Huu ni ugonjwa gani?

Dr.philosophy

Senior Member
Joined
Oct 12, 2012
Posts
122
Reaction score
27
wadau hebu nisaidieni,huyu ndugu yangu ana dalili hizi; anaumwa joint za magoti,anaishiwa nguvu,akiwa na njaa anahisi kutetemeka,anapungua wakati mwingine mwili wake unarudi kama kawaida.mara nyingi sana amewahi kupimwa amekuwa akikutwa na u.t.i na malaria.amekula dawa sana.ameshapima ukimwi kama mara tano hivi na sukari vyote hana,yaani maumivu ya joint,kuishiwa nguvu na kupungua ndo imekuwa sehemu ya maisha yake,je ni ugonjwa gani huo wanajamvi? Natanguliza shukurani
 
acheki sukar na vidonda vya tumbo dawa haziliwi mkuu zinamezwa na kunywewa
 
Nakushauri umpeleke hospitals kubwa yaani za rufaa lakini kama utaendelea na hizi za mikoa/wilaya ama private watakulia pesa na watambambikizia magonjwa ambayo hana ili wapige pesa vizuri.

Kwa hizo dalili nashawishika kusema ana Peripheral neuropathy ndo huwa inaanza hivyohivyo na akichelewa zaidi ategemee makubwa zaidi.

Narudia:Mpelekeni hospitals za rufaa though majibu huchelewa lakini huwa ya uhakika.
 

Mkuu,ana muda gani na hilo tatizo?
Kama ni miezi ama miaka then fanya umpeleke hospital za rufaa ili upate uhakika wa tatizo though zinashabihiana kabisa na za Peripheral neuropathy hasa stage za mwanzo.

Usimpeleke kwa hawa jamaa wa
tiba mbadala bila kujua tatizo lake hasa maana watakupiga pesa Tu.

Na usithubutu kumpeleka kwa sangoma maana Kuna kasumba ya watu kwenda huko wakiambiwa tatizo halionekani hospital.

Kila lenye kheri mkuu.
 
Msiache kuangalia na magonjwa mengine yasiyotarajiwa kabisa kama vile brucellosis, especially kama kuna mazingira yanayoweza kupelekea kupata ugonjwa huo japo kwa ugonjwa huo nilitegemea angekuwa anakosa hamu ya kula.
 
Hizo ni dalili za kisukari cha msingi ni kutokula masaa 12 na kwenda kupima damu asubuhi kabla ya kula chochote. Ikishajulikana au kisukari inabidi awe ana pima mara kwa mara
 
Mwanangu hz hospt ndogo havina vifaa vya haja nenda referall mkubwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…