Mgeni wa Jiji
JF-Expert Member
- Jul 27, 2017
- 9,758
- 18,431
Wasalaam JF members[emoji1538]
Moja kwa moja kwenye mada, ila kabla sijagusa mhimili wa mada niweke misamiati hii sawa kwa kiwango cha upeo wangu (siyo cha BAKITA)
Tafsiri ya haya maneno:
1. KUFA, binafsi naamini wapo wanadamu wanaokufa na wasiokufa. Kufa kwa tafsiri yangu ni roho kuukimbia mwili kutokana na uharibifu wa ghafla wa mwili utokanao ama na Ajali, Kupigwa, au Majanga asili mfano matetemeko au radi
2. KUFARIKI, hili linakaribiana sana na KUFA ila ni tofauti kimazingira. Hapa pia roho inaukimbia mwili. Ila tofauti hapa huwa si kutokana na uharibifu wa mwili bali hutokana tu na roho kuichoka hali ya mwili. Mara nyingi wanaofariki ni wagonjwa, watu waliopata njaa kali au waliokosa hewa. Yaani vile vitu vinavyoutesa na kuuchosha mwili basi utafariki
3. KUAGA DUNIA, hili kundi ndio linanishangaza kidogo katika tafakari yangu. Hapa inatokea roho inawasiliana moja kwa moja na baadhi ya viungo vya mwili hususa ubongo na kuupa taarifa kuwa sasa roho inaitaji kutoka na kwenda eneo tofauti. Hii ni hali ya bahati sana kutokea kwa mwanadamu. Je, umewahi kusikia watu wakisema "alijua atakufa akawa anatuaga" basi ndio hali hii. Tatizo ni moja tu watu hudhani mtu huyo kafa kumbe hajafa bali ameaga dunia.
Watu wa kundi hili mara nyingi huwa ni wazee au hata vijana na watoto, na hasa kwa uzoefu na fikra yangu huwa halii hii huwapata wale watu wakorofi na wenye misimamo yao.
POINT YA ZIADA:
KULALA: Umewahi kusikia habari za Yesu kristu au Nabii Issaa za kuwaambia waombolezaji kuwa "mtoto hajafa amelala tu!". Umekumbuka ee!, basi nikuongezee jambo la ziada KULALA ni hali ya roho kutoka ndani ya mwili na kuanza kuushangaa ama mwili wenyewe au mazingira yaliyoizunguka au huamua tu kutembea tembea huku na kule na hapa ndipo watu huota ndoto za ajabu kama kukimbizwa au kutaka kutokewa na jambo fulani kisha ghafla huzinduka toka usingizini na kuhema juu juu. Hali hii huzitokea roho zinazozurula.
Labda utapata swali, vipi wanaolala na kutokuamka kabisa?, je hawa hwa wana KUFA, FARIKI au WANAAGA DUNIA? Hawa hawapo kwenye kundi lolote kati ya haya matatu. Kifupi ni kuwa hawa ni watu ambao wamepatwa na 'ajali tu' yaani hakukuwa na taarifa yoyote kati ya roho na mwili.
Huo ndio utofauti angu wa mambo haya matatu. Kumbuka utofauti wangu huu unaweza kuwa tofauti na mtazamo wako.
Je, unadhani ipo mifano ya kiimani itakayoweza weka mbolea kwenye dhana hii ya utofauti wa KUFA, KUFARIKI na KUAGA DUNIA? Basi usisite ongeza nyama nyama pia.
Moja kwa moja kwenye mada, ila kabla sijagusa mhimili wa mada niweke misamiati hii sawa kwa kiwango cha upeo wangu (siyo cha BAKITA)
Tafsiri ya haya maneno:
1. KUFA, binafsi naamini wapo wanadamu wanaokufa na wasiokufa. Kufa kwa tafsiri yangu ni roho kuukimbia mwili kutokana na uharibifu wa ghafla wa mwili utokanao ama na Ajali, Kupigwa, au Majanga asili mfano matetemeko au radi
2. KUFARIKI, hili linakaribiana sana na KUFA ila ni tofauti kimazingira. Hapa pia roho inaukimbia mwili. Ila tofauti hapa huwa si kutokana na uharibifu wa mwili bali hutokana tu na roho kuichoka hali ya mwili. Mara nyingi wanaofariki ni wagonjwa, watu waliopata njaa kali au waliokosa hewa. Yaani vile vitu vinavyoutesa na kuuchosha mwili basi utafariki
3. KUAGA DUNIA, hili kundi ndio linanishangaza kidogo katika tafakari yangu. Hapa inatokea roho inawasiliana moja kwa moja na baadhi ya viungo vya mwili hususa ubongo na kuupa taarifa kuwa sasa roho inaitaji kutoka na kwenda eneo tofauti. Hii ni hali ya bahati sana kutokea kwa mwanadamu. Je, umewahi kusikia watu wakisema "alijua atakufa akawa anatuaga" basi ndio hali hii. Tatizo ni moja tu watu hudhani mtu huyo kafa kumbe hajafa bali ameaga dunia.
Watu wa kundi hili mara nyingi huwa ni wazee au hata vijana na watoto, na hasa kwa uzoefu na fikra yangu huwa halii hii huwapata wale watu wakorofi na wenye misimamo yao.
POINT YA ZIADA:
KULALA: Umewahi kusikia habari za Yesu kristu au Nabii Issaa za kuwaambia waombolezaji kuwa "mtoto hajafa amelala tu!". Umekumbuka ee!, basi nikuongezee jambo la ziada KULALA ni hali ya roho kutoka ndani ya mwili na kuanza kuushangaa ama mwili wenyewe au mazingira yaliyoizunguka au huamua tu kutembea tembea huku na kule na hapa ndipo watu huota ndoto za ajabu kama kukimbizwa au kutaka kutokewa na jambo fulani kisha ghafla huzinduka toka usingizini na kuhema juu juu. Hali hii huzitokea roho zinazozurula.
Labda utapata swali, vipi wanaolala na kutokuamka kabisa?, je hawa hwa wana KUFA, FARIKI au WANAAGA DUNIA? Hawa hawapo kwenye kundi lolote kati ya haya matatu. Kifupi ni kuwa hawa ni watu ambao wamepatwa na 'ajali tu' yaani hakukuwa na taarifa yoyote kati ya roho na mwili.
Huo ndio utofauti angu wa mambo haya matatu. Kumbuka utofauti wangu huu unaweza kuwa tofauti na mtazamo wako.
Je, unadhani ipo mifano ya kiimani itakayoweza weka mbolea kwenye dhana hii ya utofauti wa KUFA, KUFARIKI na KUAGA DUNIA? Basi usisite ongeza nyama nyama pia.