Vien
JF-Expert Member
- Mar 6, 2020
- 6,585
- 10,363
Mkuu umeeleweka vilivyo .Leseni zote za Class A zinatoka online na Class B kwa wilaya ya ILALA nazo zinatoka online unaenda kwenye website Home - TNBP unajisajili unapata username na hiyo password ambayoo email uliyoiweka ndio inakuwa username.
Click kwenye tab ya service then Business license. Baada ya hapo kuna mambo ya kujibu na kuload vitu muhimu kama ni mpya Mkataba wa Pango, Kitambulisho , kwa Kampuni memarts na hiyo tax clearance.
Unajibiwa haraka na baada ya siku moja au mbili unaletewa control number ukilipa baada ya dakika 15 mpaka nusu saa leseni inakuwa tayari unaprint unaweka kwenye biashara yako. Unachangamoto yoyote kwenye hili leta issue tusaidiane.
One love