DOKEZO Huu utaratibu wa kuzuia maiti Hospitali ya Muhimbili kisa nduguze wanadaiwa hela ya matibabu utazamwe vizuri

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Jibu jepesi mlitakiwa muwaambie basi bakieni nayo hiyo Maiti sisi tunaenda kumaliza msiba.
Wakibaki nayo baada ya muda wanawapa "Site" maiti wanaenda kuzika. Dawa ni kulipa tu. Mtu akifariki haiondoi ukweli gharama zimetumika na ndio maana Serikali yetu nzuri na Bunge letu tukufu wamepitisha Sheria ya Bima ya Afya ya Lazima kwa kila Mtanzania. Kwa wanafunzi ni shilingi 50,400/= tu! Tuhimizane tukakate bima za afya tuhepuke aibu na kusubiri huruma!
 
Wakizika City si imeisha hiyo
 
Kimsingi huu utaratibu ni wa kijinga. Na hivyo unatakiwa uondolewe mara moja.
Inakiwa Mwili Huu Wa Nyama Unapokosa Pumzi
Kwa Maana Umekufa Wapewe Ndugu
Mfano Waislam Kwa Imani Yako Mwili Hautakiwi Kuwekwa Dawa
 
Kwanini maiti idaiwe na wakati huduma hospitali iliyotoa imeshindikana kumponya mgonjwa mpaka amefariki? Huu nao ni uhuni tu. Natamani hili liangaliwe upya litungiwe sheria ya hakuna kulipia huduma ambayo haijaleta matokeo chanya ikiwemo na hii ya matibabu ili watoa huduma wawe makini na kazi zao kuhakikisha wanaleta matokeo chanya.

Nimeshuhudia uzembe wa madaktari ukisababisha mauti kwa mgonjwa wa ajili alipopelekwa hospitalini baada ya kupata ajali daktari kamshona jeraha la kichwa na baada ya muda hali ikazidi kuwa mbaya kumchunguza kumbe kuna damu imevilia kwenye kichwa ikaenda mpaka kwenye ubongo hatimae kusababisha mauti ya mgonjwa, hivi kwa scenario kama hii hawa watoa huduma wa hivi wanastahili kulipwa? Wanalipwa kwa lipi sasa na wakati wamesababisha hasara kubwa sana.
 
kuna hospital hata ukienda kupima malaria, unaweza usirudi nyumbani mzima,....
 
Kalipeni tushachoka mngemtibia nyumban
 
Wanaonesha jinsi wanavyopenda kuangalia maiti.Upendo ulioje!
 
Ondokeni na special hire nendeni wote ofisi ya waziri WA afya
Mkimkosaa ndenden ofisi ya waziri mkuu
 
Ni nani Mkurugenzi wa hiyo Hospitali?
WAISIHARAMU NDIYO WALILETA HUO UPUMBAVU KWENYE HOSPITALI ZA SERIKALI...HUWA NIKISEMA AWA WAPUMBAVU AWAFAI KUWA VIONGOZI ...WAPUUZI WANAPINGA
 
AS PER ATTACHMENTS
PLS ASSIST
TUNAOMBA MH RAISI
HON WAZIRI WA AFYA
WABUNGE WA DAR
MKUU WA MKOA
TUNAOMBA HII MAITI IACHILIWE PLS INAZIKWE KWA HESHIMA

NDUGU ZETU HAWA WANATESEKA SANA WANANMAUMIVU YA MWENDANZAKE BADO HATA KUZIKA WANAZUILIWA

MUNGU AWABARIKI
 

Attachments

  • Screenshot_20241211-110602.jpg
    332 KB · Views: 1
Ondokeni na special hire nendeni wote ofisi ya waziri WA afya
Mkimkosaa ndenden ofisi ya waziri mkuu
Ombeeni ama pigien itv
Eatv
Na wengineo waje mlipo hio MAITI mtapewa na gariyakusafirisha
 
Sasa wametumia gharama kutibu lakin
 
Inahuzunishaaa sanaa sanaa Mungu TUSAIDIE mbaya ukutrmzaziwakoo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…