St Lunatics
JF-Expert Member
- Aug 29, 2015
- 6,644
- 11,174
Leo nimepita mitaa ya Posta nikasimamishwa na traffic mmoja walikuwa wapo kama 4. Huyu mmoja akaniuliza naelekea wapi? Nikamwabia naelekea Jangwani kuna mtu namfata akaniomba nimpakie na nimshushe mitaa ya Fire. Sasa mimi gari yangu sipendi kushusha vioo lakini huyu bwana mkubwa kuingia tu kashusha vioo na kuweka mkono wake kwenye mlango. Nikamuuliza vipi mzee hupendi a/c au? Alijibu aahhh kumbe umewasha a/c samahani ndugu. Hafla sura yangu ilijaa ile mistari kwenye uso kama mzee wa miaka 60, na kutafakari hii harufu inatokea wapi. Ilinibidi nimuulize vipi mkuu umepitiwa na haja(umepufff) au? Huku nae alianza kufunga pua akizania mimi ndio nimeachia mzinga wa nuklia. Kuangalia pembeni yetu kumbe lilikuwepo gari la maji taka(gari la kusafisha vyoo). Tukabaki kucheka tu huku mimi nikimwambia nilizania yeye na yeye akisema alizania mie.😀😀😀😀