Ibara ya 15:1 na 2

Naoana Waheshimiwa mnajadili TEXT ya ibara hiyo badala ya CONTEXT!
You are very clever!
 
Naoana Waheshimiwa mnajadili TEXT ya ibara hiyo badala ya CONTEXT!
You are very clever!

i think to remove some ambiguity, both context and text matter
 
Wasababishaji wa matatizo yetu ni sisi wenyewe...

Nakubaliana na wewe mkuu...

Ila ndo hapa kinachojadiliwa....matatizo yetu ni sisi wenyewe. Sisi....inamaanisha maisha yetu, mifumo yetu ambayo ndo vyama vyetu, etc..

Kama CCM ambayo ni sehemu ya baadhi ya 'sisi' ina ubovu, tatizo litatokea au kama lipo litaendelea kuwepo...
 
Wakuu hiyo katiba ya CCM ilibuniwa na kuandikwa na Mwalimu mwenyewe, sasa hatuhitaji spin kwenye hili sasa kama hii katiba ya CCM ndio chanzo cha taifa letu kudumaaa kimaendeleo, then there you go,

Otherwise, matatizo yetu ni sisi wenyewe wananchi na viongozi, hapa tulipofikia hakuna wa kumlamu zaidi yetu sisi wenyewe, sasa ungetegemea by sasa tuwe tunajaribu ku-get things right wapi, ndio kwanza tunaiilia katiba ya CCM, ambayo hata Mwalimu mwenyewe never respected it. He only did things his ways, sasa nashangaa kwamba hata hatuelewi kuwa maneno ya kuweka chama cha siasa mbele kuliko taifa, hatuelewi yaliwekwa na nani,

Wakati Mwalimu, anampigia debe Mkapa kuwa rais, hivi mnakumbuka exactly maneno aliyokuwa akiyasema, ni haya haya ya kuweka CCM mbele kabla ya taifa, sasa kama wameamua kuyaenzi basi we are dooomed! Haya maneno ya katiba ya zamani yalikuwa goood only kwa nidhamu tu ya viongozi, lakini hayakutuletea maendeleo ya taifa, meaning kwamba ni wakati muafaka sasa wa kuachana nayo na kurudi kwenye utawala wa kuheshimu sheria za jamhuri.

Wazungu wanasema you cannot be wrong and get it right!
 
CCM kama chama kilichopewa dhamana ya kuongoza Tanzania, tulitegemea kuanzia kwenye katiba yake ingekuwa na lengo hilo hilo liwe msingi wake nambari moja.....kulitumikia Taifa letu kwa moyo mmoja.

Kumbe tumewaweka madarakani watu ambao maslahi yetu yanakuja baada ya yakwao??

Hivi na katiba za vyama vingine (CHADEMA, CUF etc) zikoje?? usikute nako kuna huu utumbo...
 

Nashukuru sana baada ya baadhi yenu kukubaliana nami .Mtanzania sasa nadhani umeona why Lunyungu aliyasema haya .Hata JK akiwa katika Ziaraya Kiseikali yeye huifanya ya mzaha kama yuko kwenye NEC.Chunguza utaona mie najionea kila siku.Ndiyo maana nakubaliana na wengine kwamba Kwa JK na wengine CCM kwanza .

Naomba kuuliza .Kumbe Katina ya CCM iliandikwa na Mwalimu peke yake ?Maana inaweza kunisaidia kuelewa mengi ama kuuliza mengi.
 
Nionesheni nchi yenye Katiba mbaya na imeendelea na nitawaonesha nchi yenye katiba mbovu na haijaendelea. Huwezi kuwa na Katiba mbovu ukategemea maendeleo, lakini ukitengeneza Katiba nzuri unafungulia msingi wa maendeleo..

Katiba ya makaburu wakati wa Apartheid...
 
