Huu ni utofauti wangu kati ya KUFA, KUFARIKI na KUAGA DUNIA

Huu ni utofauti wangu kati ya KUFA, KUFARIKI na KUAGA DUNIA

Mgeni wa Jiji

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2017
Posts
9,758
Reaction score
18,431
Wasalaam JF members[emoji1538]

Moja kwa moja kwenye mada, ila kabla sijagusa mhimili wa mada niweke misamiati hii sawa kwa kiwango cha upeo wangu (siyo cha BAKITA)

Tafsiri ya haya maneno:

1. KUFA, binafsi naamini wapo wanadamu wanaokufa na wasiokufa. Kufa kwa tafsiri yangu ni roho kuukimbia mwili kutokana na uharibifu wa ghafla wa mwili utokanao ama na Ajali, Kupigwa, au Majanga asili mfano matetemeko au radi

2. KUFARIKI, hili linakaribiana sana na KUFA ila ni tofauti kimazingira. Hapa pia roho inaukimbia mwili. Ila tofauti hapa huwa si kutokana na uharibifu wa mwili bali hutokana tu na roho kuichoka hali ya mwili. Mara nyingi wanaofariki ni wagonjwa, watu waliopata njaa kali au waliokosa hewa. Yaani vile vitu vinavyoutesa na kuuchosha mwili basi utafariki

3. KUAGA DUNIA, hili kundi ndio linanishangaza kidogo katika tafakari yangu. Hapa inatokea roho inawasiliana moja kwa moja na baadhi ya viungo vya mwili hususa ubongo na kuupa taarifa kuwa sasa roho inaitaji kutoka na kwenda eneo tofauti. Hii ni hali ya bahati sana kutokea kwa mwanadamu. Je, umewahi kusikia watu wakisema "alijua atakufa akawa anatuaga" basi ndio hali hii. Tatizo ni moja tu watu hudhani mtu huyo kafa kumbe hajafa bali ameaga dunia.

Watu wa kundi hili mara nyingi huwa ni wazee au hata vijana na watoto, na hasa kwa uzoefu na fikra yangu huwa halii hii huwapata wale watu wakorofi na wenye misimamo yao.

POINT YA ZIADA:

KULALA: Umewahi kusikia habari za Yesu kristu au Nabii Issaa za kuwaambia waombolezaji kuwa "mtoto hajafa amelala tu!". Umekumbuka ee!, basi nikuongezee jambo la ziada KULALA ni hali ya roho kutoka ndani ya mwili na kuanza kuushangaa ama mwili wenyewe au mazingira yaliyoizunguka au huamua tu kutembea tembea huku na kule na hapa ndipo watu huota ndoto za ajabu kama kukimbizwa au kutaka kutokewa na jambo fulani kisha ghafla huzinduka toka usingizini na kuhema juu juu. Hali hii huzitokea roho zinazozurula.

Labda utapata swali, vipi wanaolala na kutokuamka kabisa?, je hawa hwa wana KUFA, FARIKI au WANAAGA DUNIA? Hawa hawapo kwenye kundi lolote kati ya haya matatu. Kifupi ni kuwa hawa ni watu ambao wamepatwa na 'ajali tu' yaani hakukuwa na taarifa yoyote kati ya roho na mwili.

Huo ndio utofauti angu wa mambo haya matatu. Kumbuka utofauti wangu huu unaweza kuwa tofauti na mtazamo wako.

Je, unadhani ipo mifano ya kiimani itakayoweza weka mbolea kwenye dhana hii ya utofauti wa KUFA, KUFARIKI na KUAGA DUNIA? Basi usisite ongeza nyama nyama pia.
 
Kuna wengine wanakata roho, Kuna wanaopumzika na kuna wanaopotea, Mwiaho kabisa kuna wanodacha,kuna wanaoleft na kunawanoburiani
 
Mkuu hapo kwenye "kulala" ambapo roho huuacha mwili na kuzurura au kuushangaa mwili ambapo ndio umesema mtu huwa kama anaota ndoto. Vipi roho wakati inataka kurudi kwenye mwili ikapotea njia na kushindwa kufika nyumbani (mwilini)?

Je ndio hapo hukutwa mtu kafia usingizini?

Kama ndio ina maana huyu mtu aliefia usingizini roho yake bado inaweza kuwa ipo katika harakati za kutafuta njia ya kurudi mwilini ili huyo mtu arejelewe na uhai, si ndivyo? Sasa kwa sisi ma sheikh mtu anakufa saa kumi usiku usingizini tunamzika alasiri huoni labda roho yake inakuwa bado inazurura na labda tumemfukia mtu mzima?

Je kuna mahali popote roho inaweza kuulizia njia ya kurudi kwenye mwili pale inapotokea imepotea njia kwenye kururuza kwake? Maana ujue uswahilini kuna vichochoro vingi sana.
 
