Huu ni kweli kuhusu Kamari

Huu ni kweli kuhusu Kamari

Maisha yamejaa kamali kuanzia pale unapozaliwa hadi unakufa... Unasomeshwa huku hujui kwamba utafauru ama utaferi,... Ukiferi tayari umeliwa maana umegharamia ada

Unaumwa unaenda tibiwa kwa gharama kubwa lakini hujui kwamba utapona ama utakufa... Ukifa tuu umeliwa nayo in kamali....

So kamali ipo na itachezwa
tafsir yako ni hatar sana kwa afya ya binadam,anyway maisha ni kuchagua kk!!!
 
Ungekua na akili hayo madhara unayosema ungetafuta solution yake, biashara zote duniani ni kamari, unaenda kununua nguo dubai mfano, elfu 10 unakuja kuuza elfu 15 bila kujua nani atanunua hiyo nguo. Ukome kuponda ajira za wenzako kwa kusingizia biblia na Quran, Juzi nimetoka kushinda milioni 2 kwa elfu 50 na kodi imekatwa imeenda kwenye elimu bure ya watoto wako, afu umekunywa togwa asubuhi unatukana ajira zinazosomesha hadi watoto wako, Pumbavu sana wewe...
 
Vp sis tunaondesha maisha yetu kwa KAMARI
usitake wote tufanane na hiz dini tuliletewa tu
 
Ungekua na akili hayo madhara unayosema ungetafuta solution yake, biashara zote duniani ni kamari, unaenda kununua nguo dubai mfano, elfu 10 unakuja kuuza elfu 15 bila kujua nani atanunua hiyo nguo. Ukome kuponda ajira za wenzako kwa kusingizia biblia na Quran, Juzi nimetoka kushinda milioni 2 kwa elfu 50 na kodi imekatwa imeenda kwenye elimu bure ya watoto wako, afu umekunywa togwa asubuhi unatukana ajira zinazosomesha hadi watoto wako, Pumbavu sana wewe...
umeongea vema ila hapo kwenye tusi la PUMBAVU naona likikirudia wewe itapendeza zaidi!!!!
 
Tatizo michezo yote ambayo ilikuwa ni burudani imegeuka kuwa biashara ama kamari. Kuanzia hii michezo ya kawaida kama pool table,drwaft, karata bao nk watu wanashindana kwa madau.

Kwenye soka huko ndio biashara kubwa kabisa haswa kwenye haya makampuni ya betting. Wapenzi wa soka nao wamechukulia kama fursa ya kujipatia kipato. Ila ukiwa makini na ukacheza kwa nidhamu nakuhakikishia unapata pesa kibao huku shughuli zako zikiendelea.

Kamari mbaya ni ile inayopoteza muda mwingi ukiwa sehemu moja ama ukicheza ama ukiangalia wenzio wakicheza.

Ila kamari kuna wakati mwingine inalipa.
 
Ungekua na akili hayo madhara unayosema ungetafuta solution yake, biashara zote duniani ni kamari, unaenda kununua nguo dubai mfano, elfu 10 unakuja kuuza elfu 15 bila kujua nani atanunua hiyo nguo. Ukome kuponda ajira za wenzako kwa kusingizia biblia na Quran, Juzi nimetoka kushinda milioni 2 kwa elfu 50 na kodi imekatwa imeenda kwenye elimu bure ya watoto wako, afu umekunywa togwa asubuhi unatukana ajira zinazosomesha hadi watoto wako, Pumbavu sana wewe...

Unacheza kamari lakini hujui madhara yake___subiri siku utakapotiwa kwa mwanandani utakumbuka nasaha/ mawaidha ya mleta uzi___utajuta juto la kuzaliwa. Siku hiyo hakuna cha james wa Abdala atakaye kuja kukuokoa,,,
 
Mmehamia na huku tena, mliochafua viunga vya airport kwa kukata gogo hovyo, huku mkitaka kwenda Israel bila nauli[emoji2][emoji2][emoji2]
 
Kwasasa Watanzania wengi wanapata kuvutika kwakasi kuingia ktk michezo ya kamari bila kuelewa ina ATHARI KUBWA MNO kuanzia katika JAMII na katka DINI coz naamin zaid ya 95% ya watanzania ni wakristo na waislam, din ambazo zinapiga sana vita Kamari kupitia maandiko ya Quran na Biblia. nlitaman sana kuwapa mwanga uharamu na athari za mchezo huu kama ifwatavyo

N;B Kila ntapokuwa nalitaja neno KAMARI ntakuwa nimeyaongelea maneno 5 ya kingreza yenye maana za; GAMBLING, WAGERING, GAMING, LOTTERY, BETTING pia nkitaja kamari namaanisha kiarabu cha maneno 3, MAISIR, MAISIRA na QIMAR]

Anyway,
KUFUPI, KAMARI ni Ku-risk/hatarisha mali ya thaman katika matokeo ya bahati WANAHARAKATI au watetezi WA KAMARI WALIKUJA NA HOJA KUU 2 KUHALALISHA KAMARI

