I want to die a judge

I want to die a judge

HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: +18

UTANGULIZI................

SURA YA 1.
MIMI NI NANI?


MZIZIMA,
Mvua zilizokuwa zimeambatana na upepo mkali zilikuwa zikiendelea kulisumbua jiji la bandari ya Salama, jiji la kale ambalo watu wa zamani walilijua kama mzizima. Mvua hizo ziliwafanya Tanesco wapate kisingizio kizuri kabisa cha kuweza kuukata umeme ambao ulikuwa unaimulika mitaa mbali mbali na kuonyesha umaridadi wake.

Kwenye chumba kimoja maeneo ya Kigogo Mwisho alionekana ndani mwanaume mmoja, kuonekana kwake kulidhihirisha wasiwasi na hofu ambayo ilikuwa imeugubika uso wake na simanzi ikauzidisha upole wa ile sura yake ambayo haikuwa ikionekana vyema huenda kwa sababu ya kukosekana kwa mwanga. Uso wake ulitoa taarifa ya kwamba maisha yake hayakuwa salama ndiyo maana alikuwa hana amani wala kuwa na utulivu wa kutosha, alikuwa ameketi kwenye mkeka ambao ulikuwa umetandikwa chini kwenye chumba kidogo cha hovyo ambacho kiligubikwa na joto kali kwa kukosa nyenzo mhimu za kupambana na joto. Sanjari na hilo udogo wa chumba nao ulichangia kwa kiasi kikubwa.
Mwanaume yule alijizoa kutoka kwenye ule mkeka na kusimama, alijisogeza kwenye dirisha dogo ambalo lilifunikwa kwa tambala kuu kuu lilolokuwa chafu, alifunua kidogo pazia hilo ili kujua kama nje kulikuwa na chochote lakini hakufanikiwa kuona jambo lolote lile zaidi ya radi ambazo zilikuwa inamulika kila wakati kwenye kiza totoro kilicho lifanya jiji hilo kuwa na utulivu ambao sio kawaida yake. Alirudi tena kwenye mkeka wake akiwa anatweta kwa jasho kutokana na joto kali huku akiwa anajifuta jasho hilo kwa kutumia shati lake ambalo lilikuwa mwilini.

Akiwa anaendelea kuhema kwa hesabu maalumu ambazo alizijua yeye na nafsi yake, alihisi kama kuna kitu kinamtekenya kwenye mfuko wake wa suruali, hapo ndipo akakumbuka kwamba kwenye mfuko huo alikuwa amehifadhi kisimu kidogo ambacho alikuwa amekifunga funga kutokana na uchakavu ambao kilikuwa nao. Aliipokea haraka simu hiyo ambayo namba yake haikuwa na jina na kuiweka kwenye sikio lake.
"Ondoka haraka kwenye hilo eneo, una dakika kumi na tano tu za kuyaokoa maisha yako, vinginevyo unakufa" sauti ya upande wa pili iliongea kwa msisitizo kisha simu ikakatwa. Alibaki kwenye mshangao mithili ya mtoto ambaye alikuwa ametelekezwa na mama yake mzazi huku akiamini kwamba alikuwa na usalama wa kutosha kwa sababu mama yake alikuwa karibu.