Kifo ni kifo tu mkuu sema style za kufa ndio zipo nyingi
Ukishakata kamba unafanana na wote wenye kuitwa marehemu
 
Mkuu hapo kwenye "kulala" ambapo roho huuacha mwili na kuzurura au kuushangaa mwili ambapo ndio umesema mtu huwa kama anaota ndoto. Vipi roho wakati inataka kurudi kwenye mwili ikapotea njia na kushindwa kufika nyumbani (mwilini)?

Je ndio hapo hukutwa mtu kafia usingizini?

Kama ndio ina maana huyu mtu aliefia usingizini roho yake bado inaweza kuwa ipo katika harakati za kutafuta njia ya kurudi mwilini ili huyo mtu arejelewe na uhai, si ndivyo? Sasa kwa sisi ma sheikh mtu anakufa saa kumi usiku usingizini tunamzika alasiri huoni labda roho yake inakuwa bado inazurura na labda tumemfukia mtu mzima?

Je kuna mahali popote roho inaweza kuulizia njia ya kurudi kwenye mwili pale inapotokea imepotea njia kwenye kururuza kwake? Maana ujue uswahilini kuna vichochoro vingi sana.

Mkuu si unaujua usingizi wa fofofo, hivi hujawahi kusikia habari za watu kuzikwa wakiwa bado hai hii huwa sababu pia.

Kwa wanaokunywa sumu huwa wanafariki ila wanaojinyonga huwa wanakufa mkuu sababu ni moja kujinyonga mwili huwa unaharibiwa na kunywa sumu hadi mtu afe mwili huwa unachoka sawa na wagonjwa wengine. Ukiangalia vizuri utagundua Mtu aliyefariki kwa sumu hana tofauti na mtu aliyefariki kwa ugonjwa.

Bahati mbaya sana bado sijawa na hakika kama kuna mahali roho huweza kuulizia ikipotea. Ila nadhani ipo.

Hivi umewahi kusikia hmtu akisema aliamka asubuhi lakini hakuna kiungo kilichoweza kufanya kazi yaani alihisi kama ndio anakata moto hivi, basi pale huwa ni roho inataka kurudi kwenye mwili ila imesahau njia ya kuingilia.

Kumbuka nyumba ya roho ni fuvu la kichwa na milango ya roho kurudi mwilini ni matundu yote yaliyo kichwani. Sasa ikitokea roho ikatumia maeneo mengine ya mwili kurudi ndani ya mwili hapo ndipo hali hiyo hutokea.

Mambo ni mengi ila machache ni hayo mkuu.
 
Kifo ni kifo tu mkuu sema style za kufa ndio zipo nyingi
Ukishakata kamba unafanana na wote wenye kuitwa marehemu

Amini usiamini marehemu hawafanani mkuu. Kisema marehemu wanafanana ni sawa na kusema kuwa udongo unafanana simply kwa sababu ni udongo.
 
Amini usiamini marehemu hawafanani mkuu. Kisema marehemu wanafanana ni sawa na kusema kuwa udongo unafanana simply kwa sababu ni udongo.
Wanafanana nikiwa na maana kumbukumbu lao halipo tena kwao/ubongo wao umeharibika na kuwa maada isiyoweza kutoa sapot yoyote ya kuuendeleza uhai wa mwili husika.

Marehemu wote wapo katika hali ya kutokuwapo na kutokuwepo milele,,,,, yaani mfano wake wapo katika hali ile ya kabla hawajazaliwa

Mwaka 1,500 wewe ulikuwa haupo mahala popote.
Vivyo hivyo ukifa unakuwa haupo mahala popote
Sasa basi, nikisema marehemu wote wapo katika hali sawa namaanisha data yao yote haipo mahali popote zaidi ya miili yao kugeuka kuwa mbolea na mwisho kuufikia udongo kamili ambao katika huohuo udongo ndipo waliopatikana

Ni kama mbegu ya mmea tu kwamba ukishaila haiwezekani kuwepo tena, au ikishaota na kuwa mmea lazima ipitie hatua zake za ukuaji hadi kufikia mmea huo kufa na kuharibika. Haiwezekani kuwepo tena kwa namna ileile hata kwa utaalamu wa namna gani.

KADHALIKA NA KWA BINADAMU NI HIVYO KWAMBA, MBEGU ILIYOKUTOKEZA WEWE HAIWEZEKANI KUJIRUDIA KWA NAMNA ILEILE HATA UTUMIKE UTAALAMU WA HALI YA JUU
 
Hii sioni kama inahitaji maelezo kwa mswahili, hasa Mtanzania.