Wakuu hiyo katiba ya CCM ilibuniwa na kuandikwa na Mwalimu mwenyewe, sasa hatuhitaji spin kwenye hili sasa kama hii katiba ya CCM ndio chanzo cha taifa letu kudumaaa kimaendeleo, then there you go,

Mzee, walioshiriki kuandika Katiba ya CCM wanajulikana mmoja wao ndio aliyesoma maazimio ya CCM Butiama. Nyerere hakukaa chini kubuni na kuandika Katiba hiyo.


Mzee, hapa hatuzungumzii Katiba ya Muungano tunazungumzia Katiba ya CCM. Katiba ya Muungano ni chanzo cha matatizo mengi ya nchi na Taifa, Katiba ya CCM ni chanzo cha matatizo mengi kwa CCM yenyewe na kwa vile wao ndio chama tawala basi by inference matatizo yaliyoko kwenye Katiba ya Taifa na hivyo matatizo ya utawala wetu. Katiba ndio msingi wa maisha ya taifa lolote lile.

He only did things his ways, sasa nashangaa kwamba hata hatuelewi kuwa maneno ya kuweka chama cha siasa mbele kuliko taifa, hatuelewi yaliwekwa na nani,

wrong again mzee, Katiba niliyonukuu ya CCM ni toleo la 2005, nikukumbushe kuwa Mwalimu alifariki mwaka 1999! Na hii ya Taifa mabadiliko ya mwisho ni 2004!


Nakubaliana na wewe on principle, lakini kwa kadiri ya kwamba Wajibu wa kwanza wa mwana CCM ni kuilinda na kuienzi CCM we are already doomed.


[/quote] Wazungu wanasema you cannot be wrong and get it right![/QUOTE]

Well, wazungu wanasema mengi sana...
 
Upande gani? unanionesha Katiba mbovu na nchi iliyoendelea, au Katiba nzuri na nchi isiyoendelea..?

Separate but equal...hiyo haikuwa kwenye katiba? Kama ilikuwepo kwenye katiba basi hiyo katiba ilikuwa mbofu lakini uchumi wa nchi (kwa ujumla) uliweza kushamiri.
 
Separate but equal...hiyo haikuwa kwenye katiba? Kama ilikuwepo kwenye katiba basi hiyo katiba ilikuwa mbofu lakini uchumi wa nchi (kwa ujumla) uliweza kushamiri.

mzee nilisema wapi kuwa Katiba nzuri inahusiana na uchumi mzuri?
 
mzee nilisema wapi kuwa Katiba nzuri inahusiana na uchumi mzuri?

Unaposema maendeleo unamaanisha nini sasa?

Wewe ndio umesema huwezi kuwa na katiba mbovu na ukategemea maendeleo...niambie basi hayo maendeleo kwako ni yapi....
 
Unaposema maendeleo unamaanisha nini sasa?

Wewe ndio umesema huwezi kuwa na katiba mbovu na ukategemea maendeleo...niambie basi hayo maendeleo kwako ni yapi....

Nyani, nilidhani muda wote huu utakuwa umeelewa mawazo yangu kuhusu maendeleo; maendeleo ni ya watu na si vitu. Katiba nzuri inaendeleza watu siyo vitu. Yaani, vitu vinatumika kuendeleza watu na hapa watu nina maana jamii nzima ya watu wa nchi ile na siyo kikundi kimoja cha watu.
 

Kwa hiyo basi katiba ya Marekani nayo sio nzuri maana kuna idadi kubwa ya raia wake ambao hawana maendeleo. Leo nimesikia redioni kuwa katika kila sekunde 29 kuna mwanafunzi wa high school ana drop out! Hapa nilipo kwa mfano ni asilimia 44 tu ya wanafunzi wa high school wanaomaliza mafunzo. Hii ni asilimia chini ya hamsini! Kwa mtaji huo basi hata katiba ya Marekani si nzuri...hasa ukiangalia mambo mengine kama welfare, teenage pregnancy, idadi ya watu wanaoishi chini ya mstari wa umaskini n.k.....
 

Je, wanashughulikiaje matatizo uliyoyaanisha kuhakikisha kuwa hata dropout wanafanikiwa? Je wanafanya nini kutoa nafasi hata kwa waliopata mimba kuendelea na masomo? Je kuna program ngapi za kuwapa watu second chance katika maisha badala ya kuwa condemned to life of misery?