KWANZA husema kamari ni kama bima tu coz kwote si unatoa ela afu mwisho wa siku unaweza ukazipata likitokea la kutokea japo hawa wanaharakati wanasahau bima ipo kumsaidia mtu mwenye matatzo tofauti na kamari huleta matatzo ktk jamii

PILI hutumia vifungu vya bible kama vile walawi walivokuwa wanapiga kura kuchagua mbuzi wa kafara, Yoshua kupiga kura ktk kugawa ardhi kwa makabila 12 ya Israel, Nehemia pia alipga kura kuamua nan wataish ndan ya ukuta wa Yerusalem, mitume wa yesu kupga kura mrithi wa nafas ya Yuda etc. Japo hapa wanakamari hushindwa kutambua kuwa hakuna mali zilizowekwa na washindan(risked assets) tofauti na kamari zilivo ambapo A na B hupanga kila mtu kuweka sh 1000 na mshind wa tukio la la kuamua mshind atapata sh 2000.

TUANZE NA ATHARI ZA KAMARI # KIJAMII ZAID
1. KUCHOCHEA Uvivu - Uchezaj kamari hauusish kufanya kaz inayoongeza pato la taifa GDP kihalali ivo mtu akshnda anapata kpato bila kufanya kaz(hakuna bidhaa au huduma aliyoiongeza ktk uchumi), mbaya xana kiuchumi coz kund kubwa la wananchi likijitoa liwe linaishi kwa kutegemea kamari sjui itakuwaje na tutakula nini.kwamfano!

2.KUHARIBU MICHEZO. Somtyms makampun makubwa ya kamari yanaweza mwonga mchezaj flan mkali acheze chn ya kiwango au yanampa madawa ili acheze chn yakiwango ili timu wanayoamin weng huyo mchezaji ana mchango mkubwa ili ishinde, ifungwe wao wapge pesa ndefu Mfano mzuri MARADONA aleingzwa ktk utumiaj madawa ili Napoli iwe inafungwa na wao wale pesa za wanaozan uwepo wake uwanjan utasaidia Napoli kushnda. Hii ilichangia sana kumuua kiwango Maradona, Napoli ilianza kupata matokeo mabovu na tunaweza kusema pia kashfa ya caciopori, anguko la soka la Italia limechangiwa sana na makampun ya kamari manake kule ndo kama nyumban kuanzia kupanga matokeo nk

3. UJAMBAZ NA WIZ
Wengne wakiliwa pesa hawana seem nyngne ya kupata ivo hulazmika kutafta pesa isivo halali kwa kupora watu,mabenk maofis etc. Nch kama Italy ilipata xana tatzo ili lililoletwa na wanakamari ambao weng hawkuwa na ajira

4. ADDICTION yake ni mbaya sana kama ulevi wazungu weng wameathrika na ulev wa kamari kama watz tulivoathirika na ulevi wa pombe za madebe eg mbege, ilanz, chimpumu, pombe ya mahindi etc

MECHANISM ukishndwa utataman utafte ela tena ukacheze kurudisha ulizoliwa na ukishinda utataman ucheze tena kujiongezea ela zaid si mnajua ela ikishakutawala hautarizika nayo

5. USTAWI_MDOGO WA JAMII coz mshahara wa baba unatumika zaid ktk kamali na si ma2miz ya nyumban ata ndoa yaweza vunjka coz family haipat maitaj muim,

6. MADENI umekopa ili ucheze umeliwa aya utalipaje xaxa!!

7. MAISHA YA PRESHA ukishaweka ela au mali yako kitachofwata ni kuish kwa presha had matokeo yatapotoka, hii huweza kuleta madhara makubwa kama vifo vya gafla , magonjwa ya moyo, kuzmia nk

VITABU VYA DINI VINASEMAJE?
1. QURAN
Japo Koran imepiga marufuku. chakuskitisha baaz ya nchi za kiislam kama Iran zmeanza nazo kuzidiwa na wimbi la “business” hii , ila tukija ktk Koran, kamari mekatazwa kabisa na Mwenyezi Mungu Subhanahu wa ta'ala kwa mfano wa vifungu vifwatavyo Surat Al Baqarah 2;219 inasema kwamba “wanakuuliza juu ya ulevi na [HASHTAG]#kamari[/HASHTAG].

