Hapana mkuu, kuna maendeleo makubwa sana mkuu, kama freedom of speech, umiliki wa mali binafsi, tatizo ni kwamba maendeleo haya hawakupata wengi kama ambavyo tungetaka, hasa wananchi wa hali ya chini, lakini mabadiliko yapo mengi sana mkuuu, hivi mkuu huoni kuwa siku hizi wananchi tunakula luninga?
Mzee maendeleo ya vitu yapo na ni kweli kuna watu wachache wameendelea na kauli yangu ya "mbona hatujaendelea" naifuta kwani siku iqualify nilivyotaka. Maendeleo ambayo tunayazungumzia siyo mabadiliko yanayoendana na wakati, yaani kama ulikuwa na shule 20 halafu miaka 10 baadaye ukawa na shule 40 unaweza kusema umeendelea lakini ukweli ni kuwa umekidhi natural demand ya shule.
Sasa isingiwezekana Tanzania kubakia vile ilivyokuwa pasipo mabadiliko ya ongezeko la vitu; je tulivyoongeza ni bora zaidi kuliko tulivyokuwa navyo?
nia yake ingekuwa ni njema kwa taifa, basi angeyasema mwenyewe aliyoyakosea, na aliyeyakosea ni yeye binafsi maana viongozi wengine walikuwa wanafuata upepo tu! Lakini hata siku moja hakusema alikosea wapi, ndio maan sasa tunahangaika tuu hatujui pa kugusa?
Once again, unazungumza kwa uthabiti kuwa "hata siku moja hakusema alikosea wapi" sasa nikikuonesha kuwa aliwahi kusema alikosea wapi utafuta kauli hiyo na hiyo kuthibitisha kuwa hujafuaitilia yote aliyoyasema na unajenga hoja kwa imani siyo facts? Well, nitakusaidia.
Alifanya interview mwezi Disemba 1998 karibu mwaka mmoja kabla ya kifo na aliulizwa na mwandishi wa "New Internationalist Magazine" toleo la 309:
Sehemu ya
Mahojiano ilikwenda hivi:
IB
: What were your main mistakes as Tanzanian leader? What should you have done differently?
MJN: There are things that I would have done more firmly or not at all. For example, I would not nationalize the sisal plantations. This was a mistake. I did not realize how difficult it would be for the state to manage agriculture. Agriculture is difficult to socialize. I tried to tell my government that what was traditionally the family's in the village social organization should be left with the family, while what was new could be communalized at the village level. The land issue and family holdings were very sensitive. I saw this intellectually but it was hard to translate it into policy implementation. But I still think that in the end Tanzania will return to the values and basic principles of the Arusha Declaration.
Mzee katoa mfano! viongozi hawaogopi kukiri makosa na kusema walikosea wapi. Na madai yako kuwa hakuwahi kusema amekosea wapi hayana ukweli, kwa sababu nimekupa mfano mmoja kama hautoshi niombe nitakupa mwingine na mwingine tena.
Mambo ya maazimio ya Arusha, yamepitwa sana mambo ya maadili ya viongozi yamepitwa sana tunatakiwa kuheshimu sheria za jamhuri sio maadili ya CCM
Mzee, nakuomba usome Azimio la Arusha halafu nioneshe ni nini kilichopitwa na nakuhakikisha utakuta kitu kimoja tu ambacho na mimi sikikubali. Azimio bado lina uhai ni wahuni wale walioliua kule leo hii hawana cha kushikilia. Wamebakia kutembelea kaburi.
Maendeleo ya watu mbona yeye mwenyewe yalimshinda kuya-implemment tikaishia kula yanga tu, huku wakubwa na wenye nguvu wakila unga mweupe, angalau sasa hata wanyonge tunapata angalau harufu maana ni hela yako tu, watu walio huru aliwajenga wapi mbona kina Seif Bakari, Seif Hamadi, na Jumbe walipojaribu kuwa huru aliwafukuza? Can you imagine Zitto na Salaa wangekuwepo enzi zile za Mwalimu, saaa hizi wangekuwa wapi?
mzee kujenga Taifa si lelemama, hivi umesoma historia ya Wamarekani? Umeshawahi kumsikia mtu anaitwa Benedict Arnold au watu wengine ambao walikuwa upande wa Mfalme.Kujenga Taifa siyo kula keki, believe me, compared to others around us.. Mwalimu alifanya kazi kubwa kweli, nisingetaka kuzaliwa nchi nyingine yoyote ya kiafrika isipokuwa Tanzania chini ya Nyerere. Hivi unafikiri kina Mkapa ndio wangekuwa Marais wa Kwanza Tanzania ingekuwa ilivyo sasa? thubutu!! tungeuza hadi jengo lenyewe la Ikulu.
Kweli baadhi yetu hatuna shukrani na mchango wa Taifa ambalo leo tunasema tunafurahia. Mzee wakati wa Nyerere tulikula Yanga.. leo hii watu bagamoyo wamekufa kwa kula mizizi!!! Mzee tulikula Yanga na tulikuwa na afya, Ethiopia katika njaa ile ile waliimbiwa "we are the world". Tuwe na shukrani kaka, niishi katika nchi ambayo angalau naweza kula Yanga, kuliko nchi ambayo wachache wanakula pilau wengine tunaishia mizizi. Nenda pale Mwaloni uone ni watu wangapi huishia kuokoteza vidagaa pale, ni wangapi wanakula mapanki (well matamu pia).
Haya ndio baadhi ya maandishi ya Mwalimu, ninayosema kila wakati yalikuwa mazuri kusoma tu, ila kwa sasa yamepitwa na wakati tena sana!
Nakupa changamoto, pick any writing of Mwalimu na unioneshe kuwa yamepitwa na wakati na kwanini yamepitwa na wakati.