Huyu Salah anastahili Ballon d'or.

Vigezo wanavyozingatia pia ni kuisaidia timu yako kupata mafanikio, labda tumuombee wapate ndoo
hili haliangaliwi. wanaangalia performance na tabia nje na ndani ya uwanja.
 
Kama ni hivyo Messi 2015/16 aliongoza kilakitu na kupata copa del ray tu angepata ile Ballon lakn Ronaldo kachukua na Alishine 9 UCL matches za mwisho...Akibeba ndoo hakina wakumpingaa hata UCL stuffs wanajuaa
 
Hahah!! Mkuu unakosea kusema hivyo huwa wanaangalia timu yako umeisaidia vipi kupata mafanikio na mafanikio yenyewe ndio makombe, ingekua kama hivyo unavyosema wewe Mess angekua anachukua kila mwaka
Vigezo official ndiyo hivyo mkuu.Kusaidia timu hakipo. Sema kwasababu ni upigaji wa kura ndiyo maana haya mambo hutokea.
 
Tatizo Ballon D'Or inatolewa kwa bias sana...ila kwa msimu wa 2017/2018 nakuunga mkono Salaha ameonesha udambwi dambwi wa kufa mtu.

Hapa namuangalia anavyowapelekesha Roma mpaka najiuliza usikute ni Messi kavaa jezi ya Liver.

Baada ya kusema hayo, nikiweka ushabiki wangu wa Chelsea, potelea pote wakafungwe fainali tu..hakuna kuchukua kombe Liver!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…