madeinmusoma
JF-Expert Member
- Jan 7, 2014
- 324
- 387
Umeenda nyumbani kwa mtu, halafu unakutana na toto sumbufu balaa! Hamjawahi kuonana, lakini limeshakuzoea...
Unakuja mwenyewe labda umechomekea shati, nini!! Linaanza kukurukia rukia, mara linakuvuta shati mpaka linachomoka... Mama yake anabaki, "we Junior hebu muache uncle...."
Basi unafika, unakaa sebuleni, linaanza kukusumbua. Mara likupige kibao cha kushitukiza ulikuwa unaangalia zako mbele kwenye TV, mara linakudandia mapajani... Unajibalaguza kuliambia, "haya nenda kwa mama.." Linakutemea mate usoni na mama yake anacheka tu na kukwambia, "Nakwambia leo utakoma!" (Mimi huwa nayafinya kisiri siri). [emoji12][emoji12][emoji12]
Sasa unakuta umeletewa chai na maandazi, toto lipo mbele yako linakuangalia, linataka kuokota andazi. Kwakuwa unaona mikono yake michafu, unaamua kulimegea kipande... Halitaki, linataka zima...! Hujakaa vizuri, limemwaga chakula kwa hasira...! [emoji853][emoji853][emoji853]
Masaa yanaenda, kwenye TV muda wa habari lenyewe linataka kuweka cartoon... Linaanza kulia kwa nguvu, mamaake anasema, "Hebu liwekeeni makatuni yake!" Kipindi hicho wewe unatamani lipigwe balaa...! Hujakaa sawa, unashangaa umepigwa na remote kichwani!! Unageuka kwa hasira, unakuta toto linacheka.... [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Ngoja niishie hapa, ila kama upo hivyo na mtoto wako, watu hawapendi..... [emoji36][emoji36][emoji36]
Unakuja mwenyewe labda umechomekea shati, nini!! Linaanza kukurukia rukia, mara linakuvuta shati mpaka linachomoka... Mama yake anabaki, "we Junior hebu muache uncle...."
Basi unafika, unakaa sebuleni, linaanza kukusumbua. Mara likupige kibao cha kushitukiza ulikuwa unaangalia zako mbele kwenye TV, mara linakudandia mapajani... Unajibalaguza kuliambia, "haya nenda kwa mama.." Linakutemea mate usoni na mama yake anacheka tu na kukwambia, "Nakwambia leo utakoma!" (Mimi huwa nayafinya kisiri siri). [emoji12][emoji12][emoji12]
Sasa unakuta umeletewa chai na maandazi, toto lipo mbele yako linakuangalia, linataka kuokota andazi. Kwakuwa unaona mikono yake michafu, unaamua kulimegea kipande... Halitaki, linataka zima...! Hujakaa vizuri, limemwaga chakula kwa hasira...! [emoji853][emoji853][emoji853]
Masaa yanaenda, kwenye TV muda wa habari lenyewe linataka kuweka cartoon... Linaanza kulia kwa nguvu, mamaake anasema, "Hebu liwekeeni makatuni yake!" Kipindi hicho wewe unatamani lipigwe balaa...! Hujakaa sawa, unashangaa umepigwa na remote kichwani!! Unageuka kwa hasira, unakuta toto linacheka.... [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Ngoja niishie hapa, ila kama upo hivyo na mtoto wako, watu hawapendi..... [emoji36][emoji36][emoji36]