Huu uzi ni maalumu kwa ajili ya kujadili uwekezaji ambao ni rafiki kwa Waajiriwa

Huu uzi ni maalumu kwa ajili ya kujadili uwekezaji ambao ni rafiki kwa Waajiriwa

Mimi nimefikisha 70m nimeitoa mwezi uliopita. Ila nitaendelea tena. Ni sehemu ya kuhifadhi fedha huku ukiendelea kudunduliza ila siyo sehemu ya kutegemea faida kubwa.
Hongera mkuu, mie ndio nimeanza upya kudunduliza,sasa nina milion 5... kuna jambo nataka kufanyia hii pesa, lengo likitimia naitoa nafanyia mambo yangu alafu naanza upya.
 
Mwaka jana biashara ilipamba moto nikaona bora nikomae na biashara niachane na mambo za kuajiriwa

Mwaka huu upepo umegeuka biashara ngumu kuliko jiwe hadi natamani ajira. Nishaurini wakuu

Ninaingiza net profit ya 800k kwa mwezi(hapo nimetoa gharama zote) niendelee kukaza au niajiriwe?
Endelea kukaza ndugu yangu uko kwenye right path cha msingi zidisha nidhamu ya pesa tuu.Biashara kuwa ngumu ni mapito tuu mambo yatakuwa sawa cha msingi usifanye biashara ya bahati nasibu au inshaallah Mungu atafanya wepesi.Kuwa mbunifu na researcher mzuri kuhusu biashara unayoifanya namna ya kuiboresha na kupata wateja wengi zaidi.
 
Mwaka jana biashara ilipamba moto nikaona bora nikomae na biashara niachane na mambo za kuajiriwa

Mwaka huu upepo umegeuka biashara ngumu kuliko jiwe hadi natamani ajira. Nishaurini wakuu

Ninaingiza net profit ya 800k kwa mwezi(hapo nimetoa gharama zote) niendelee kukaza au niajiriwe?
800k mbona kubwa kabisa, au kwakua mie sina hela.....
 
Maisha ya utumishi ni mafupi hivyo ni heri kujiandaa na maisha ya kustaafu mapema.

Kipato vya wafanyakazi wengi ni kidogo sana hivyo kuna ulazima kuwa na kipato cha ziada.

Changamoto ya wafanyakazi wengi ni muda wa kufanya biashara na projects kama kilimo na ufugaji haupo na risk ya kupoteza hela zako ni kubwa kuliko kupata faida sababu ya usimamizi duni.

Huu uzi ni maalumu kwa ajili ya kujadili uwekezaji ambao ni rafiki kwa mfanyakazi, hauhitaji muda mwingi,risk ya kupoteza pesa sio kubwa na wenye faida ya kueleweka.

Naongelea vitu kama UTT, treasury bills na Bonds, Hisa kwenye makampuni ya kitaifa na kimataifa na fursa nyingine nyingi na nzuri ambazo mfanyakazi anaweza kujiingiza ili kutunza na kuongeza kipato chake.

Nafahamu humu ndani kuna wataalamu wa mambo ya uchumi na uwekezaji, kuna wawekezaji wakubwa na wadogo, kuna matajiri wa kutosha, njooni mtushike mkono tujue namna gani tunaweza kukuza vipato vyetu vidogo na kuingia kwenye utajiri.
Karibuni.
Ukiwekeza 50m unapata ngapi kwa mwaka mmmoja
 
Na hii taasisi ni ya nani na security yake ipo vipi isije kuwa mambo kama ya deci ikafilisika tuaachwa masikini
Sio taasisi ya mtu, iko chini ya serikali kupitia wizara ya Fedha. Ina miaka mingi sana hakuna malalamiko. Wana ofisi kwenye miji mikubwa yote,Labda uhofie vitu vingine lakini sio usalama wa pesa.
 
Sio taasisi ya mtu, iko chini ya serikali kupitia wizara ya Fedha. Ina miaka mingi sana hakuna malalamiko. Wana ofisi kwenye miji mikubwa yote,Labda uhofie vitu vingine lakini sio usalama wa pesa.
Ok je naweza kutoa mtaji wangu wakati wowote nikihitaji au kuna utaratibu gani?
 
Ok je naweza kutoa mtaji wangu wakati wowote nikihitaji au kuna utaratibu gani?
Unatoa muda wowote unaotaka,ila process inatumia siku tatu za kazi...ukiomba jumatatu jumatano unapata hela yako.
 
kwenye biashara unafanya maamuzi ya kuanza, hayo mengine utajifunzia mbele kwa mbele mangi. Chenye uhakika chini ya hili jua ni kifo tu...vingine ni leap of faith.

Kama unapenda uhakika usiguse biashara, utakuja kufungua nyuzi za kulalamika tu huku
 
We elewa WALIPITA NAZO.

Ngoja kwanza ipite bahati, wanasema bahati ni fursa ilikutana na maandalizi.
Hapa silaha zishaandaliwa, inasubiriwa vita tuu..!!!

Sheria za nchi hii lope hole ni nyingii, IKO SIKU.
Ndio itakuwa mwisho wa Ajira za CCM.

Nataka kuwa Tajiri na biashara ndio kimbilio sahihi..!!!

NB.
Usiibe bila kujua SHERIA.
Usiache ushahidi..!!
#YNWA
Nimeipenda hyo usiibe bila kujua sheria, sasa ww nenda kichwakichwa uone😂
 
Back
Top Bottom