Mswahili Mtanzania, ukimueleza fulani, ameaaga Dunia, fulani ametutoka, fulani, ametangulia mbele haki, fulani, amekufa, fulani amekata roho, fulani hatuko nae nae Duniani.
Kinachofuata kwa aneepewa taarifa anaelewa kilichotokea, hivyo atasikitika ama atafurahi, itategema.
 
Mkuu hapo kwenye "kulala" ambapo roho huuacha mwili na kuzurura au kuushangaa mwili ambapo ndio umesema mtu huwa kama anaota ndoto. Vipi roho wakati inataka kurudi kwenye mwili ikapotea njia na kushindwa kufika nyumbani (mwilini)?

Je ndio hapo hukutwa mtu kafia usingizini?

Kama ndio ina maana huyu mtu aliefia usingizini roho yake bado inaweza kuwa ipo katika harakati za kutafuta njia ya kurudi mwilini ili huyo mtu arejelewe na uhai, si ndivyo? Sasa kwa sisi ma sheikh mtu anakufa saa kumi usiku usingizini tunamzika alasiri huoni labda roho yake inakuwa bado inazurura na labda tumemfukia mtu mzima?

Je kuna mahali popote roho inaweza kuulizia njia ya kurudi kwenye mwili pale inapotokea imepotea njia kwenye kururuza kwake? Maana ujue uswahilini kuna vichochoro vingi sana.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] et kuulizia njia hahahah
 
Mkuu hapo kwenye "kulala" ambapo roho huuacha mwili na kuzurura au kuushangaa mwili ambapo ndio umesema mtu huwa kama anaota ndoto. Vipi roho wakati inataka kurudi kwenye mwili ikapotea njia na kushindwa kufika nyumbani (mwilini)?

Je ndio hapo hukutwa mtu kafia usingizini?

Kama ndio ina maana huyu mtu aliefia usingizini roho yake bado inaweza kuwa ipo katika harakati za kutafuta njia ya kurudi mwilini ili huyo mtu arejelewe na uhai, si ndivyo? Sasa kwa sisi ma sheikh mtu anakufa saa kumi usiku usingizini tunamzika alasiri huoni labda roho yake inakuwa bado inazurura na labda tumemfukia mtu mzima?

Je kuna mahali popote roho inaweza kuulizia njia ya kurudi kwenye mwili pale inapotokea imepotea njia kwenye kururuza kwake? Maana ujue uswahilini kuna vichochoro vingi sana.
Mkuu umemalizaaa!!!
 
Nikipanda rocket kwenda sayari nyingine hapo nakuwa sijaaga Dunia?
 
Mkuu hapo kwenye "kulala" ambapo roho huuacha mwili na kuzurura au kuushangaa mwili ambapo ndio umesema mtu huwa kama anaota ndoto. Vipi roho wakati inataka kurudi kwenye mwili ikapotea njia na kushindwa kufika nyumbani (mwilini)?

Je ndio hapo hukutwa mtu kafia usingizini?

Kama ndio ina maana huyu mtu aliefia usingizini roho yake bado inaweza kuwa ipo katika harakati za kutafuta njia ya kurudi mwilini ili huyo mtu arejelewe na uhai, si ndivyo? Sasa kwa sisi ma sheikh mtu anakufa saa kumi usiku usingizini tunamzika alasiri huoni labda roho yake inakuwa bado inazurura na labda tumemfukia mtu mzima?

Je kuna mahali popote roho inaweza kuulizia njia ya kurudi kwenye mwili pale inapotokea imepotea njia kwenye kururuza kwake? Maana ujue uswahilini kuna vichochoro vingi sana.
Hahaaaaaa
 
Mkuu ahsante sana kwa kushare nasi kuhusu kifo. Dhana ya kifo imeelezewa kwa namna mbalimbali katika tamaduni, watu au jamii mbalimbali.
Kwa tafsiri yangu inaonekana una uelewa mzuri kuhusu dhana ya kifo na inawezekana kuna source ya ideas zako.
Hivyo, kama hutojali naomba utusaidie vitabu ulivyopitia hasa vinavyoelezea kuhusu kifo, itakuwa vyema.
Natanguliza shukrani.

Hapana tatizo mkuu baadhi ni The four agreements by Don Ruiz, The Vortex kimeandikwa na Jerry Hicky na Esther, Invisible acts of power by Caroline, Bible na Quran pia mkuu huwa nazipitia pamoja ila kikubwa zaidi huwa nasoma sana articles na posts kwenye forum tofauti tofauti hasa za Quora.
 
Nikipanda rocket kwenda sayari nyingine hapo nakuwa sijaaga Dunia?

Mkuu kuaga dunia ni roho kutoka ndani ya mwili na kuamua kutokurudi tena. Sasa ukienda mfano Mars bado hujaaga dunia hapo kwa muktadha husika
 
Back
Top Bottom