I am happily divorced, women are devil.!

Mtambuzi

Platinum Member
Joined
Oct 29, 2008
Posts
8,809
Reaction score
15,421
Tulikuwa tumetoka outing kwa ajili ya kupata winywaji na kubadilishana uzoefu, na katika mazungmzo yetu tulifikia mahali tukajikuta tukizungumzia masuala ya familia na hapo ndipo aliponijulisha kwamba aliachana na mkewe miaka miwili iliyopita nchini Uingereza baada ya kuishi pamoja kwa miaka mitano na kujaaliwa kupata mtoto mmoja wa kiume.

Huyu hakuwa mwingine bali alikuwa ni mfanyakazi mwenzangu ambaye ndio amejiunga na Kampuni yetu akitokea nchini Uingereza.

Alidai kwamba mkewe alikuwa ni kero kero kero, na mtu ambaye yuko juu kwa kila kitu, kwa kipindi cha hiyo miaka mitano, alichoishi naye alikjikuta akiwa kama yuko Jehanamu. Kwani hakuwahi kuifurahia ndoa yake kamwe tangu walipojaaliwa kupata huyo mtoto wao pekee.

Aliniambia kwamba alijitahidi kuilinda ndoa yake na mkewe lakini ilifika mahali akajikuta kama anafanya kazi bure, huyo mkewe hakuonekana kujali wala kuonesha ushirikiano na ndipo alipofika mahali akaamua bora yeshe…………………..Wakayamaliza kisheria na sasa anayo furaha kuachana na mkewe na wala hajuitii kitendo hicho.

Sikutaka kuchangia chochote wala kutoa maoni yangu, bali nilimpa pole na nikabadilisha topic maana niliona anataka kuchakachua outing yetu.

Hivi inakuwaje, haya mambo jamani……………………….Watu leo wanaoana wakiwa na furaha na amani, lakini mara tu, watu wanaachana baada ya sarakasi nyingi na kufikia kutamka maneno kama haya……!
 
You are a devel that's why you married a devel. Acha kutuita wanawake wote madevel ni wewe na mkeo. Nenda kwa TB Joshua ukatolewe spiritual wife
 
You are a devel that's why you married a devel. Acha kutuita wanawake wote madevel ni wewe na mkeo. Nenda kwa TB Joshua ukatolewe spiritual wife

Hujasoma vizuri, umekurupuka, Mimi nimenukuu kutoka kwa huyo mhanga aliyeacha na mkewe..............!
 
ahahahaaaaa...there is nothing like shared experience in marriage life...TAKE OR HATE IT BUT THATS A ONLY REMAINING FACT.
 
Ndoa ni nyingi zenye matatizo.... Mara nyingi inapotokea ndoa imevunjika kila mmoja wa ma ex's hao hushuhudia kua wao walikua wema na kwamba ex wake ndie alie kua na madhaifu zaidi. Kuweza pata Ukweli ni pale tu wote wawili wanapokuwepo.

Hata hivo kwa kuzingatia topic yako; napenda nigusie kua hapo ndipo watalaka hukosea... Unapomkashifu huyo ex wako mara kwa mara ina maana hata kwa watoto wafanya hivo hivo (kuonesha mama/baba yao alikua in the wrong; which is not rite sababu watoto wanatakiwa waheshimu mzazi wao no matter ana madhaifu yepi!). Ingekua kila mtalaka anakaa vizuri na kutafakari nafasi yake katika kuvunjika kwa ndoa... Ingesaidia sana sisi kujifunza tokana na Makosa, Ingesaidia kua wastaarabu na saingine hata kutambua kua kwa kweli spouse wako alikua akijitahidi juu yako ila wewe mwenyewe ulikua na madhaifu mno, na pia kutujenga kama wanadamu; through learning from mistakes.

Hata hivo kuna ex's wanaumiza jamani..... Wanaumiza mno na watamani Umtukane kabisaaaa! Hasa kama bado ana uwezo wa kukuumiza na hali msha talakiana. It hurts....
 
Ha2fahamu walikutana wapi na walianza vipi 2mebahatika kujua matokeo tu "Divorce!"..May be mwanaume alikurupuka!hakua amemfahamu vizuri labda kwa sbb zake binafsi may be kuna alichokikimbilia kwnye hiyo ndoa..yalishatokea anachotakiwa kufanya ni kuangalia alipojikwaa lawama hazitomsaidia kitu..
 
Umenena sawa sawa, niliwahi kuandika uzi unaozungumzia jambo hilo, ngoja niutafute kisha niuweke hapa, kama rejea....
Sikutaka kujadili jambo hilo na huyo mfanyakazi mwenzangu, kwani niliamini kwamba huenda mjadala huo ukachukua sehemu kubwa ya mazungmzo yetu, wakati lengo letu lilikuwa ni kufahamiana na kubadilishana uzoefu maana tutakuw atukifanya kazi katika kitengo kimoja.

Hii hapa nimeshaipata:

https://www.jamiiforums.com/mahusia...ia-zenye-mduara-wa-talaka%85%85%85%85%85.html
 
Yaani mtu akitendwa tu, basi hiyo jinsia yote ishakuwa devil!
Bora umesema, hata mimi mwenyewe nilishangaa, kwa jinsi ninavyompenda mama Ngina hata sitegemei siku moja kumuita Devil!
 
Dingi, tuweke lile deni letu pending kwanza, I miss blackmailing u.

Hiyo naitafakari sana nikiangalia wedding shows. Kuna kipindi chaitwa 'poor bride rich bride', huwa nikiangalia mchakato mzima na jinsi wenzetu wanavyowasiliana kuhusu taratibu zote, natamani kupata feedback baada ya mwaka kuona kama ndoa bado ipo ama ilishavunjika. There are so many things we should notice from first date, basi tu self denial inatusumbua! Kila mtu ana mchango wake in each mess!
 
Hawa watakuwa walitamaniana kabla ya ndoa na baada ya tamanio kuwakinaisha wakajiona kila mmoja na mtazamo wa kishetani kwa mwenzie, tungesikia na upande wa mke wa huyp jamaa pengine yangekuwa ni zadi ya mwanaume. Mkiamua kutalikiana haifai kuchafuana kwa watu hata kama mlitendana uovu hapo ni inaonyesha jinsi gani busara ya huyo bwana ni ndogo.
 
baadhi ya wanawake hata uwape nini bado ni problems tu ninakubali kwamba they are troublesome not devils by the way.
 
Unapokutana na mwanamke na kumpenda na kuamua kuishi nae ......na wote makakubaliana ... UKUMBUKE UMEOA MWANADAMU [HUMAN BEING] HUJAOA MALAIKA [ANGEL] .......hivyo DONT HAVE TOO HIGH POSITIVE EXPECTAIONS .......ELEWA NA NEGATIVE ZITAKUWEPO - na hii ni kwa WOTE [MUME/MKE].

Ndoa ni kuvumiliana, kusameheana, kurekebishana, kupendana na kupeana ...... Kama small negative unaifanya BIG ISSUE - matokeo yake ni DIVORCE .. na inapotokea ......TAFAKARI - WAPI WEWE ULIKOSEA KABLA YA KUMNYOSHEA MWENZIO KIDOLE
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…