Sema: Katika hivyo zipo # dhambi kubwa na manufaa kwa watu. Lakini dhambi zake ni # kubwa zaidi kuliko manufaa yake” (inamaanisha japo kamari ina faida kwa mshind anapata mali ila ina madhara makubwa kuliko faida na ni dhambi kubwa kwa Mungu) pia, Surat Al-Ma’idah 5;90-91 pia inasema “Enyi mlio amini! Bila ya shaka ulevi, na kamari, na kuabudu masanamu, na kupiga ramli, ni uchafu katika kazi ya Shet'ani. Basi jiepusheni navyo, ili mpate kufanikiwa.”
.
Wacheza kamari huendeleza roho mbaya na yakiadui dhidi ya mshindani wake japo wanaweza wakadai kupoteza hela kwao sio ishu ila naweza kuhoji hili, mtu alepoteza ela ktk kamari weng huwa frustrated kutokana na matokeo kuwa mabaya, hasira ya kushindwa na majuto ya kucheza

2. BIBLE
KIufupi tu hakuna kifungu cha bible kinachokataza DIRECT kamari ila kuna rundo la vifungu linalokataza kila mchakato wa kamari unavunja sheria

Kwanza USITAMAN MALI YA MTU MNGINE – kamari ni mchezo ulolenga ktk tamaa za kujtajirisha kwa # haraka kwa kujinufaisha kwa hasara, maumivu, na kuptia mali za m2 mngne huku mwenzako akpata # hasara na Mungu ametukataza # tustaman mali za m2 mngne kutoka 20:17.

Na pia tunaona ktk mithal 13:11Mungu kuptia mfakme Suleiman anaonya kuwa tuspende sana utajir wa haraka (kwanjia za panya) ni bora ujitaftie # kdogokdogo lakn cha halali. Kushinda kamari ni utajiri wa haraka na wa njia za panya kwa kufaidika 100% kwa machoz ya mtu. mithali 10:4 inatukumbusha tujtajirishe kwa bidii za mikono na sio kuwa wavivu Vifungu hivi vinatuonya attitude unayotakiwa kuwa nayo kuusu pesa I Tim 6:10 Pesa ndo shina la maovu meng dunian kuwa nayo makn Waebr 13:5 kaa mbali na tamaa ya pesa, rizka na ulichonacho pia Marko 4;19, 10;25 na Luka 16;13 zinatueleza ilivo ngumu kwa mtu mwenye tama ya pesa na mali kama mcheza kamari kumpenda Mungu huwez mtumikia Mungu huku una tamaa ya Pesa

SO UKIWA KAMA MTANZANIA MWENZANGU NAKUSHAURI PIGA VITA VITENDO VYOTE VYA KAMARI NA ATHARI ZAKE kama una tabia ya kubetbet acha kiroho safi, kama una tabia ya kuwafwata wale wahuni wa kamari Ubungo acha pia utakuwa umeisaidia jamii na kidini pia umepunguza madhambi. ASANTENI
Hamna kitu unajua wewe. Kwa taarifa yako kucheza kamari siyo dhambi. Kila kitu ni jinsi unavyokichukulia wewe binafsi. Wanaocheza Kamari huweka pesa kwenye mchezo kwa hiari yao kabisa na tena wanalipa na kodi ya Serikali. Kamari ninayozungumzia mimi ni ile iliyoruhusiwa kisheria. Kama hujaiba, hujadhulumu, hujaua mtu, umetumia pesa yako ya halali kucheza kamari kuna ubaya gani?
Labda nikuulize, hivi ukilima shamba na ukagharamia maelfu ya fedha kuanzia kuandaa shamba, kununua mbegu na kupanda halafu mvua zisinyeshe na mazao yakakauka shambani au ukavuna kidogo sana na kupata hasara; hiyo inatofauti gani na kucheza kamari?
Au ukawekeza pesa zako kwenye soko la hisa (stock market) na mwisho wa siku ukaambulia hasara, hiyo nayo inatofauti gani na kamari?
Au ukaamua kufuga kuku na ukawekeza mamilioni kwa kujenga banda na kununua vifaranga na chakula chao, halafu kuku wote wakaugua "mafua" ya ndege na kufa, hiyo nayo inatofauti gani na kamari?

Kila kitu kina madhara yake na faida zake. Ni namna tu unavyofanya. Mimi naamini kuwa kila kitu kikifanyika kwa kiasi na kwa utaratibu basi hakina madhara. Kuna namna ya kucheza kamari na ukafanikiwa sana tu na pia kuna namna ukicheza kamari unafilisika kabisa. Pia kuna namna ya kuwa mkulima mzuri na ukafanikiwa, lakini pia ukiwa mkulima "mjinga" unafilisika na kuwa maskini vile vile. Hata biashara pia ni hivyo hivyo. Wapo wengi tu wamefanya biashara na kuishia kufilisika kabisa na kubakia na majuto. Na kuna watu wanacheza kamari na wanapiga "hela" ndefu kila siku.

Kwa kifupi, chochote unachokifanya, kifanye kwa akili na maarifa na kiasi. Ndiyo maana hakuna mahali ukisoma kwenye Biblia utaona imeandikwa usicheze kamari. Lakini imeandikwa "kuweni na kiasi katika mambo yote". Dhambi ni nini? Dhambi ni kuasi, kwa kuvunja amri, sheria na maagizo ya MUNGU. Biblia haisemi kama kucheza "kamari" ni kuvunja "amri", "sheria" au "maagizo" ya MUNGU.
 
Back
Top Bottom