Katiba ya Marekani ni nzuri lakini siyo kamilifu, lakini imesimamia maendeleo makubwa ya watu wa Taifa hili. Katiba nzuri haina maana itaondoa matatizo yote, bali itatoa nafasi ya kuhakikisha kuwa matatizo yanashughulikiwa kwa mujibu wa sheria na taratibu.

Hapa tunavyozungumza nimesilikiza ripoti hiyo hiyo ya NPR kuhusu hali ya elimu kutoka America's Promise na nilikuwa natatizika na contradiction which is the American society. Marekani ni alama ya ukingano, na ndiyo matokeo ya Katiba nzuri.

Hivyo Katiba nzuri siyo tu inafanya jamii iliyoendelea iwepo, bali inafanya iwezekane iwepo.
 
Hicho kifungu in question kiliandikwa/ kiliwekwa lini kwenye hiyo katiba ya CCM?
 
Mzee, walioshiriki kuandika Katiba ya CCM wanajulikana mmoja wao ndio aliyesoma maazimio ya CCM Butiama. Nyerere hakukaa chini kubuni na kuandika Katiba hiyo.

Mkuu nijuavyo ni kwamba katiba ya CCM originally iliandikwa na Mwalimu, mwaka 1977 kisiasa alitakiwa kuwa ameiandika na Jumbe, aliyekuwa makamu na rais wa Afro Shirazi, I mean that never happened kwa sababu kama Jumbe amngekuwa alishiriki, basi Mwalimu asingekuja kumtema baadaye as he did kutokana na Jumbe kutokubaliana na maamuzi mengi ya mbio mbio ya Mwalimu, ambayo ndio hasa yanatusumbua sasa hivi,

Kama kuna viongozi walishirikiana na Mwalimu, kuandika ile katiba, basi walikuwa ni wasindikizaji tu au hawakuwa na uwezo kabisa wa kufikiri, maana ukifuatilia maneno the founding fathers wa US, kina Madison, Hamilton, George Washington mwenyewe, utagundua kuwa walikuwa ni watu wenye kuona mbali sana, ndo maana huko ma-US hakuna noma kila kitu kipo kwenye sheria,

Katiba ya CCM hata ibadilishwe vipi, siku zote ni lazima ifanane ma mawazo ya Mwalimu, we all rememmber maneno aliyokuwa akiyasema 1995, wakati wa kampeni I mean mengine ni aibu hata kuyarudia akisema kuwa CCM ni lazima itawale bongo, upinzani ni good tu for sidelines, Mrema agombee ubunge tu, mtu ambaye alikuwa deputy Prime minister, I mean my point ni kwamba all in all Mwalimu, ndiye muanzilishi wa haya mawazo ya chama kwanza kuliko taifa, chama kushika hatamu, ili kuondokana na haya mawazo kwanza ni lazima tuanze na ku-denounce yalikotokea, otherwise, tutaendelea kudanganyana tuu!
 
Mzee mwenzangu ndio uchovu wenyewe nini maana leo reasoning yako kidogo ina kutu kidogo. Nitachukulia ni majukumu mengi mzee.

Mkuu nijuavyo ni kwamba katiba ya CCM originally iliandikwa na Mwalimu, mwaka 1977

Mzee hili la "ujuavyo" ni vigumu kubishana nalo kwani sijui msingi wa ujuzi wako huo ni nini. Uliona Nyerere akiandika Katiba hiyo, ulisikia Nyerere ndiyo kaandika, ??

Ukiondoa usahihi wa mwaka wa Katiba hiyo nadhani habari nyingine hujazipatia. Ngoja nikupatie tamko lililotolewa na mkutano mkuu wa 1977 wa vyama viwili vya TANU na ASP.