Alijizoa kivivu huku moyo wake ukiwa unamuenda mbio, alisogea kwenye ule mkeka na kuukunja upande wa juu ambapo eneo hilo kulikuwa na udongo ambao ulijazwa, aliufukua haraka haraka na kukitoa kimfuko cha plastiki. Alikifungua na ndani yake kulikuwa na pesa za kigeni maarufu kama dola huku pembeni yake kukiwa na bastola moja pamoja na kisu kimoja. Alizoa pesa haraka haraka na kuzitupia kwenye mfuko wake, bastola akaipachika kwenye kiuno chake huku kisu akikishika mkononi.
Alipafukia kama alivyokuwa amepakuta mwanzo na kuurudishia ule mkeka kwa mara nyingine tena kisha akanyanyuka na kuanza kutoka nje. Baada ya kufika mlangoni alikuwa amepoteza dakika tatu tayari, aliufungua mlango taratibu kisha akaangaza kila upande ili kuona kama angefanikiwa kuona kile ambacho alikuwa ameambiwa kinaenda kutokea lakini hali ilikuwa shwari kabisa hivyo akajitosa kwenye maji ya mvua na kuanza kutembea haraka haraka ili kuelekea kilipokuwepo kituo cha magari.
Alikunja kona ya kwanza akiwa anapishana na sauti ya kudondoka kwa maji, akakutana na uwazi ambao ulikuwa na mita kama kumi na tano, sehemu ambayo ilimshtua kidogo kwa sababu moyo wake ulimuenda mbio isivyokuwa kawaida. Alitembea haraka haraka ili aweze kulivuka eneo hilo salama huku kwenye mkono wake kisu akiwa amekishikilia vyema, ila hakupiga hatua hata kumi akahisi kabisa kulikuwa na harufu ya mtu ndani ya eneo hilo hali ambayo ilimfanya kupunguza mwendo na kumfanya aanze kutembea taratibu.

Aligeuka kuangalia nyuma yake, hakuona kitu zaidi ya anga ambalo lilikuwa linamcheka hivyo akahitaji kuendelea na safari yake tena lakini nafsi iligoma kabisa, moyo wake ulikuwa mzito na hakuwa mtu wa kuupuuzia huo mlango wake wa sita ambao ulikuwa wa hisia. Alishuka chini kama anajilaza kifudi fudi lakini hakufika chini kwa sababu ule mkono wenye kisu ndio ambao ulitangulizwa kisu ndicho kikafika chini na hata baada ya kufika pale chini kwa mkono wake hakuzubaa, alijigeuza kwa sarakasi kwa kuuviringisha mwili wake hali ambayo ilimfanya atue pembeni.

Mahesabu yake yalikuwa sahihi kwa sababu wakati anashuka pale chini, juu yake kilipitishwa kisu kutoka kwenye mikono ambayo ilionekana kuwa na nguvu kubwa na lengo la mtu huyo halikuonekana kuwa kumzimisha tu bali alikuwa anahitaji kuondoka na nafsi yake moja kwa moja. Hata baada ya kutua pale chini hakuzubaa kwa sababu alijua huenda akampa adui nafasi nzuri ya kuweza kufanikisha jambo lake kitu ambacho hakutaka kiweze kutokea kwake yeye ndiyo maana alijiviringisha kwa sarakasi na kutua pembeni. Kujiviringisha kwake kulimfanya kulikwepa buti zito la ngozi ambalo lilikuwa limeshushwa na mwanaume ambaye alionyesha kuwa na uhasama naye mkubwa mithili ya mtu ambaye alimuibia mkewe, buti hilo kama lingefanikiwa kutua kwenye mgongo wake basi asingefanikiwa kutembea tena kwenye maisha yake yote.

Kiza kinene kilimfanya mwanaume huyo ashindwe kumtambua mwanaume ambaye alikuwa amekuja mbele yake ila mwanga wa radi ulimumulika mtu huyo ambaye bila shaka alikuwa ni mweusi usoni akiwa kwenye ghadhabu isiyo pimika. Aliukunjua mkono wake ambao ulikuwa na kisu kwa sababu alijua kwamba anatakiwa kufa wakati huo asipo yatetea maisha yake, hakupata muda wa kutosha wa kupiga tathmini juu ya uwezekano kama alikuwa anamfahamu mwanaume huyo kwa sababu alikuwa anamjia kwa kasi pale alipokuwepo huku mabuti yake yakiwa yanapiga piga kwa nguvu kwenye maji ambayo yalikuwa yametuama chini.
Miguu yenye nguvu miwili ilikuwa inakuja kwenye uso wake, kama bahati tu, tope lililokuwa chini lilimsaidia kuteleza kidogo na kurudi nyuma hali ambayo iliifanya miguu hiyo kumkosa na badala yake akarushiwa maji machafu usoni ambayo yalimuingia kwenye macho. Mtetemo wa ardhi aliusikia vyema baada ya ile miguu ambayo ilimkosa kutua chini na kukita kwa nguvu. Aliyafumbua macho yake haraka ili kujilinda, alichelewa kwenye mahesabu, ngumi ilizama kifuani na kumfanya ahisi kama kuna mtu alimpasua na shoka.

