Huyu ni samaki wa aina gani?

Namjua kwa kisukuma tu anaitwa starfish ukienda ferry wapo wanauzwa
 
Kwanini haliwi, ana nini? Naomba kujua
Huyu mdudu wapo species karibu 2000 duniani kote. Hawa wa huku kwetu gamba au ngozi yake ina sumu kali ikiliwa au ikigusa zile sehemu za ndani ambazo hazina sumu.

Kinachowashinda wengi ni maandalizi yske maana inaihitajika uangalifu sana na muda mrefu. Ni kama unakuwa huna uhakika iyo sumu umeitoa yote na gozi ya nje au nyingine imebaki. So watu wengi wameamua kuachana nae, ila wachina na baadhi ya mataifa ya asia kama kawa wangagonga tuu.
 
Dah wachina
Bora wamle na ngozi. Wapo wengi wale
 
ni kutokuwa na umakini tu ndio maana wanaojua vitu vizuri hawamuachii
 
Huyo kiumbe anaitwa Sea star au "starfish" kama walivyosema wadau hapo juu. Lakini huyo kiumbe kwa viwango vyoyote vile yeye sio samaki.



Ila kwa sababu ya mazoea, tumezoea kuita viumbe mbalimbali wa majini "samaki". Mifano mingine ni Pweza (octopus), ngisi (squid), kamba miti na kamba koche (prawns and lobsters), nguva (dugong), kasa (sea turtle), chaza (oyster), konokono wagumu na laini (gastropods), kaa (crabs), jongoo bahari (sea cucumber) na wengine wengi.



Kwa ufupi kuhusu huyo sea star.

Kama unakumbuka kuhusu makundi mbalimbali ya wanyama, kama vile ndege, mamalia, amphibia, reptilia n.k.... basi huyo yeye yuko kwenye kundi lake linaitwa "ekainodemata" echinodermata.



Je, ni kina nani hao ?

Echnoderms ni viumbe wasio na uti wa mgongo, wanaopatikana baharini, wenye ngozi yenye miba. Tunaweza "kuwatania" kwa kuwaita "nungunungu bahari".



Ndugu zake sea star katika kundi lao la echnoderms ni sand dollar (kabla ya ugunduzi wa fedha hizi za sasa, hawa viumbe walikua wanatumika kwa ajili ya manunuzi na mauziano), jongoo bahari (holothurians) pamoja na sea urchins (hawa wana miba mirefu kabisa, kama ya nungunungu).



NB: Nimeelezea aspect kibailojia zaidi. Mengine (kama analiwa, ana sumu, maandalizi yake yakoje, n.k wameshaeleza vyema wenzangu hapo juu).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…