Huyu ndio Camilius Wambura, Inspekta wa Polisi - Mpenda haki

Nimejawa na furaha kuona mtu makini ndani ya Jeshi la Polisi mwenye uzoefu na weledi anakabidhiwa majukumu makubwa ya kuliongoza Jeshi letu la Polisi. Hakika CAMILIUS WAMBURA ni mtu sahihi mno.
Hivi yule kamanda aliemwambia Msukuma hawezi kuomba radhi, Kama ni cheo chao wachukue, Yuko wapi?na jina lake nani
 
Kuongoza jeshi la Polisi sio jambo rahisi hasa kwenye nchi za kiafrika.

Tuna siasa za hovyo sana kuwa IGP ni mtihani mkubwa sana msidhani ni rahisi
 
Kila mtanzania mwenye uelewa wa mambo anayofuraha kubwa kutokana na uteuzi uliofanywa na Rais Samia katika kumteua CAMILIUS WAMBURA kuwa Inspekta Jenerali wa Polisi. Ni mtu sahihi kwa wakati sahihi.

UZOEFU KATIKA MAJUKUMU MAKUBWA

-Kamanda wa Polisi Mkoa Maalum wa Kipolisi - KINONDONI

- Mkurugenzi wa Operesheni- Makao makuu DODOMA

- Kamanda wa Polisi -Kanda Maalum-DAR ES SALAAM

- Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI).

UMARIDADI NA HISTORIA

- Utumishi uliotukuka katika medani

-Uzalendo na uchapakazi katika majukumu mbalimbali ndani ya Jeshi la Polisi

-Ushiriki katika masula mbalimbali ya kijamii

-Mwanazuoni aliyefanya vizuri katika masomo na tafiti za kitaaluma

-Mwakilishi wa Tanzania katika mijadala ya Usalama ya Kimataifa

-Kachero mwenye uweledi katika kutekeleza Operesheni zenye maslahi kwa nchi yake.

-Kamanda wa Polisi aliyejipambanua katika kutetea haki na kulinda katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Sent from my SM-A325F using JamiiForums mobile app
 
Nimejawa na furaha kuona mtu makini ndani ya Jeshi la Polisi mwenye uzoefu na weledi anakabidhiwa majukumu makubwa ya kuliongoza Jeshi letu la Polisi. Hakika CAMILIUS WAMBURA ni mtu sahihi mno.
Mshaanza kujikanyaga wenyewe. Tupe na historia ya elimu yake
 
Uteuzi huu unefanyika lini
 
Na wengine walipepewa hivihivi mwisho wa siku tulijionea wenyewe uhalisia ulivyo

Za kuambiwa changanya na zako
 
Alisoma sheria au kitu gani?
Ni lingusitic mmoja wa ajabu tu; mmojawapo wa watu waliokuwa wanategemewa sana kwenye engklsh debates. Lingusitics wengi wanapokuwa wako jeshini huwa wanapenda kusoma sheria
 
Tupe kiwango cha juu cha taaluma yake mkuu.
Sababu hata mimi nilieishia 'la-saba A' ni msomi na mbobevu kwenye emneo langu la udalali 🤣
 
Vipi utendaji na kushiriki kwenye medani za kimataifa kwa overall huko nje?.
 
Jambo la msingi kwa sasa ni kukomesha uhalifu, kuwabaini na kuwatokomeza.
hatutaki kusikia majambazi wala wavutaji wa bangi na madawa ya kulevya.

Kama alivyo sema Amiri Jeshi Mkuu, kuwa anataka kuona jeshi linajibadilisha na kuwa lenye weledi wa na nidhamu ya hali ya juu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…