Ndiyo kwanza kabisa tunaufungua utangulizi wa simulizi hii mpya ya NAFSI ZILIZO TELEKEZWA. Hii ni simulizi bora zaidi kati ya simulizi zangu tisa za kijasusi ambazo nimeziandika.
Ndani yake utakutana na stori kali zilizo simama, utakutana na watu kutoka mataifa makubwa na mashirika makubwa ja kijasusi duniani hususani IRINA ESPANOVICH, mwanamama kutoka ndani ya KGB ambayo alikuja akaiweka Tanzania kwa mkono wake baada ya kutoroka nchini mwake akiwa anatafutwa kwa nguvu na Moja ya mashirika makubwa duniani, shirika la kijasusi la Uruai KGB kwa kuwasaliti wenzake na kufanya Umoja wa nchi za kisovieti kudondoka mwaka 1991.

Kutoroka kwake ukawa mwanzo wa kuanzisha jamii ya hatari ndani ya TANZANIA ambayo ilifahamika kama LUNATIC SOCIETY. IRINA alifanikiwa vipi kuwakimbia watu wa kutisha hao wa KGB kwa kuwasaliti mbele ya CIA halafu akafanikiwa kufika Tanzania?
Hiyo jamii ambayo aliianzisha ilikuwa inajishughulisha na nini hasa na mwisho wake ulikuwaje?
IRINA ni nani hasa na alifanya usaliti wa namna gani mpaka KGB wamsakame kila kona ya ulimwengu huku yeye akipotelea Tanzania?

Hizo NAFSI ZILIZO TELEKEZWA Zina maana ipi na ni NAFSI za nani na nani?

Maswali ni mengi lakini ungana NAMI wakati huu uweze kusoma simulizi yangu bora kuliko zote ambazo nimeziandika. Ipo tayari kuanzia muda huu.

Bei yake ni shilingi 6000 tu za kitanzania unajipatia nakala yako kwa mfumo wa softcopy (pdf) kwa kulipia kwa namba hizi hapa.

0621567672 (HALOPESA)..... WHATSAPP

0745982347 (M-PESA)

0714581046 (TIGO-PESA)

0689440143 (AIRTEL MONEY)

Zote jina ni FEBIANI BABUYA
IMG-20240526-WA0009.jpg
 
NINI SIRI YA NAFSI ZILIZO TELEKEZWA?

Inahusu nini, inamhusu nani, kipi kipo nyuma yake? Ungana nami kwenye mtiririko huu uweze kuelewa NAFSI ZILIZO TELEKEZWA inahusu nini.

Mwaka 1991, ni mwaka ambao umoja wa nchi za Kisovieti ulidondoka baada ya kushindwa kwenye vita baridi dhidi ya watu wa Magharibi hususani Marekani. Baada ya vita hiyo kuisha kulikuwa na sababu nyingi sana zilizo wafanya washindwe ikiwemo utaifa na mchango wa nchi za magharibi.

Kwa madhara makubwa ambayo yalipatikana, nchi ya Urusi ilikaa chini kufanya tathmini ili kujua ni wapi walifanya makosa mpaka jambo hilo likatokea nchini mwao. Moja kati ya sababu kubwa ambazo walizipata ni kufeli kwa shirika lao la kijasusi la KGB kushindwa kutekeleza majukumu yake ya kiusalama kwa asilimia miamoja, waliamini kwamba huenda kama shirika hilo lingekuwa imara mapema na kutekeleza majukumu yake kwa usahihi basi wangeishinda vita hiyo.

