Ibara ya 30:5

Ibara ya 30:5

Kuna hukumu vilevile ya Jaji Mwalusanya kuwa hukumu ya kifo siyo halali.

Hukumu hii haijatekelezwa hadi leo.
 
Lazaro kwenye hiyo Ibara ya Katiba ni wapi wametumia neno "kushauri" serikali. Mahakama haina kazi ya kushauri.

Mkjj,

Ref: “Mahakama Kuu ikiona kuwa yafaa au hali au masilahi
ya jamii yahitaji hivyo, badala ya kutamka kuwa sheria au hatua
hiyo ni batili, itakuwa na uwezo wa kuamua kutoa fursa kwa ajili
ya Serikali au mamlaka nyingine yoyote inayohusika kurekebisha
hitilafu iliyopo"

Unaelewaje neno Kuamua kutoa fursa?

Lazaros alikuwa anaelezea, na ndio maama neno kuishauri alilifungua na kulifunga. Ref: Lazaros comment, "Mahakama Kuu itachukua option ya "kuishauri" Serikali irekebishe sheria au hatua inayolalamikiwa."

Lizy
 
Sina uhakika hii inakwendaje lakini miezi miwili au mitatu nimesikia BBC kuwa serikali kupitia kwa AG wamekata rufaa, utashindwa kuelewa serikali inalinda maslahi ya nani hapa.
 
Sina uhakika hii inakwendaje lakini miezi miwili au mitatu nimesikia BBC kuwa serikali kupitia kwa AG wamekata rufaa, utashindwa kuelewa serikali inalinda maslahi ya nani hapa.

Alwaya, wananchi.
 
Ni kweli Mwanakijiji kazi ya Mahakama si kushauri. Lakini wakati wa mabadiliko ya katiba, wataalamu wengi wa sheria walilalamikia kifungu hiki kuwa kinaigeuza Mahakama Kuu kaka advisory body ya Serikali. Just read the clause between the lines, suggestion ni ya kuipa Serikali fursa ya kubadilisha sheria au hatua yenyewe bila kuamriwa na Mahakama! Cheers
 
Kwa ninavyoelewa mimi, and that is just the basics, ni kwamba mahakama ndiyo ina wajibu na uwezo wa ku interpret laws, na moja kati ya kazi hizo ni ku ascertain the constitutionality of the said laws./QUOTE]

You are right Pundit.

Huko Mahakamani kuna Mahakimu/Judges. Wao pia sometimes "Wanamisinterpret laws" na kutoa wrong directions/decisions. Thats why kuna APPEALS ambayo ina uwezo wa ku-quash ama kumaintain decision kwa kutokana na facts za kesi husika na ushahidi wa pande mbili (Prosecution/defence).

Ni appeal court pekee ndiyo yenye uamuzi wa mwisho wa kusitisha sheria itayolalamikiwa. Kwa huku chini, of course wanaweza kuona sheria hiyo haipo sahihi na wakaisitisha, it will only work endapo hakutakuwa na rufani. Please correct me if I am wrong.

Lizy
 
...Mahakama Kuu inapochukua the other option ya kutangaza moja kwa moja kuwa sheria au hatua fulani ni unconstitutional, sheria au hatua hiyo inakuwa unconstitutional mara moja!

Hicho kitu umekitoa wapi?

Hicho ndicho Mwanakijiji hakioni kwenye "Katiba."

Hakimo!

Pundit, "Katiba" ya Tanzania sio sheria Mama ya nchi.

To the extent that Katiba maana yake Sheria Mama ya nchi, kama inavyojulikana duniani kote, Tanzania hatuna Katiba.

Hakuna iliposemwa ndani ya "Katiba" yetu kwamba yenyewe ndio supreme law of the land.

To the contrary, inasema sheria inayopingana na "Katiba" haitakuwa batili!

Shangaa usingae, taka usitake. Hivyo ndivyo Ibara ya 35 inavyosema.

Kuhusu kesi ya Mtikila, hii kesi sio mfano mzuri wa kutumia kuhusha na hili swala kwa sababu haijafikia mwisho bado. Kesi inaisha pale haki zote za rufaa zinapoisha, kama alivyodokeza Lizy. Swali ni kwamba itaisha lini?
 
Mkjj,

Ref: “Mahakama Kuu ikiona kuwa yafaa au hali au masilahi
ya jamii yahitaji hivyo, badala ya kutamka kuwa sheria au hatua
hiyo ni batili, itakuwa na uwezo wa kuamua kutoa fursa kwa ajili
ya Serikali au mamlaka nyingine yoyote inayohusika kurekebisha
hitilafu iliyopo
"

Unaelewaje neno Kuamua kutoa fursa?

