hili limekuwa sugu kutokana na mtaro huo kuwa na miundo mbinu mibovu inayoshindwa kusafirisha maji ipasavyo.

Eneo hili linapakana na biashara nyingi, hasa za vyakula, jambo linaloongeza hatari ya maambukizi ya magonjwa kutokana na mazingira duni.

Hali hii inawafanya hata wapita njia na abiria wanaopitia Mwembeyanga kulazimika kushika pua ili kukwepa harufu mbaya.

Malalamiko ya Wakazi na Wafanyabiashara
Nilipozungumza na baadhi ya wenyeji wa eneo hili, wakiwemo waendesha bodaboda kutoka Kituo cha Gereji, walionyesha kusikitishwa sana na hali hiyo.

Wanasema harufu kali kutoka kwenye mtaro huo inawakera, lakini hawana namna ya kurekebisha tatizo hilo kwa sababu mamlaka zinazohusika hazijachukua hatua stahiki.

Kwa mujibu wa wakazi hao, maji yanayotoka kwenye mtaro huo ni ya mvua ambazo hunyesha mara kwa mara, lakini hayawezi kupita kwa sababu mtaro umejaa uchafu na ni mbovu.
Ingawa hivi karibuni kulionekana juhudi za kuchimba na kusafisha mtaro, kazi hiyo ilikatizwa kabla ya kuzaa matunda.

Athari za Kiafya na Mazingira
Harufu inayotokana na maji yaliyotuama kwenye mtaro huu si tu inakera, bali pia ni hatari kwa afya ya watu wanaoishi na kufanya kazi katika eneo hilo.

Biashara za vyakula zinazofanyika karibu na mtaro huo zinaongeza hatari ya kuenea kwa magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu, huku hali ya mazingira ikizidi kuwa mbaya.

Wito kwa Mamlaka Husika
Ni dhahiri kuwa hali ya mtaro wa Mwembeyanga inahitaji kushughulikiwa haraka.
Mamlaka za Manispaa ya Temeke zinapaswa kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha mtaro huo unasafishwa na kurekebishwa ili kudhibiti maji yaliyotuama na kuondoa harufu kali.

Afya za wananchi na usitawi wa biashara za eneo hilo vinategemea juhudi za dhati kutoka kwa mamlaka husika.

Bila hatua za haraka, eneo hili linaweza kuwa kitovu cha mlipuko wa magonjwa na changamoto kubwa za kimazingira.

Nihitimishe Kwa kusema Mwembeyanga ni mfano hai wa Changamoto zinazotokana na miundombinu mibovu na ukosefu wa usimamizi thabiti.

Natoa wito kwa mamlaka kuchukua hatua za haraka kurekebisha hali hii na kuhakikisha mazingira rafiki kwa wananchi na wajasiriamali wa eneo hilo.
Wale WA mwembeyanga, mshayazoea haya na na nyie?
 
Mwembe yanga sio buza. Hayo ni maeneo mawili tofauti japo yapo katika wilaya moja ya Temeke.
 
Sawa Mkuu.
Sasa tuachane na sehemu, tuzungumze kuhusu Hali ya huu mfereji
Huo mfreji kweli umejaa michanga pamoja na taka maji hayatembei kabisa lakin hapo kwa pembeni kuna kiwanda cha ngozi ndicho kinachotoa iyo harufu kali na sio huo mfereji.
 
Huo mfreji kweli umejaa michanga pamoja na taka maji hayatembei kabisa lakin hapo kwa pembeni kuna kiwanda cha ngozi ndicho kinachotoa iyo harufu kali na sio huo mfereji.
Mimi nilifika na ku survey, watu mabodaboda wenyewe wamekiri kuwa maji hayo yanatoa harufu. Na juzi walivokuja kuchimba upya huo mtaro ndo Hali ya harufu ikazidi.
Hicho kiwanda kinawezakuwa kinatoa harufu, lakini harufu inayotapakaa ni ya maji,
Na wenyeji wenyewe wamekiri
 
Mimi nilifika na ku survey, watu mabodaboda wenyewe wamekiri kuwa maji hayo yanatoa harufu. Na juzi walivokuja kuchimba upya huo mtaro ndo Hali ya harufu ikazidi.
Hicho kiwanda kinawezakuwa kinatoa harufu, lakini harufu inayotapakaa ni ya maji,
Na wenyeji wenyewe wamekiri
sijakataa kua huo mfereji hauna harufu ila harufu yake sio kali hivyo. Hio harufu kali ni ya kutoka katika hicho kiwanda cha ngozi hapo.
 
Kwakweli huu mfereji tangu nipo mdogo mpaka utu uzima, unanuka sana yaani ni kama umeunganishwa na vyoo vya gereji za hapo. Sasa hapo pakinyesha mvua barabara yote inajaa maji, mfereji umejaa tope la uchafu
 
Kwakweli huu mfereji tangu nipo mdogo mpaka utu uzima, unanuka sana yaani ni kama umeunganishwa na vyoo vya gereji za hapo. Sasa hapo pakinyesha mvua barabara yote inajaa maji, mfereji umejaa tope la uchafu
Acha tu Yani, ukipita pale hutamani hata kuvuta pumzi
 
Hivi hii miundombinu ya mifereji kwa miaka yote imeshindwa kubadilishwa nakufanyiwa ubunifu mpya?
 
Kwakweli huu mfereji tangu nipo mdogo mpaka utu uzima, unanuka sana yaani ni kama umeunganishwa na vyoo vya gereji za hapo. Sasa hapo pakinyesha mvua barabara yote inajaa maji, mfereji umejaa tope la uchafu
Inasikitisha sana yaani kama hakuna halmashauri hapo,
Kama tatizo ni la miaka basi inabidi wachangishe tu hela kila mwezi wapambane na hii kadhia
Wananchi wenyewe wakisafisha watajua uchungu wake na watahakikisha hakuna mchafu yeyote anaemwaga uchafu humu

Mtalindana sana
Ila mkisubisubiri serikali utaazeekea hapo na utawahadithia wajukuu na kusema hapa nina miaka 70 hali ilikuwa hivi hivi tangu udogo wako

Aitwe yule mdada wa kuchangisha
 
Unajiita unaishi dar tena mkunduni kwa mpalange hujaona masaki upanga ostabei na kunduchi.bora hata alieko mwanza nyamanoro au buzuruga.kuishi buza ni kama gaza.ondokeni huko dar kumeoza majengo yanaanguka na mitaro itapeana kipindupindu na nyinyi masikini
 
Back
Top Bottom