BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,165
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
NakuonaDaah nimetengeneza vibanda vyangu vya kujifukizia
Naona hasara inaninyemelea
Ule mtambo wa kujifukiza vipi tena?
Hivi watu mkoje? Kwa nini mnalazimisha kuwa mkuu wetu amefariki kwa corona wakati tumeelezwa na viongozi wetu kuwa amefariki kutokana na ugonjwa wa moyo.Binafsi nilishangaa Sana kusikia Katibu Mkuu Kiongozi, na Makamu wa Rais Zanzibar wamefariki kwa changamoto ya upumuaji (Korona in advance) viongozi wa juu kabisa wa kiserikali.
Nilishangaa pia jinsi misiba ilivyoendeshwa bila tahadhari yyte. Kwa uchungu nilihoji pia usalama wa Rais, kama walio karbu na Rais wanakufa Kwa huu ugonjwa basi Kwa vyovyote vile Raisi hayupo salama na nikasema itakuwa aibu ya karne kwa Raisi kufa kwa ugonjwa huo, sababu niliona kama tunaufanyia mzaha.
Bahati mbaya Jambo hili limejitokeza, so sad Kwa kweli na ni aibu, Dunia yote inapambana angalau kuweka mikakati madhubuti ya kujikinga, hata nchi zinazopinga chanjo ya Korona zimejiwekea utaratibu maalum wa kujikinga na mamlaka husika zinausimamia.
Sisi tunapinga chanjo lakin hatuna utaratibu wala mikakati madhubuti ya kujikinga, ni hatari sana hii. Mungu yupo, lakni kamwe Maombi hayakuwekwa kuwa mahali pa wajibu. Mungu hawezi laumiwa kwa uzembe wa mhusika. Kifo cha Rais kinaweza kikafanya tukajisahau tena lakini viongozi wengi wataendelea kushuka kaburini kama hli halitafanyiwa kazi.
Ifikie hatua hata viongozi mjithamini pia, na niseme Tu wazi, mamlaka za juu pamoja na wizara ya Afya kaeni haraka kuangalia namna ya kuipeleka nchi Kati Kati ya janga hili, inawezekana ikawa too late lakn bado kuna nafasi ya kufanya. Acheni mzaha kabisa, na bado viongozi wengi na wananchi hasa wazee ambao wapo relaxed, wapo hatarini na huu ugonjwa tukiendelea kuuchekea. Msiogope Hali ya uchumi wa nchi. majanga kama haya hubadirisha mkondo wa maisha hii ipo wazi watu watajishape tuu mbali na Gharama itakayojitokeza.
Nimalizie Kwa kusema viongozi wa juu wa hii nchi, tunaomba muiongoze nchi kwa utaratibu wa katiba na Sheria, muache kuiendesha nchi Kwa pressure ya mashambulizi ya matamko ya watu walioko nje akina Kigogo na wengine.
Ni aibu jaman kuutangazia uma ghafla kuwa Raisi amefariki, tena kwa ugonjwa ,whatever ni ugonjwa gani. Kwa nini hamkutangaza alipougua. Hata kusema tu kuwa amelazwa anaumwa ilitosha kabisa, hata kama mngechelewa kutangaza msiba wake watu wasingekuwa surprised. Mliwanyima haki wananchi; wenye kumuombea wangemuombea, badala yake mnasema Rais yupo salama anachapa kazi kweli? Makawakamata vijana wa watu waliopata taarifa ya kwamba Rais hayupo poa na kweli kumbe vijana walikuwa sahihi.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Africa 🚶🚶🚶🚶
Wewe umeishia darasa la ngapi? korona ni second hand disease , inamalizia penye tatizo ..... Mna vichwa vigumu Sana , na Vifo ndo vitaendelea kuwa Gharama ya ubishiHivi watu mkoje? Kwa nini mnalazimisha kuwa mkuu wetu amefariki kwa corona wakati tumeelezwa na viongozi wetu kuwa amefariki kutokana na ugonjwa wa moyo.
"Watu wenye magonjwa mengine hasa yasiyo ya kuambukiza wapo katika hatari zaidi kuathirika na UVIKO" what's the coincedence?Kufa ni kufa babu. Hizo nyingine ni kuongeza complications na kuwapanikisha wananchi.
So far hakuna ushahidi kuwa kafa kwa UVIKO. Naomba nisieleweke vibaya, UVIKO upo ila sio kila anaekufa basi ndo umemuua unless kuna ushahidi unaoshikika.
Watu wasife kwa magonjwa mengine kwa kuwa kuna UVIKO??[emoji2369][emoji2369]