I don't know if I can make it through this year

Wakuu asanteni kwa kuchangia huu uzi, hakika mmenisaidia sana. Sasahivi akili yangu imetulia na nnaweza kufanya maamuzi sahihi, mbarikiwe sana

Sent using Jamii Forums mobile app

Jipe moyo mkuu, simama kwa imani. tuliza akili yako utashinda.

Kama ulikuwa tajiri sana na mali zikapotea zote... msome mtu anaitwa Ayubu. Kama umejikuta huna mali na bado maisha magumu msome Mwanamke wa Serepta na masikini wengine waliosimama na Mungu akawainua. sio wa kwanza wewe kuingia katika hali hiyo. Jua tatizo lako chagua njia ya kujipanga. Relaxxxx life is gudoooooo, be hapi...
 
Asante kwa kunitia moyo mkuu, kiukweli nilikua nimevurugika..hata ule mda naandika hii thread nilikua nimekata tamaa kabisa.

Pesa ya biashara nataka sana na nitahangaika kuipata, kula nakula chakula kipo, hapana siyo ada..niliamua ku postpone masomo tangu mwaka jana kwa kukosa ada lakin naamini nitaendelea baadae, hilo sio muhimu sana kwa sasa. Suala la kodi hilo ndo kikwazo kikubwa, lkn kilichofanya nipandishe huu uzi sio kuikosa hiyo kodi mana najua wapo wengi kama mimi ila ni vile niliona kila nnachokifanya kuipata hiyo kodi kinakwama hadi nikafikia hatua ya kujiona sifai, nina mikosi kuliko yeyote, sina maana au niliumbwa kwa bahati mbaya n.k

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli kabisa mkuu, ipo sehemu nilijikwaa na nmeifahamu. Asante

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukipata nafasi unaweza ukaelezea hapa mwanzo mpaka mwisho nini tatizo?

Hujawa straight, probably kuna watu wanaweza kusaidia kama utakuwa on point, binafsi nimeona kama hujawa direct.
 
Starboywiz,

Kwanza Muombe Mungu wako Samahani ili kusafisa kabisa ubongo wako uliojaa mawazo potofu. Hivi unaujua mkosi??? acha kabisa.... unakula unashiba!!!! mtukuze Mungu.

Kama nilivyosema haya mengine jipange tu. Pesa inatafutwa kwa njia nyingi. Tena kama uko dar... mtoto wa kiume huwezi kosa angalau 5,000 kwa siku ukiamua kujituma. Angalia nyumba unayoishi.... maaana isije ikawa umechukuwa nyumba nzima Sinza, halafu unalia kodi. Ishi maeneo ya kodi ndogo ili ujikusanyie mabaki kwa malengo. Hiviii ulishawaza kwa nini kuna watu wanapanga nyumba pale jangwani mabondeni???? sijasema ukapange jangwani.
Ninachokiona kwako ni mipango, hakuna cha mkosi, wala mchawi wala eti dunia sio yako..... dunia yetu as long as tuko ndani yake tukiwa hai.... let us enjoy life no matter what...
 
Da'Vinci,
Kuna siku nilianzisha Uzi wadau wakani ignore ila ukweli ni kwamba vijana tunapitia magumu sana and no one who's care
 
Kuna siku nilianzisha Uzi wadau wakani ignore ila ukweli ni kwamba vijana tunapitia magumu sana and no one who's care

Umeshajiita Gundu... what do you expect?? watu wakuelewe.... yaani umejikubali na magundu yako, lazima uendelee nayo
 
Ni rahisi sana mtu ku comment vile anaona,kuna maisha mtu unapitia dah!!unafanya biashara watu wanakupita kama hawakuoni,kila mlango wa ridhki unafungwa, hata kibarua cha kuchimba choo hupati,saidia fundi sijui hupewi!Binafsi niliwahi kupitia hayo maisha kipindi fulani, zile mia mia zikiwa 2 tu hupati!! Kuna maisha kama hujapitia ni ngumu sana kumuelewa mtu anaesema hajala kwa sababu hana pesa!kikubwa kama hujapitia magumu kwenye hii Dunia mshukuru Mungu tu ba si kuona watu wenye changamoto ni wazembe!!
Hayajakukuta


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hay
Umeshajiita Gundu... what do you expect?? watu wakuelewe.... yaani umejikubali na magundu yako, lazima uendelee nayo
Acha ufala kwani ningejiita pandri ningekua pandri kweli, we na wenzio wote ambao hua mnaliandama hill jina hamna akili kabisa, hakuna uhusiano wowote kati ya jina na mafanikio ya mty
 
Pole mkuu hayo mambo yapo kwenye safari ya maisha ni phase tu unapitia na Kuna kitu utajifunza...Kuna siku utakua vizuri then unakumbuka kipindi hiki ni moja Kati ya vitu vilivyokujenga na kukufundisha,usikate tamaa.
 
Tafuta hii kitabu brow itakusaidia, wengi tumepita kwenye changamoto za kukosa pesa vitabu vimekuwa msaada mkubwa kunibakiza kwenye kusudi. Wakati mwingine dunia lazima ikutest kuona kama uko tayari kubeba majukumu zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mkuu usijali man, step up and be a man, kwanza kabisa nimekukubali kuadmit ukweli hiyo pia huwa ni tiba, pili, haya mambo yanapita tu man jikaze tu mzee baba, ni shtani huyo anataka kukutoa kwenye reli, omba sana na pambana sana mungu ni wa woteee


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Pole sana mkuu najua maumivu unayoyapitia ila mwenyezi mungu hamtupi mja wake uwe na subira.

Mwisho kabisa kisicho kuua kinakukomaza amini siku utakuwa OK.

Sent from my TECNO WX3 using Tapatalk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…