Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Libwata siku hizi dili mama,
Mtu anamlisha mwanaume kwa matakwa yake binafsi na akili za mwanaume zinahamia kwa huyo kimada.
Nina jamaa zangu kadhaa walilishwa hii kitu ikabidi tufanye kazi ya ziada kwenda kwenye kamati za ufundi sasa hivi wanafrahia maisha yao.
Manaume mengine bana, kama hayawezi kuendesha ndoa zao kwanini yanaoa.......nimekasirika kweli!...wengine tunahaha kupata wake, mijitu mingine inatesa wake zao....aaaaaaaaaaarrrrrrrrrrgggggggg
Libwata siku hizi dili mama,
Mtu anamlisha mwanaume kwa matakwa yake binafsi na akili za mwanaume zinahamia kwa huyo kimada.
Nina jamaa zangu kadhaa walilishwa hii kitu ikabidi tufanye kazi ya ziada kwenda kwenye kamati za ufundi sasa hivi wanafrahia maisha yao.
Mh dada nawe ushakutana na design hizi nn, umesema kwa uchunguWewe unaye haha kutafuta mke, na huyo mwanaume aliyemsema Boflo wote lenu moja.
Huwa mnaanza hivyo hivyo. 'ooh nahaha kumtafuta mke..' mkishapata sasa.
Yani wanaume!! Mungu atawalipa.
Mh dada nawe ushakutana na design hizi nn, umesema kwa uchungu
Yalishanikuta mpendwa na sina hamu.
asante mkuu, nimerudi salama....mambo niliyoyakuta huko sina hamu na wakenya..hawafai
My dear kwanza pole sana pia hongera kwa kuwa mwanamke mwenye uvumilivu kwa kizazi hiki ni wachache sana wanaoweza kuishi kwenye mateso na mkunguto kama wewe! ingekuwa mimi nilishaondoka! samahani dada kwani huna ndugu jamani? na je ni nini kikubwa hicho unachongangania kwa huyo bwana? ondoka unasubiri aje akuulie huko ndani! ondoka nenda kwenye ofisi haki za binadamu watakusaidia samahani kwa kukushauri uondoke nimeumia sana! hawa wahaume siku hizi wameingiliwa na ungojwa wa kusahau maagano yao timua usisubiri aje akumalizie huko ndani....ninazo kesi nyingi nimeziona na kuzisikia za aina hii wanawake wanateseka...jamani kama kuna mwanaume katika forum hii ana hii tabia aache!! mwisho wa dunia cha moto utakiona...pole dada lakini ushauri wangu miaka kumi unapigwa sasa itakuja miaka inayokuja kuuliwa ondoka nenda kwa ndugu wakusaidie huku unafuatilia haya mambo sehemu zinazohusika...Habari zenu?
Kila napoangalia wanawake wengine wanapendwa na waume zao roho huwa inaniuma sana ,sio kwasababu naona wivu ila kwasababu nawaza kwanini isiwe mimi.
Nimeolewa mwaka wa kumi na moja huu sasa tuna watoto watatu .mume wangu ana kimada nje ambae amezaa nae na ndio anaemthamini zaidi yangu na wanawe.kuna wakati hawalipii watoto ada ya shule hadi wanarudishwa nyumbani, mwaka jana mtoto wetu wa mwisho ndio alizaliwa pale katika hospitali ya tmj,mikocheni.nilijifungua kwa operesheni na nilikaa hospitali siki 3 bila mume wangu kufika hospitali na nikawa nashindwa kurudi nyumbani kwasababu sikuwa na pesa ya kulipia kila akipigiwa simu hapokei,mpaka siku ya tano ndio alinifata na kunipeleka nyumbani.
Ni visa vingi na mateso mengi nimeyapata kwa huyu baba.huwa anatuacha nyumbani hata wiki nne bila pesa ya chakula inabidi niende kuomba chakula kwa majirani,akirudi nikimuuliza ananipiga sana mpaka kuna siku alinivunja taya.sijui nifanye nini,sina pa kwenda,sina pa kuwapeleka wanangu.nifanye nini?je kuna sehemu yoyote nayoweza kwenda nikapata msaada
Dada, uyo mmeo ametekwa tu na shetani, siku akija kufumbuka macho, atasikitika sana juu ya anachokifanya, na atakuheshimu kwa uvumilivu uliompa....wakati mwingine wanakuwa wamelishwa dawa tu na hao nyumba ndogo hivyo hajielewi pengine, mwonee huruma tu..usishindane na mtu asiyeelewa utakuwa unamwonea. Nakushauri mwombe Mungu, atakusaidia, Mungu anaweza kuzibua hata kama alilishwa libwata, atarudi kwako na atakuheshimu. ila ukichukua uamzi mbaya, yeye atakaporudi kujitambua na kuona wewe ambaye ulikuwa unaelewa haukumsaidia kwa maombi na uvumilivu, huta pata heshima ile ambayo ungepata kama ungemwomba Mungu na kumsubiria....hii ni ngumu sana kuifanya ktk ulimwengu huu wa usawa ktk jinsia etc. wengi hapa watakushauri mengine...
nenda kanisani kwa watu waliookoka, shirikiana na wachungaji kumwomba Mungu, Mungu atambana kwenye kona yeye mwenyewe atajileta akitembelea magoti. tumeona watu waliokuwa wamebebwa na machangu wanalia kama watoto wadogo kuomba msamaha kwa wake zao baada ya maombi...wakati mwingine mchungaji wangu alishawai kumwombea mtu fulani, aisee, varangati lililotokea huko kwa nyumba ndogo, hamu yote ya nyumba ndogo iliisha siku hiyo hiyo na akarudi moja kwa moja kwa Mke wake. Mungu anao uwezo wa kuwagombanisha hao mahawara za mmeo naye, akarudi home akaona hamna faida kabisa kuitelekeza familia. SO PLEASE, SOLVE IT IN THAT WAY, usi sovu kwa namna ingine, kwani ukisolve kwa namna ingine inaweza kuongeza madhara badala ya kupunguza.
Libwata siku hizi dili mama,
Mtu anamlisha mwanaume kwa matakwa yake binafsi na akili za mwanaume zinahamia kwa huyo kimada.
daaaah mi nahuzunika sana kwa nini jamni inakua hivi wababa kwa nini hamna huruma....jana nusu jirani yetu afekule mtaani mume wake ameoa anapitisha miezi haji home mama wa watu anauza mkaa apate hela ya kula na wanae sita yule baba amewaacha akija hapo home ni matusi kwenda mbele mtu mbaba mzima miaka 60 halafu BOSI WA DOWUTA BANDARI....Inatia kinyaa..hela mpaka akatwe kwenye mshahara kutoka oFisini ndo ipelekwe home daaah wanaume mnatutisha sisi ambao bado hatujaolewa jamani itakueje...huyu jirani yetu jan apresha nusu afe.....dada pole sana mungu akusaidie NENDA TAMWA WAMKOMESHE HUYO MBABA ASO HAYA....yani na hasira kama ntukane...lakini naheshimu kijiwe....ila kina baba mmezidi jamani....MBONA ZAFANANA TU KWANINI HAMTULIII.....