Sasa mjadala ukawekwa mezani, walishindwaje? Ndipo ikanukia harufu ya usaliti ndani yao, iligundulika kwamba ndani ya shirika lao kuna watu ambao walikuwa wasaliti na usaliti wao ndio ambao ulifanya shirika hilo kuyumba na kufeli. Sasa wasaliti walikuwa nani na nani? Jina ambalo lilitokezea kwenye makablasha yao ni jina la mwanamke wa miaka ishirini na mitano (IRINA ESPANOVICH). Sasa IRINA ni nani na alitokea vipi kwenye hiyo orodha ya wasaliti?

IRINA ESPANOVICH alikuwa ni jasusi mbobevu ndani ya shirika hilo, Moja kati ya wapelelezi ambao waliaminika mno kiasi kwamba akapata bahati ya kuolewa na moja kati ya maafisa wakubwa ndani ya shirika hilo la KGB. Kuolewa kwake na kiongozi mkubwa wa shirika hilo ikawa nafasi ya yeye kupata taarifa nyingi na za siri za shirika hilo kwa njia ya kawaida ama kuziiba kwa sababu huyo mwanaume alikuwa akiishi naye nyumba moja. Sasa kwenye ule mchakato wa kuwatafuta wasaliti, waligundua kwamba kuna akaunti ndani ya Urusi ilipokea mabilioni ya fedha kutoka ndani ya nchi ya Marekani na walipo jaribu kuichunguza akaunti hiyo ili wajue sababu ya msingi ya pesa nyingi kiasi hicho kutumwa kwa mtu ambaye taifa lake lilikuwa vitani na nchi hiyo ni ipi! Ndipo wakagundua kwamba akaunti hiyo ilikuwa inamilikiwa kwa siri na mwanamke huyo IRINA ESPANOVICH.

Baada ya kuunganisha doti, wakagundua kwamba hizo pesa zilitoka ndani ya shirika la kijasusi la Marekani CIA ambalo wengi huwa wanaamini kwamba ndilo shirika namba Moja kwa ubora zaidi duniani kutokana na kuwa na bajeti kubwa ya uendeshwaji wake. IRINA alipokea pesa nyingi ambazo hata angefanya kazi miaka mia-moja asingeweza kuzipata, CIA wamtumie pesa kama nani? Ikahitimishwa kwamba huyo ndiye msaliti ambaye alikuwa akiwauza kwa CIA ndiyo maana walifeli hivyo ikatolewa amri kwamba asakwe popote alipo, akamatwe, ateswe kisha auawe mrembo huyo.

Bahati ikawa upande wake, mlinzi mkuu wa mumewe akampatia taarifa kwa simu kwamba Maam you are to be killed (unatakiwa kuuawa) hawa watu wanajua kila kitu hivyo KIMBIA (RUN). Alikuwa hatarini hivyo hakuwa na muda wa kupoteza akapotea haraka, KGB hawakumpata mwanamke huyo hivyo ukaanza msako wa kimya kimya kwa sababu waliogopa kuziweka taarifa hizo wazi kwani zingewavua nguo kwa kuonekana ni wazembe mpaka yote hayo yanatokea na hawana taarifa! Hawakutaka aibu wakaamua kuifanya siri kumtafuta huyo DOUBLE AGENT IRINA ESPANOVICH.

