Nilikuwa muumini mkubwa sana wa huo msemo wa 'usirudie matapishi' hadi miaka miwili iliyopita.
Mwaka 2015: Moshi, KLM
Kuna mzee mmoja wakati tunakuwa alikuwa ndo kipimo cha ulevi. Ulevi wake ulikithiri kiasi kwamba alifukuzwa kazi. Alikuwa mwalimu mzuri sana. Wale waliokwenda kusoma huko ulaya enzi za Nyerere. Ulevi wake ulimfanya wakaachana na mkewe.
Mwaka 2015 baada ya kuacha pombe kwa miaka miwili walirudiana na mkewe na tulienda kwenye sherehe yao ya kubariki ndoa. Mpaka ninaandika hapa wapo pamoja na ndugu zangu walio Moshi wanasema wanaishi kwa amani.
Mwaka 2017: huku na kule duniani
Hawa ni wazungu. Walioana kijana akiwa 22 na binti 19. Wakazaa watoto. Baadaye wakashindwana tu. Kijana alikuwa mkorofi tu hakumaliza mambo ya ujana anajisemea mwenyewe. Miaka 30 baadaye, huku kila mmoja akiwa na mtoto wa nje, wamerudiana na wanaishi pamoja.
Mimi: 2008
Nilimpenda binti. Baada ya mimi kumaliza chuo nilienda kufanya kazi mbali na yeye. Alianza kuonesha hints za kushindwa akisema alitamani ule ukaribu kwenye mahusiano. Baada ya muda tukaachana. Miezi michache baadaye nikambembeleza turudiane nikiahidi nitajitahidi kuwa nakwenda kumsalimia. Baada ya kufanya safari mbili, akaniacha akisema ananipenda sana lakini anashindwa. Mara hii, alirudi yeye kutaka tujaribu tena.
Nilipima malalamiko yake ya mwanzo na hali tuliyokuwa nayo nikaona hakuna kilichobadilika. Nilikuwa ninampenda nakuhakikishia. 2009/10 ndo enzi facebook imeshika kasi kweli basi nilikuwa nimemuweka huko kote. Ila nilijua najiset up for maumivu tu, kwa kuwa hakuna kilichobadilika katika kilichotufanya tuwe pamoja. Nilifanya maamuzi ya kutokukubaliana na hilo.
In short, hakuna formula kwenye mapenzi. Cha maana ni kuhakikisha kile kilichofanya muachane kimerekebishwa ama la. It may work kama hao wawili it may not work kama mimi, lakini hakuna matapishi kwenye mapenzi. Ndiyo maana watu wanaoa watu waliokwisha kujifungua hata watoto wawili, wanaoa divorcees.
La pili na la muhimu, unapoamua kurudiana naye, hakikisha mnaanza moja. Mara nyingi wengi hukosea hapa na ku-assume walipoachia. Anza moja kwenye urafiki.
Mwisho, kwako
Mama Sabrina, naamini mpaka umeileta hii huku kuna hisia moyoni mwako (unless wewe ni wale wa kuanzisha thread ali mradi uonekane umeanzisha). Do not ignore the feeling, do not fight it...jiridhishe tu uanze moja. Mwisho wa siku tunahitaji kuwa na tumpendaye.