Huyu msichana kaninunia ghafla bila sababu

Huyu msichana kaninunia ghafla bila sababu

Katika kitu ambacho kilikuwa kinaniumiza kichwa kipindi nimeanza mapenzi kipindi hicho nipo Form 3 mwaka 2012 ni kuhusu mapenzi. Zamani nakumbuka nilishawahi kupendana na msichana mmoja tulikuwa tupo mtaa mmoja, sasa kama mnavyojua hawa viumbe wakiona wanapendwa sana basi wataanza kuleta visa mara hivi ili kupima attention yako.

Kipindi kile walikuwa wakichezea sana kama gari bovu hadi nakuja kukomaa kwenye masuala ya mapenzi nilikuwa tayari nishaumizwa vya kutosha.

Nije kwenye mada, kuna huyu msichana wangu tulikuwa tupo kwenye mahusiano now ni miezi mitatu sasa toka tumekutana. Nakumbuka kipindi cha mwanzo alikuwa akinionyeshea mapenzi na kunipa maneno matamu kuwa nipo pekeeangu na kuniaminisha kuwa ananipenda haswa ila baada ya masiku kusogea ghafla akaanza kubadilika tabia, ikawa inapita hata siku mbili bila kuona sms yake.

Mambo sasa yamekuwa mambo kwani ameamua tu kuuchuna kimya na sasa imepita wiki mbili na mbaya zaidi amekuwa akiview status zangu za Whatsapp na kupita kimya.

Japo hakuna kosa nililomkosea, kinachonishangaza ni kwanini kaamua hivi?

Wakuu naombeni mnipe mitazamo yenu na natumaini nitapata mawazo bora kutoka kwenu🙏🙏🙏🙏🙏🙏
Kutokujibiwa nalo ni jibu
 
Maaan! Now this is what i call a troll.
You are really gifted in the art of vexing.
 
Back
Top Bottom