Kupotea kwake Urusi mikononi mwa KGB ambao walimpachika jina la LUNATIC GIRL, ukawa mwanzo wake wa kuingia ndani ya nchi ya Tanzania. Kwanini iwe Tanzania? IRINA alipiga hesabu zake akagundua kwamba kama angeenda nchi kubwa hususani ambazo zina usambaaji wa taarifa haraka wangekuja kumpata tu siku moja hivyo alihitaji kuishi sehemu ambayo hata KGB wenyewe wasingeidhania kwamba anaweza kuwepo na ile amani ambayo imetawala Tanzania ikamvutia kuishi hapa kwani ingekuwa ni ngumu kuja kujulikana kwamba yupo hapa. Yes, mpango ulikuwa sahihi sasa Tanzania angeishije na angeweza vipi kujilinda? Ukawa mwanzo wa kuanzisha jamii ya Siri ambayo aliiita LUNATIC SOCIETY, jina ambalo alipewa na KGB kwa usaliti wake. Kumbuka alikuwa mgeni hivyo asingeweza kuianzisha jamii hiyo mwenyewe ikamlazimu kumtafuta mtu.

Macho yake yakadondokea kwa Novack Nyangasa, mdogo wa raisi wa Tanzania ambaye aliamini angekuwa na nguvu ya kumpeleka anapo pataka yeye. Alimshawishi mwanaume huyo kwa urembo wake na kumpa mpango mzima juu ya utajiri ambao wangeenda kuutengeza, Novack akatokwa na mate ya uchu, akakubali. Jamii hiyo ikaanzishwa kwa nguvu ya mdogo wa raisi ambapo waliwasajili watu wakubwa; wanasiasa wakubwa, maprofesa, wanafalsafa, madaktari bingwa, wafanya biashara wakubwa na kila ambaye walimuona anafaa. Baadae raisi akazipata habari, akachukia sana na kumuita mdogo wake IKULU.

Akamtaka aifute jamii hiyo kwa mwezi mmoja tu pekee, huo mwezi ukatumika kummaliza yeye, raisi akawekwa kati akatakiwa kufa ili jamii hiyo iwepo. Moja kati ya mipango mikakati ambayo waliiweka ili kujilinda ni kuanzisha chuo cha kuwatengeneza vijana hatari kwa ajili ya ulinzi na kufanya kazi yao kwa nguvu pale ambapo ingebidi, zoezi hilo likatua mikononi mwa jasusi wa zamani wa Tanzania ambaye aliachana na kazi hiyo baada ya kuhusika na mauaji ya watu wengi sana, NIKOLAI GIBSON. Mwanaume huyo kwenye moja ya mazao yake alifanikiwa kumtengeneza kijana wa kuitwa YOHANI MAWENGE, bwana mdogo ambaye alimuokota Tandale kwa Tumbo akililia mapenzi na kutaka kujiua kisa uchi wa mwanamke.

Alimfunza namna ya kuwa mwanaume akampa begi la pesa akale maisha kwa mwezi mzima, alale na wanawake warembo ambao aliishia kuwaona kwenye runinga ili ushamba umtoke kisha baada ya hapo alikuwa na kazi naye. Alitengenezwa kikawa kiumbe cha kutisha na Kazi yake ya kwanza ikawa kwenda kumuua mcheza KAMARI mmoja huko BAMBALI Senegal na alitakiwa kurudi na bilioni 30 zilizokuwa mkononi mwa bwana huyo..... Huyu tuna mengi ya kuyasoma kwake ni mhimu sana.

Ukawa mwanzo wa mwanamke huyo wa KGB kuitawala Tanzania kwa miaka takribani thelathini. Lakini baadae Moja kati ya makosa makubwa ambayo waliyafanya ni kumuua mwanasayansi aliyedaiwa kuwa binadamu mwenye akili zaidi nchini.

NAFSI ZILIZO TELEKEZWA ni zipi na za nani?
Kulikuwa na utata wa maisha ya mwanaume Edison, bwana ambaye hakuwa na kumbukumbu na kwenye mfuko wake alikuwa anatembea na picha ambayo walidai ni ya mkewe, bwana huyu alikuwa akishangaa kwa sababu yeye binafsi hakuwa na kumbukumbu yeyote kama aliwahi kuwa na mke au familia. Kitu cha kushangaza kwa EDISON ni kwamba alikuwa anatafutwa ili auawe kuliko hata pesa inavyo tafutwa na maskini mpaka yeye mwenyewe akawa anashangaa.

