Huu uzi ni maalumu kwa ajili ya kujadili uwekezaji ambao ni rafiki kwa Waajiriwa

Huu uzi ni maalumu kwa ajili ya kujadili uwekezaji ambao ni rafiki kwa Waajiriwa

clinician

JF-Expert Member
Joined
Mar 5, 2014
Posts
2,098
Reaction score
4,926
Maisha ya utumishi ni mafupi hivyo ni heri kujiandaa na maisha ya kustaafu mapema.

Kipato vya wafanyakazi wengi ni kidogo sana hivyo kuna ulazima kuwa na kipato cha ziada.

Changamoto ya wafanyakazi wengi ni muda wa kufanya biashara na projects kama kilimo na ufugaji haupo na risk ya kupoteza hela zako ni kubwa kuliko kupata faida sababu ya usimamizi duni.

Huu uzi ni maalumu kwa ajili ya kujadili uwekezaji ambao ni rafiki kwa mfanyakazi, hauhitaji muda mwingi,risk ya kupoteza pesa sio kubwa na wenye faida ya kueleweka.

Naongelea vitu kama UTT, treasury bills na Bonds, Hisa kwenye makampuni ya kitaifa na kimataifa na fursa nyingine nyingi na nzuri ambazo mfanyakazi anaweza kujiingiza ili kutunza na kuongeza kipato chake.

Nafahamu humu ndani kuna wataalamu wa mambo ya uchumi na uwekezaji, kuna wawekezaji wakubwa na wadogo, kuna matajiri wa kutosha, njooni mtushike mkono tujue namna gani tunaweza kukuza vipato vyetu vidogo na kuingia kwenye utajiri.
Karibuni.
 
Kuna watu wana hisa kwenye kampuni za kimataifa kama Amazon,Google,Apple Cocacola etc,natamani sana kujua uwekezaji huko upoje,Kuna Daktari bingwa mmoja aliniambia yeye alinunua hisa za kampuni ya mafuta wakati anasoma Russia na gawio alikuwa anapata mpaka vita ilipokuja kuharibu mambo.
 
Ufugaji utakulipa zaidi
Hii ishu ya ufugaji niliwaza kuifanya kwa large scale,Nitafute eneo kubwa huku mkoani Mara,nijenge mazizi na kijumba cha mchungaji,alafu niweke ng´ombe,mbuzi na kondoo. Ila ishu ya usalama wa hiyo mifugo ndio ilinipa wasiwasi maana inabidi ufuge eneo ambalo halina watu wengi,porini huko kwenye majani mengi.
 
Back
Top Bottom