Kwa hiyo basi:-
(1) Sisi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa
pamoja wa TANU na ASP tuliokutana leo
tarehe 21 Januari, 1977 mjini Dar es Salaam,
chini ya uongozi wa pamoja wa Mwalimu Julius
K. Nyerere Rais wa TANU na Ndugu Aboud
Jumbe, Rais wa ASP, kwa kauli moja tunaamua
na kutamka rasmi kuvunjwa kwa Tanganika

African National Union (TANU) na Afro Shirazi
Party (ASP) ifikapo tarehe 5 Februari, 1977, na
wakati huo huo kuundwa kwa Chama kipya cha
pekee na chenye uwezo wa mwisho katika
mambo yote kwa mujibu wa Katiba.

(2) Vyama vya TANU na ASP vinavunjwa kwa
taadhima kubwa. TANU na ASP havikuamua
kujivunja kama vyama kwa kuwa vimeshindwa
kutekeleza jukumu lao. Kwa hakika TANU na
ASP ni Vyama vilivyopata mafanikio ya kipekee
katika Afrika katika kulitekeleza jukumu la
kihistoria na mafanikio hayo ndiyo leo
yamewezesha kitendo hiki cha Vyama viwili
kujivunja vyenyewe. TANU na ASP
vitaheshimiwa siku zote kama viungo muhimu
katika Historia ya Mapambano ya Ukombozi wa
Taifa letu na wa Bara la Afrika, na waanzilishi wa
TANU na ASP watakumbukwa daima kama
mashujaa wa taifa letu waliotuwezesha leo
kupiga hatua hii ya kufungua ukurasa mpya
katika Historia ya Tanzania.

(3) Tumeamua kwa pamoja kuunda Chama kipya
cha kuendeleza mapinduzi ya kijamaa nchini
Tanzania na Mapambano ya Ukombozi wa Afrika
juu ya misingi iliyojengwa na TANU na ASP.
Chama tunachokiunda tunataka kiwe chombo
madhubuti katika muundo wake na hasa katika fikra
zake na vitendo vyake vya kimapinduzi vya kufutilia



kisiasa alitakiwa kuwa ameiandika na Jumbe, aliyekuwa makamu na rais wa Afro Shirazi, I mean that never happened

Tamko la mkutano mkuu limejibu hilo so your "never" is not really "never" for it did happen.

kwa sababu kama Jumbe amngekuwa alishiriki, basi Mwalimu asingekuja kumtema baadaye as he did kutokana na Jumbe kutokubaliana na maamuzi mengi ya mbio mbio ya Mwalimu, ambayo ndio hasa yanatusumbua sasa hivi,

Mzee hii reasoning leo ikoje? Mbona Lowassa katemwa na walikuwa kwenye makubalianao huko nyuma na JK? Watu wanaweza kufanya kazi pamoja leo lakini uko mbele ikabidi waachane, so sioni hii hoja yako nguvu yake iko wapi.


Kama kuna viongozi walishirikiana na Mwalimu, kuandika ile katiba, basi walikuwa ni wasindikizaji tu au hawakuwa na uwezo kabisa wa kufikiri,

Nadhani hicho ni kiwango cha juu cha dharau mzee; maana ningependa kweli kujua majina ya watu wote waliokuwemo kwenye kamati iliyoandika Katiba ya CCM.

maana ukifuatilia maneno the founding fathers wa US, kina Madison, Hamilton, George Washington mwenyewe, utagundua kuwa walikuwa ni watu wenye kuona mbali sana,

Ni kweli waliona mbali lakini siyo mbali kupita Utumwa kwani waliposema kuwa "binadamu wote wameumbwa sawa" hawakumaanisha na watumwa! Lakini hilo haliondoi ukweli wa mchango wao katika mfumo wa Katiba ya sasa na uthibitisho kuwa hata watu wakubwa na mashujaa kama kina Hamilton, Jefferson, Washington na wengine wanaweza kukosea. Nadhani ni sisi tu ambao tunataka kukana kila alichoandika muasisi wa Taifa letu ati kwa sababu "hakuona mbali".

ndo maana huko ma-US hakuna noma kila kitu kipo kwenye sheria,

Mzee kuna noma huku, si unajua kuna mabadiliko mangapi ya Katiba ya Marekani? Je unajua sheria ngapi zimefutwa kwenye mahakama kwa kupingana na katiba?

