Huyu mwanaume ana makosa?

Huyu dada the next thing ilikuwa ni kumpa mume wake ugonja wa moyo maana kama ni kuvumulia mume amevumilia vya kutosha ni mtu gani unafanya kitu karibia mara tatu na haujifunzi wala kuona kama unakosea

Nakwambia wanawake wengine wana raha kweli kupata waume wapole kiasi hicho kha!!!
 
Huyu mwanamke ana matatizo ,bora hata hizo pesa angefanyia vitu vya maana ambavyo hata mme angeona ,
lakini alikuwa anahonga?mme hana kosa kachoshwa na vituko vya mkewe
 

Kwa suala la kutunza familia kiukweli siishi humo ndani lakini huyo baba anajitahidi sana maana huwa namuona sana anatoka na familia yake akirudi kapita supermarket shule watoto wakifungua haendi kazini anawapeleka mwenyewe kwa gari yake. Huyo Mama kamuudhi kila mtu bana ukiangalia utaona tu kama Baba anatunza familia sasa nini kimemsababishia huyu mama kukopa na pesa inakopelekwa haijulikani??

Nimeogopa kukopa Benki kama ndo mtindo wenyewe huo wa kubebewa vitu kama unahama aka sikopi mie kabisa kha....
 
Huyu mwanamke ana matatizo ,bora hata hizo pesa angefanyia vitu vya maana ambavyo hata mme angeona ,
lakini alikuwa anahonga?
mme hana kosa kachoshwa na vituko vya mkewe

Hapo ndo tatizo lilipo
 
Huyu mwanamke ana matatizo ,bora hata hizo pesa angefanyia vitu vya maana ambavyo hata mme angeona ,
lakini alikuwa anahonga?mme hana kosa kachoshwa na vituko vya mkewe


1ST Lady mimi naona labda ndo moja ya wale watu kua ana nia nzuri na hizo pesa lakini hajajaliwa kua na business acumen. Labda angejua uendeshaji, jinsi na wapi a iinvest, jinsi ya kutoa faida ili aweze kugawa za kulipa deni na matumizi, yote yasingemkuta. Aliposhindwa the first time naona akaamini kajifunza kutokana na makosa, na ataboresha biashara alafu akachemka, mara ya pili, ya tatu.... Kwa upande wangu Makosa yake makubwa ni kutomshirikisha the husband.
 
Kuna wanawake wengine wa ajabu kwa kweli.....................lakini ndio wenye bahati ya kuwapata waume wema

na wanashangaza pia, sasa kaam ameamua kuchukua kimya kimya(siri yake) y acfanye juu chini kupata pesa ya kurudisha? kuna watu wapumbavu balaa, c angewalisha hata ugali mchicha hapo ndani ili a save pesa za kurudisha kaama aliamua iwe cri yake?kuna vitu vinachosha sana.
 

Good Girl......
 

nyamayao dunia hii inavisa we acha tu................
 
yaani vululu vululu, unaona kwako kunaungua kumbe kwa wengine kumeteketea kabisa.....
Ah Sasa huyu mwenzetu kwanza kampata mwelewa yeye hata hana haja ya kuona wala kusikia senti tano yako nyekundu, bado umekopa mara ya kwanza usimweleze wala hakukuuliza kisha matunda ya mkopo huo hana haja ya kuyaona wala jua ikisha umeshindwalipa nadala ya kumweleza akusaidie unamwacha aaibike kwa kutaifishwa mali na samani za nyumbani kwake.... akakusamehe
Mara ya kwanza, ukarudia ya pili na sasa ya tatu kakusamehe zote hizo ah........................ hebu ngoja kwanza ninywe maji
 

DA
Huyu mmama alikuwa anakopa hizo hela anafanyia nini? hukufanikiwa kujua hilo? hakueleza?
Naamini huyu bwana angalau alimuuliza mkewe mara ya kwanza na kuambiwa kuhusu alichokuwa anafanya , kiasi cha kushindwa kurudisha mkopo. Je alifanya nini kumsaidia?
Manake tusimlaumu kumbe likuwa anataka kuendeleza familia yake lakini hakupata msaada wa mumewe.
Ila ni ngumu sana kuamini kama alifanya yote haya 3 times bila mumewe kujua chochote.

Mbaya zaidi uambiwe alikuwa anafanyia mambo ya kipuuzi, kama kuhonga vi serengeti Boys!!
 
Dah....wanaume wengine wana kazi kweli!!
Sasa huyo mama mkopo wa kwanza hakufanikisha kitu....akafikiria mara ya pili labda ntaweza hilo naelewa ila baada ya kufeli alirudia mara ya tatu akiwa anafikiria nini???MIUJIZA??
Swala la kutokumshirikisha mume kama angefanikiwa isingekua kitu kibaya...baada ya kuona mambo yameenda vizuri angeifanya kua sapraiz kwa mumewe na wote wangefurahi.Ila kitendo cha kumtaaarifu mume Kwa kunyang'anywa mali mara tatu sio vizuri kabisa!!Inabidi akalishwe chini aelezwe kwamba anachofanya ni ujinga na ubinafsi.Watu wa aina yake hua hawafikirii watu wengine wataathirika vipi na maamuzi yao na asipojirekebisha sasa hivi siku ya siku watajikuta hata pa kuishi hawana tena!!!

Huyo baba namuonea huruma kweli....ni mmoja kati ya wanaume !Ingekua mwingine angeshamlamba makofi yakifuatiwa na barua ya kumrudisha kwao akajifunze!
 

The Guy yupo sahihi, arudishwe wapi? :A S cry:
 

yaani mie nafikiria wakati mwingine wanawake tunawaza kwa kutumia kitu gani, yaani kaona jahazi linazama akaona bora tu lizame kuliko kutafuta njia mbadala....na kweli wamepata wanaume wa kuwachezea.
 
Huyo mama ana makosa , pia hiyo nyumba yao ina matatizo.Dah akampumzishe kidogo akirudi atapata akili.Dunia ina mambo.
 

cku hizi wanaopataga muda wa kuandika barua bac, unatupiwa vinguo viwili vitatu vya kukusitiri kwa cku kadhaa huko kwenu kabda haujajipanga kuja kufungasha kilicho chako....(viasarawili an viagauni ulivyobakiaza)
 

Tulimuuliza akawa hana jibu akaniudhi nikamuachilia mbwali
 

Kwa kweli ilinisikitisha kweli na ukiwaona wanavyopendana huwezi kuamini haya la we acha tu dunia ina mambo
 
cku hizi wanaopataga muda wa kuandika barua bac, unatupiwa vinguo viwili vitatu vya kukusitiri kwa cku kadhaa huko kwenu kabda haujajipanga kuja kufungasha kilicho chako....(viasarawili an viagauni ulivyobakiaza)

Umenichekesha umenikumbusha kuna mdada jama katupiwa nguo zake hapa hadharani, ukipita jirani na hapo unarushiwa begi au kiatu hakuna aliekua anasogea yaani huyo baba utadhani alivuta kidogo, kosa lenyewe kisa kakuta matairi ya gari mlangoni mama kuulizwa anababaika. Sasa sijui ndio ingekua anakaa na huyu mmama mkopaji halafu akaja kuta watu wa bank wanabeba vikochi na visufuria vyake ingekuwaje, nahisi angemchinjilia mbali walahi kuna watu wana wanaume bwana.
 

Ha ha ha umenichekesha hiyo red mie basi tu ha ha ha kavuta nini lakini maty mchokozi wewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…