Hali hiyo ilimlazimu kwenda kuishi maisha ya chini sana huko Kigogo Mwisho ili awe salama kwani hakuna ambaye angempata kirahisi akiwa kwenye maisha ya kifukara huko lakini usiku mmoja mvua ikiwa inanyesha akiwa ndani ya kijumba kibovu kwenye mkeka, anapokea simu ambayo ilimtaka atoweke eneo hilo kwa dakika kumi na tano vinginevyo angekufa. Aliduwaa ila hakuwa na namna aliondoka haraka ila kabla hajafika mbali akavamiwa na wanaume wa kutisha ambapo alimuua mmoja akafanikiwa kutoroka.

Safari yake ikawa ni kwenda kwa mlezi wake ambaye ndiye alimpa taarifa hiyo na ndiye alimtaka akaishi huko Kigogo mapaka mambo yakae sawa ili akampe ukweli wa kwanini anatafutwa sana? Kufika kwa huyo mlezi wake ambaye alikuwa ni mchungaji wa KKKT pale Mabibo Mwisho karibu na hosteli za wanafunzi wa NIT, alimkuta mtu huyo yupo kwenye hatua za mwisho za uhai wake. Hakumwambia kitu zaidi ya kumtaka aende nyumbani kwake kwenye banda la mbwa akachukue kitabu ambacho kingemfunulia ukweli kwamba yeye ni nani, kwanini hana kumbukumbu, maisha yake kabla yalikuwaje na kwanini anatafutwa sana na watu ambao yeye alidai hawajui!

EDISON alishangaa baada ya kuambiwa kwamba anatafutwa kwa kuhusika na mauaji ya makomando TISA wa kikosi maamulu cha KOM (KILL ON MISSION).akabaki ameduwaaaa!!!!!!!

Ilishawahi kukukuta kwenye maisha yako ukatakiwa kumuua mama yako mzazi kwa mkono wako mwenyewe? Hilo ni jambo baya na gumu lakini Yes, kuna mwanaume alitakiwa kumuua mama yake aliye mzaa ili nchi iwe salama. Je huyu naye hatima yake ilikuwaje?

Kuna uhusiano gani kati ya hizo NAFSI ZILIZO TELEKEZWA, IRINA ESPANOVICH na EDISON?

Unataka kumjua zaidi IRINA ESPANOVICH? Unataka kuijua kiundani LUNATIC SOCIETY? Unataka kujua uhalisia wa maisha ya EDISON kabla na baada ya hapo? Hizo nafsi ZILIZO TELEKEZWA ndizo hizo za makomando TISA (9) ambao alidaiwa kuwaua au kuna mengine nyuma ya mlango wa siri? Ungana nami kwenye simulizi yangu bora zaidi kuwahi kuiandika kwa mkono wangu.

1. Storyline yake ni kali sana
2. Dialogue (majibizano) yake ni kali sana.
3.Haitabiriki kabisa (huwezi kutabiri kinacho tokea baadae)
4.Lakini pia ina actions kali mno.

Simulizi hii imetoka tayari na unaweza kuipata kwa shilingi ELFU SITA (6000 tu za kitanzania). Unaweza ukalipia 6000 yako kwa namba hizi ili uipate muda huo huo. Inapatikana kwa Softcopy.

0621567672 (HALOPESA)..... WhatsApp.
0745982347 (M-PESA)
0714581046 (TIGO-PESA)
0689440143 (AIRTEL MONEY)

FEBIANI BABUYA

Lipia muamala wako Kisha nicheki nikutumie yote, ama unaweza ukanicheki WhatsApp, ukatuma sms ama ukapiga cm kama utakuwa na swali lolote.

CIAO.
FB_IMG_1716969749372.jpg
 
Back
Top Bottom