Huyu muuaji ni shujaa kama mashujaa wengine

Huyu muuaji ni shujaa kama mashujaa wengine

MakinikiA

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2017
Posts
5,104
Reaction score
6,827
MKAZI wa Majohe, Dar es Salaam, Ramadhani Juma, amekiri kumuua kaka yake Fikiri Juma bila kukusudia baada ya kutokea ugomvi baina yao, mshtakiwa huyo akidai chanzo cha ugomvi ni kaka yake huyo kutaka kumlawiti.

Inadaiwa wakati ugomvi huo unaendelea, mshatakiwa alichukua chepe na kumpiga nalo kaka yake kichwani kabla ya kumchoma kisu tumboni, hivyo kusababisha kifo chake.

Ramadhani alikiri kosa hilo la mauaji mwishoni mwa wiki mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Susan Kihawa wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kusomewa maelezo ya awali na Wakili wa Serikali, Esther Chale na kuyakubali yote.

Wakili Esther alidai Ramadhani na Fikiri ni ndugu waliokuwa wanaishi pamoja eneo la Majohe jijini Dar es Salaam na kabla ya tukio, mshtakiwa na kaka yake huyo walikuwa na ugomvi, Ramadhani akilalamika kwamba kaka yake Fikiri alitaka kumlawiti.

Alidai ndugu hao walishauriwa na mtu ambaye alitambulika kwa jina la Abdallah Seleman kuwa wanatakiwa kutengena, wasiishi pamoja tena na wote wakakubaliana na ushauri huo wa kutengana.

Hata hivyo, ilidaiwa mahakamani huko kwamba Januari 22, 2017, wakiwa nyumbani, ugomvi uliibuka tena, Fikiri (marehemu) alikuwa akimlalamikia mshtakiwa kwanini amemsaliti.

"Wakati ugomvi huo unaendelea, mshtakiwa alimchukua chepe na kumpiga nalo marehemu kichwani kabla ya kumchoma kisu tumboni na baada ya hapo kilichotokea aliyepigwa alifariki dunia.

"Mshitakiwa alifungua mlango na kuanza kukimbia lakini alikamatwa na polisi jamii na kurudishwa eneo la tukio na wakati wanaingia ndani, walikuta mwili wa marehemu, kisu na chepe vikiwa na damu," alidai Wakili Esther.

Baada ya mshtakiwa kukiri kufanya mauaji hayo, Hakimu Kihawa alimwambia mahakama inaona ana hatia katika kosa la kuua bila kukusudia, huku Wakili Esther akidai hawana kumbukumbu za makosa ya nyuma ya mshtakiwa.

Wakili huyo aliomba mahakama itoe adhabu stahiki ili iwe funzo kwa mshtakiwa na kwa watu wengine kwa sababu kitendo kilichofanyika ni cha kukatisha uhai wa mtu.

Baada ya wakili huyo kuwasilisha ombi hilo, Wakili wa Mshtakiwa, Precious Hassan aliomba mteja wake aachiwe kwa masharti kwa sababu akiwa gerezani alilazwa hospitalini kutokana na maradhi ya figo zake kushindwa kufanya kazi na taarifa hizo Jeshi la Magereza linazo.

Pia alidai kuwa kwa miaka mitano na miezi 11, mshtakiwa alipokuwa mahabusu, alipata tatizo la afya ya akili na alipelekewa Hospitali ya Taifa Muhimbili na baadaye alipelekewa Dodoma kwa matibabu zaidi.

Hakimu Kihawa baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili, alisema adhabu ya mshtakiwa ataitoa Novemba 29, mwaka huu, huku akiagiza kuwa siku hiyo Jeshi la Magereza liwasilishe mahakamani huko vielelezo vya mshtakiwa kuwa alikuwa mgonjwa.
 
Nadhan watakuwa ndugu na walikuwa wanaishi pamoja
 
MKAZI wa Majohe, Dar es Salaam, Ramadhani Juma, amekiri kumuua kaka yake Fikiri Juma bila kukusudia baada ya kutokea ugomvi baina yao, mshtakiwa huyo akidai chanzo cha ugomvi ni kaka yake huyo kutaka kumlawiti.

Inadaiwa wakati ugomvi huo unaendelea, mshatakiwa alichukua chepe na kumpiga nalo kaka yake kichwani kabla ya kumchoma kisu tumboni, hivyo kusababisha kifo chake.

Ramadhani alikiri kosa hilo la mauaji mwishoni mwa wiki mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Susan Kihawa wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kusomewa maelezo ya awali na Wakili wa Serikali, Esther Chale na kuyakubali yote.

Wakili Esther alidai Ramadhani na Fikiri ni ndugu waliokuwa wanaishi pamoja eneo la Majohe jijini Dar es Salaam na kabla ya tukio, mshtakiwa na kaka yake huyo walikuwa na ugomvi, Ramadhani akilalamika kwamba kaka yake Fikiri alitaka kumlawiti.

Alidai ndugu hao walishauriwa na mtu ambaye alitambulika kwa jina la Abdallah Seleman kuwa wanatakiwa kutengena, wasiishi pamoja tena na wote wakakubaliana na ushauri huo wa kutengana.

