Hammaz
JF-Expert Member
- May 16, 2018
- 6,607
- 14,076
Binafsi neno/msamiati KUFA nalitafsiri ni hali ya "umaalumu" ya kushindwa kufanya kazi kabisa, na miale ya tafsiri hii( kwangu ni mipana). Inahusisha viumbe vilivyo hai na vile visivyo hai( vilivyotengenezwa kwa kukamilisha kazi "maalumu")
Mfano1: kwa viumbe hai unaposema ame'KUFA' una maana ya kwamba zile biological function zote(umaalumu) zinazomfanya aendelee kuwa hai zimeshindwa kabisa kuendelea kufanya hiyo kazi.
Mfano2: kwa viumbe visivyo hai( hapa nazungumzia vitu vya kuyengeneza) kama vitu vya electronics na vinginevyo vilivyotengenezwa kwa kufanya kazi " maalumu" navyo, vikishindwa kufanya kazi yake kabisa iliyokusudiwa; binafsi natafsiri ya kwamba kime'KUFA'
Kwa mantiki hiyo, KUFA huwa nalitafsiri ni kushindwa kabisa kwa kufanya kazi "maalumu" kiwe kwa kiumbe hai au vitu vinavyotengenezwa kwa kazi husika. Kwa hiyo, hili neno linatumika kote kote kama mifano ya juu inavyoonesha.
Tukija kwenye KUFARIKI+KUAGA DUNIA kwa ufahamu wangu mdogo ni maneno yenye maana moja tena yenye kubagua, na kubagua kwake ni kwa viumbe hai tu na si viumbe hai vyote. Bali ni mmoja tu naye ni binadamu na limempa hadhi ya kumchagua yeye tu, kwa sababu binadamu ana ule upekee kwa viumbe hai kwa ujumla(ijapokuwa maneno yenyewe ni yenye kuleta majonzi). Kwa sababu huwezi kusema Kuku amefariki au ameaga Dunia. Ni kweli italeta maana lakini tutasema sentensi imekosa ile " Collocation " Vilevile inaonesha utajiri wa Lugha wa kuwa na maneno/misamiati mingi yenye kurejelea maana moja.
KUFARIKI/KUAGA DUNIA ni kanuni na nidhamu ya maumbile ya mwanadamu kufikia utamati wa mawasiliano ya kiroho, kimwili na kiakili. Kwa sababu tupo kwenye Sayari Dunia ndipo likapatikana KUAGA/ KUFARIKI DUNIA. Kama tungekuwa sayari ya Krypton basi tungesema KUAGA/KUFARIKI KRYPTON.
Additional point:
Ukija kiistilahi KUFARIKI kumetokana na neno "al faraqa" la kiarabu kwa maana ya tengana au kutengana. Kwa kiswahili linaongezewa nyama na kulingana na sentensi husika. Mfano; usilete m'faraka'no kwa maana usilete utengano. Kufariki ni Faraqa ukijumlisha Dunia inakuwa Al faruq bayna dduniya( kutengana na dunia) Waswahili wanasema kafariki Dunia.
Ni mtazamo wangu, ni ruhusa kunisahihisha.
Mfano1: kwa viumbe hai unaposema ame'KUFA' una maana ya kwamba zile biological function zote(umaalumu) zinazomfanya aendelee kuwa hai zimeshindwa kabisa kuendelea kufanya hiyo kazi.
Mfano2: kwa viumbe visivyo hai( hapa nazungumzia vitu vya kuyengeneza) kama vitu vya electronics na vinginevyo vilivyotengenezwa kwa kufanya kazi " maalumu" navyo, vikishindwa kufanya kazi yake kabisa iliyokusudiwa; binafsi natafsiri ya kwamba kime'KUFA'
Kwa mantiki hiyo, KUFA huwa nalitafsiri ni kushindwa kabisa kwa kufanya kazi "maalumu" kiwe kwa kiumbe hai au vitu vinavyotengenezwa kwa kazi husika. Kwa hiyo, hili neno linatumika kote kote kama mifano ya juu inavyoonesha.
Tukija kwenye KUFARIKI+KUAGA DUNIA kwa ufahamu wangu mdogo ni maneno yenye maana moja tena yenye kubagua, na kubagua kwake ni kwa viumbe hai tu na si viumbe hai vyote. Bali ni mmoja tu naye ni binadamu na limempa hadhi ya kumchagua yeye tu, kwa sababu binadamu ana ule upekee kwa viumbe hai kwa ujumla(ijapokuwa maneno yenyewe ni yenye kuleta majonzi). Kwa sababu huwezi kusema Kuku amefariki au ameaga Dunia. Ni kweli italeta maana lakini tutasema sentensi imekosa ile " Collocation " Vilevile inaonesha utajiri wa Lugha wa kuwa na maneno/misamiati mingi yenye kurejelea maana moja.
KUFARIKI/KUAGA DUNIA ni kanuni na nidhamu ya maumbile ya mwanadamu kufikia utamati wa mawasiliano ya kiroho, kimwili na kiakili. Kwa sababu tupo kwenye Sayari Dunia ndipo likapatikana KUAGA/ KUFARIKI DUNIA. Kama tungekuwa sayari ya Krypton basi tungesema KUAGA/KUFARIKI KRYPTON.
Additional point:
Ukija kiistilahi KUFARIKI kumetokana na neno "al faraqa" la kiarabu kwa maana ya tengana au kutengana. Kwa kiswahili linaongezewa nyama na kulingana na sentensi husika. Mfano; usilete m'faraka'no kwa maana usilete utengano. Kufariki ni Faraqa ukijumlisha Dunia inakuwa Al faruq bayna dduniya( kutengana na dunia) Waswahili wanasema kafariki Dunia.
Ni mtazamo wangu, ni ruhusa kunisahihisha.