Huyu Baghdad mmh, ameamua kujilipua kama Roma

mpenda pombe

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2010
Posts
1,406
Reaction score
711
Huyu rapper anaekwenda kwa jina BAGHDADY nimesikiza ngoma yake mpya daah..

Dogo ameamua kujilipua kama Roma.. Nimependa uandishi wake, dogo sasa amekua..

Huu ujasiri tumeu miss sana sie mashabiki wa Bongo Hiphop..

Ule ujasiri wa kina Sugu wa enzi zile "Hali halisi" Kalapina "Alikua tayari kukipaka hata kwa bwana Mkapa".

Hongera Baghdady kwa kutokua muoga kama kunguru wapigie tu.
 
Me napenda mziki mzuri wa Bongo Hiphop... Nimewahi leta mada nyingi tu za hawa wasanii wetu...
 
Nimemsikiliza jamaa kaimba kinoma noma big up kwake
 
Wacha ujinga si ukamsifie mwenyewe sasa hapa unamsifia nani wewe?
 
Huu ni ujumbe nimeutoa sehemu wa Baghdad....

...............................


Kituo pekee nilichofanikiwa kuitambulisha #NipeNamba live with intaview ni magic tu peke yake. Radio baadhi imeupokea wimbo na kuutambulisha bila mahojiano kwa sababu mbalimbali. Sasa ninaomba niweke wazi tu ya kuwa vipo vituo vya radio vikubwa tanzania 3 ambavyo viliahidi kunipa intaview ya kuachia wimbo wangu jana kama exclusiv lakini kimoja kiliniomba radhi kwa jana na kusema tufanye leo. Cha pili walidai nilifanya intaview siku chache zilizopita hivyo watatambulisha tu. Na cha tatu walidai watanipa intaview jumamosi hivyo nangojea. Sasa kile kilichosema nitafanya leo nimepigiwa simu na muhusika kwa kusema kwanza wimbo hautachezwa hadi nipeleke wimbo wenye maneno sahihi wakidai ule unaweza kupelekea wakapigwa fine na TCRA kwa kuwa una uchochezi. Nilipoomba anipe vipengele vya mashairi yanayoleta uchochezi alidai kwa namna moja ama nyingine awezi kuipeleka hewani kwa kuwa anahofia kupigwa faini. Hiv kweli niingie studio kwenda kufumba mdomo kwa kusifia uozo... sasa mimi nawaheshimu sana mashabiki wangu nimerejea hapa ili mnishauri nini nifanye juu ya hili kwa maana hata hapa nilipo siwezi kusema niko wapi kwa kuwa kuna na hadi simu za mikwara zimeanza kuingia kuhusu nipe namba. Naomba ushauri wako tafadhali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…