Huu uzi ni maalumu kwa ajili ya kujadili uwekezaji ambao ni rafiki kwa Waajiriwa

Mimi nimefikisha 70m nimeitoa mwezi uliopita. Ila nitaendelea tena. Ni sehemu ya kuhifadhi fedha huku ukiendelea kudunduliza ila siyo sehemu ya kutegemea faida kubwa.
Hongera mkuu, mie ndio nimeanza upya kudunduliza,sasa nina milion 5... kuna jambo nataka kufanyia hii pesa, lengo likitimia naitoa nafanyia mambo yangu alafu naanza upya.
 
Endelea kukaza ndugu yangu uko kwenye right path cha msingi zidisha nidhamu ya pesa tuu.Biashara kuwa ngumu ni mapito tuu mambo yatakuwa sawa cha msingi usifanye biashara ya bahati nasibu au inshaallah Mungu atafanya wepesi.Kuwa mbunifu na researcher mzuri kuhusu biashara unayoifanya namna ya kuiboresha na kupata wateja wengi zaidi.
 
800k mbona kubwa kabisa, au kwakua mie sina hela.....
 
Ukiwekeza 50m unapata ngapi kwa mwaka mmmoja
 
Na hii taasisi ni ya nani na security yake ipo vipi isije kuwa mambo kama ya deci ikafilisika tuaachwa masikini
Sio taasisi ya mtu, iko chini ya serikali kupitia wizara ya Fedha. Ina miaka mingi sana hakuna malalamiko. Wana ofisi kwenye miji mikubwa yote,Labda uhofie vitu vingine lakini sio usalama wa pesa.
 
Sio taasisi ya mtu, iko chini ya serikali kupitia wizara ya Fedha. Ina miaka mingi sana hakuna malalamiko. Wana ofisi kwenye miji mikubwa yote,Labda uhofie vitu vingine lakini sio usalama wa pesa.
Ok je naweza kutoa mtaji wangu wakati wowote nikihitaji au kuna utaratibu gani?
 
Ok je naweza kutoa mtaji wangu wakati wowote nikihitaji au kuna utaratibu gani?
Unatoa muda wowote unaotaka,ila process inatumia siku tatu za kazi...ukiomba jumatatu jumatano unapata hela yako.
 
kwenye biashara unafanya maamuzi ya kuanza, hayo mengine utajifunzia mbele kwa mbele mangi. Chenye uhakika chini ya hili jua ni kifo tu...vingine ni leap of faith.

Kama unapenda uhakika usiguse biashara, utakuja kufungua nyuzi za kulalamika tu huku
 
Nimeipenda hyo usiibe bila kujua sheria, sasa ww nenda kichwakichwa uone😂
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…