Huyu ndie Rais wa muda wa Burundi

WilsonKaisary

JF-Expert Member
Joined
Apr 4, 2017
Posts
392
Reaction score
949

Pichani spika wa jamhuri ya Burundi kwa jina anaitwa Paschal Nyabenda. Kwa mujibu wa katiba ya jamhuri ya Burundi huyu ndie atakuwa raisi wa muda mpaka mwisho wa mwezi wa name mpaka atapoapishwa raisi aliyeshinda uchaguzi wa mwaka bwana generali Evariste Ndayishimiye.

Nyabenda atashika nyadhifa hi kwa muda tokana na matakwa ya katiba ya jamhuri ya Burundi. Katiba inafanunua endapo raisi atafariki au kushindwa kuongoza tokana na maradhi basi spika wa jamhuri ya Burundi ndie atakuwa raisi wa muda mpaka raisi mwingine atapopatikana kupitia uchaguzi mkuu.

Kwa bahati nzuri uchaguzi ulikuwa umeshafanyika na kumpata mshindi bwana generali Evariste Ndayishimiye ambae atapishwa mwishoni mwa mwezi wa nane. Bunge la jamhuri ya Burundi litakuwa chini ya naibu spika bwana Agathon Rwasa pichani.


Agathon Rwasa alichaguliwa mwaka 2015 kushika hatamu ya unaibu spika, ikumbukwe mwaka 2015 ndipo Pierre Nkurunzinza alikuwa anaingia awamu ya tatu kwenye kiti Cha uraisi kupitia mabadiliko mbali mbali ya katiba.

Paschal Nyabenda kazaliwa 12/4/1966, mnamo mwezi 6/2020 alifanywa kuwa acting president of Burundi.
Amewahi kuwa gavana wa Jimbo la Bubanza kupitia chama tawala Cha CNDD–FDD na pia amewahi kushika hatamu mbali mbali Kama unaibu spika wa jamhuri ya Burundi.
 
Wa hapa akipata ngekewa kama hii, ata-suspend katiba na kuwa rais wa maisha!
 
All the best wana Burundi

Ova
 
President: Pierre Nkurunziza Trending
Capital: Gitega
Area: 27,834 km²
Population: 11.18 million (2018) World Bank
Currency: Burundian franc
Official languages: Kirundi, French, English

RegionHASCISOFIPSPopulationArea(km.²)Area(mi.²)Capital

KageraTZ.KG05TZ192,458,02328,38810,961Bukoba

Nchi eneo kama mashamba makubwa ya USA!
 
Kama wamechagua Rais kwanini asishike sasa madaraka wanasubiri nini mpaka mwezi wa 8.
 
Hilo jina la Agathon Rwasa mbona linataka lifanane na yule aliye kuwa anataka ampindue Nkurunzinza.
 
Kama wamechagua raisi kwann asishike sasa madaraka wnasubiri nn mpaka mwesi wa 8.
Ni matumizi mabaya ya kodi, ingekuwa uchaguzi haujafanhika ingekuwa sawa ila Rais anasubiri kuapishwa tu mwezi wa 8 wangemwapisha ili kuokoa fedha ya umma

Nalog off
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…