Ndi yale anayo yasema Shibuda kuwa ukisema ukweli ndani ya CCM wewe hufai na Fitna itakuandama mpaka kufa na ndio walivyo mfanyia Lyatonga Mrema Iala bado yumo na Vunjo anaichukuwa kuilaini bila ubishi kwani wale wote wanajua alichowafanyia na anarudi tatizo la CCM yetu watu hawajipangi wao wanawaza pesaaaa tuuuna ndicho hata Mwl. JK Nyerere aliwahi sema mtu anaye lilia kwenda Ikulu anataka nini na anwapa vijisenti vyake vya nini huyu mtu si mtu, nawakumbusha hata Sita(spika) aliwahi kuimbia CCM jamani hawa matajiri wanaingia kwenye chama wanakiharibu sasa hivi,
Enzi za Mwl. Matajiri hawakuwa wana nafasi ndani ya chama ni Mwl. aliweza Jenga hoja ya kufanya hao matajiri wasiwe na nafasi ndani ya chama, leo hii viongozi wakubwa wa CCM wanawatetemekea matajiri kwanini wajua ni kuwa na upeo mdogo wa kukiongoza chama wanashindwa kujenga hoja ya kuimarisha miradi ya chama na kukiendeshe na kukalia kungojea misaaada toka kwa matajiri sasa CCM kweli kujigomboa huko itakuwa kazi kweli kweli