Hata hivyo, ilidaiwa mahakamani huko kwamba Januari 22, 2017, wakiwa nyumbani, ugomvi uliibuka tena, Fikiri (marehemu) alikuwa akimlalamikia mshtakiwa kwanini amemsaliti.

"Wakati ugomvi huo unaendelea, mshtakiwa alimchukua chepe na kumpiga nalo marehemu kichwani kabla ya kumchoma kisu tumboni na baada ya hapo kilichotokea aliyepigwa alifariki dunia.

"Mshitakiwa alifungua mlango na kuanza kukimbia lakini alikamatwa na polisi jamii na kurudishwa eneo la tukio na wakati wanaingia ndani, walikuta mwili wa marehemu, kisu na chepe vikiwa na damu," alidai Wakili Esther.

Baada ya mshtakiwa kukiri kufanya mauaji hayo, Hakimu Kihawa alimwambia mahakama inaona ana hatia katika kosa la kuua bila kukusudia, huku Wakili Esther akidai hawana kumbukumbu za makosa ya nyuma ya mshtakiwa.

Wakili huyo aliomba mahakama itoe adhabu stahiki ili iwe funzo kwa mshtakiwa na kwa watu wengine kwa sababu kitendo kilichofanyika ni cha kukatisha uhai wa mtu.

Baada ya wakili huyo kuwasilisha ombi hilo, Wakili wa Mshtakiwa, Precious Hassan aliomba mteja wake aachiwe kwa masharti kwa sababu akiwa gerezani alilazwa hospitalini kutokana na maradhi ya figo zake kushindwa kufanya kazi na taarifa hizo Jeshi la Magereza linazo.

Pia alidai kuwa kwa miaka mitano na miezi 11, mshtakiwa alipokuwa mahabusu, alipata tatizo la afya ya akili na alipelekewa Hospitali ya Taifa Muhimbili na baadaye alipelekewa Dodoma kwa matibabu zaidi.

Hakimu Kihawa baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili, alisema adhabu ya mshtakiwa ataitoa Novemba 29, mwaka huu, huku akiagiza kuwa siku hiyo Jeshi la Magereza liwasilishe mahakamani huko vielelezo vya mshtakiwa kuwa alikuwa mgonjwa.
Inaonekana mshitakiwa alivumilia manyanyaso kutoka kwa ndugu yake kwa siku nyingi. Na huenda marehemu (kaka wa mshitakiwa) alikuwa anakaa na mdogo wake (mshitakiwa) kama mlezi, kama ilivyo kwa familia nyingi katika utamaduni wetu.

Kumekuwa na tabia za wakubwa (kaka au dada) kutumia vibaya ukuu wao (kama wakubwa katika familia) kuwanyanyasa wadogo wao kwa sababu mbambali. Wapo wanaofanya hivyo ili kuhalalisha ukubwa (huu ni ushamba), lakini wapo wanaofanya hivyo ili kukidhi mahitaji yao.

Niliwahi kusema humu, kuwa, wazazi wawe makini na wazaliwa wao wa kwanza, kuwaamini katika suala la kuangalia wadogo zao, maana katika utamaduni wetu, tumekuwa na kasumba hii (labda kutokana na ugumu wa maisha), kuwaamini watoto wakubwa katika familia na kuwapa jukumu la kuwalea wadogo zao (hasa umri wa wazazi ukiwa umeenda).

Kumekuwa na manyanyaso (kwa baadhi ya ndugu) kwa wadogo zao, na wakati mwingine hata kuwadhurumu haki zao! Hapa wakati mwingine wazazi hawawezi kubaini kama kuna tatizo linaloendelea baina ya hawa ndugu. Na hata ikitokea mdogo akapaza sauti, bado wazazi (baadhi) hawaamini, kwani humuona dogo ni mwongo, na matokeo yake jambo linazidi kuwa kubwa!

Turudi kwenye jambo la mahakama; kwa saikolojia ya kawaida, inaonyesha wazi kuwa, mtuhuhmiwa (mdogo) alimvumilia kaka yake kwa muda mrefu, lakini ikafika mahala uvumilivu ukamshinda. Siku ya tukio, (sisi hatujuwi ilikuwaje); lakini hebu fikiria kama marehemu alitumia nguvu kutaka kumwingilia (kumbaka) mdogo wake, je, dogo angefanyeje katika mazingira hayo?!

Tunatambua mahakama ni chombo chenye weledi katika kutoa maamuzi, busara itumike katika kumuhumuku dogo huyu (kwa umri wa mahakama anaweza kuwa mkubwa). Ni jambo jema kuwa mahakama imetambua kuwa ameua bila kukusudia, lakini zaidi ya hapo, waangalie kuwa ni kweli anastahili adhabu yoyote?!
 
Ushujaa upi aliokuwa nao!!!??? Mtu analalamikiwa kumsaliti mwenzie (marehemu) hiyo inamaanisha alikuwa anabanduliwa muda mrefu ila baadae akabadilika (labda alipata bwana mpya)
Mh!
yupo sahihi kwa sababu moja tuu.
kufanya mapenzi ya jinsia moja hasa kipindi hiki chenye mibomondo mingi

Hivi inakuaje madem hawapo? Bar maids hawapo?hata virabuni kweli mpaka unainamisha mwanaume mwenzio kweli?
 
Back
Top Bottom