Katiba ya CCM hata ibadilishwe vipi, siku zote ni lazima ifanane ma mawazo ya Mwalimu,

Si kweli, na kama kuna wana CCM wanaofikiri hawawezi kubadili Katiba yao (kama kukifutilia mbali kipengele hiki) basi wao ni watumwa wa mawazo ya Nyerere. Lakini kama fikra na mawazo ya Nyerere yalikuwa sahihi katika mambo fulani ni ubaya gani kukubaliana nayo au kureflect mawazo hayo? Si leo hii tunajaribu kurudi kwenye miiko ya uongozi na maadili ya uongozi ambayo Nyerere aliyasimamia. Tusifanye hivyo kwa kuogopa kurudi kwenye mawazo ya Nyerere?

we all rememmber maneno aliyokuwa akiyasema 1995, wakati wa kampeni I mean mengine ni aibu hata kuyarudia akisema kuwa CCM ni lazima itawale bongo, upinzani ni good tu for sidelines,

Mzee, Nyerere hakuwahi kusema unayoyasema wewe; Mwalimu alisema kile alichomaanisha, ni kumuwekea maneno ambayo hakuyasema. Naomba unioneshe ushahidi mahali popote ambapo Mwalimua "alisema" kuwa "CCM lazima itawale" Bongo au "Upinzani ni good tu for sidelines". Ukinionesha nitakubali, and believe me I'm a very good student of Mwalimu.

Mrema agombee ubunge tu, mtu ambaye alikuwa deputy Prime minister,
Hapana hakusema "agombee ubunge tu", muulize Mrema akuambie alichosema Mwalimu au angalia ripoti utajua what Mwalimu actually told Mrema na guess what, he was right. Yaani Mrema angekuwa Rais wetu?


yawezekana uko sahihi hapo, lakini kama yeye alikuwa ni mwanzilishi basi tumpe credit ni yeye aliyeanza kuyakataa. Lakini pia inasikitisha kuwa hadi leo kuna wana CCM na akili zao timamu ambao bado ni watumwa wanaoogopa kubadili katiba ya CCM kwa vile "iliandikwa" na Mwalimu. Wana CCM hawa ni aibu kwa watu wote wenye fikra huru. Wananikumbusha wale watu-mashine wa Star Trek wenyewe wanajulikana kama "borgs". (pichani)


Ma bogi wanafanya kazi kama "mmoja" na lolote linalomtokea mmoja mwingine analijua kile wanachokiita "hive mind". CCM wako kama hivyo kiasi kwamba wamefungwa na fikra za Chama kiasi kwamba hawaoni kitu kingine chochote kile.

a. Aliwaambiwa CCM siyo "mama" na akamwambia Kawawa kuwa ana ujasiri sana kwa kuapa kuwa atakufa CCM.

b. Aliwakatalia CCM walipoamua kufuata haki ya wananchi kuchaguliwa bila chama na akaweka haki za raia mbele wakati CCM imebadili Katiba kuzuia hilo, na hadi leo hakuna kiongozi yeyote wa CCM ambaye amepingana na chama chake kuhusu hilo isipokuwa alivyofanya Nyerere.

c. Ni Nyerere aliyekuwa tayari kurudisha kadi ya CCM wakati wamemtumia ujumbe wale jamaa wa kumtetea Lowassa.

Mwalimua aliiweka CCM mbele pale tu CCM ilikuwa inaitumikia nchi kwanza lakini naamini kwa mishipa ya damu yangu yote, kama Mwalimu angekuwepo na kuona waliyoyafanya kina Mkapa, JK na ukimya wa vigogo wengine wa CCM, angerudisha kadi jangwani!! Hakuwa anajikomba kwa mtu yeyote ndani ya CCM.
 
Wewe kweli unampenda Nyerere...
Sitabishana tena na wewe kuhusu yeye...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…