Lazaros alikuwa anaelezea, na ndio maama neno kuishauri alilifungua na kulifunga. Ref: Lazaros comment, "Mahakama Kuu itachukua option ya "kuishauri" Serikali irekebishe sheria au hatua inayolalamikiwa."

Lizy

Hapo maana yake mahakama ina discretion,yaani inao uwezo wa ama kuifuta sheria hiyo moja kwa moja toka kwenye vitabu vya sheria kwa kutamka kuwa "this law is unconstitutional and it should be struck out of statute book,and we hereby so do" au ikasema ikasema kwamba sheria hii ni unconstitutional na kutoa mwanya kwa serikali kuirekebisha.

Na kwa upande wa rufaa,kwa mujibu wa sheria rufaa au kusudio la kukata rufaa halizuii utekelezaji wa hukumu unless kama muomba au kata rufaa ameomba kusitisha utekelezaji wa hukumu yaani "stay of execution" hivyo iwapo serikali imekata rufaa bila kuomba stay bado utekelezaji wa kilichoshinda unaweza kuendelea tu.

Hiyo ni kwa mujibu wa civil procedure Act na The Appellate jurisdiction Act.
 
Kuna hukumu vilevile ya Jaji Mwalusanya kuwa hukumu ya kifo siyo halali.

Hukumu hii haijatekelezwa hadi leo.
Hukumu hiyo ilishatanguliwa na mahakamani ya rufani, ndio maana haijatekelezwa kwa maana hiyo death penalty is still a good law.Nadhani ulikuwa unarejea kesi ya Mbushuu Dominic Mnyaroje vs. R
 
Hapo maana yake mahakama ina discretion,yaani inao uwezo wa ama kuifuta sheria hiyo moja kwa moja toka kwenye vitabu vya sheria kwa kutamka kuwa "this law is unconstitutional and it should be struck out of statute book,and we hereby so do" au ikasema ikasema kwamba sheria hii ni unconstitutional na kutoa mwanya kwa serikali kuirekebisha.


Augustinoons, thanks.
"au ikasema ikasema kwamba sheria hii ni unconstitutional na kutoa mwanya kwa serikali kuirekebisha". Hii (kutoa mwanya) itawakilishwa vipi huko serikalini? Je, ni kwa kuishauri serikali irekebishe sheria hiyo ama kwa KUIAMURU serikali ibadili sheria hiyo, ama kwa kukaa kimya na its up to serikali kugundua hilo na kubadili hiyo sheria (endapo itatakiwa kubadilishwa)?


"Na kwa upande wa rufaa,kwa mujibu wa sheria rufaa au kusudio la kukata rufaa halizuii utekelezaji wa hukumu unless kama muomba au kata rufaa ameomba kusitisha utekelezaji wa hukumu yaani "stay of execution" hivyo iwapo serikali imekata rufaa bila kuomba stay bado utekelezaji wa kilichoshinda unaweza kuendelea tu"

Hapo pia nimepotea. Sidhani kama kitu imekatiwa rufaa then tuseme imeshinda na utekelezaji wake uendelee. Mind you hii ni kesi ya madai na siyo jinai. Kwa kesi ya Mtikila ambayo ndio tunaiongelea sasa, serikali imekata rufaa, then wewe unadai Madai ya Mtikila yapitishwa/ameshinda vile serikali haija sitisha, so whats the meaning of appeal? Na endapo serikali ikipitisha madai ya Mtikila kama ilivyoamriwa na High Court, Vipi Mahakama ya Rufaa ikija kupitisha madai ya Serikali na kuquash madai ya Mtikila? Je, tutavunja hii sheria iliyopendekezwa katika madai ya Mtikila na kurudia ile ya Mwanzo (iliyoonekana incorect High Court, na kuonekana correct Appeal court), ama itabidi iundwe sheria mpya kabisa, au ndio zote zivunjwe na kusiwepo na sheria ya namna hiyo au itakuwa vipi? Katika hili, naomba unijibu katika sheria za kesi za madai na siyo jinai.

Thanks,
Lizy
 
Lizy... hapa itakuwa kazi kidogo.. itabidi ufanye sehemu ya homework hii wewe mwenyewe. Kwa kifupi ni kuwa kulifanyika mabadiliko ya Katiba ambayo yaliingiza kipengele kinachotaka wagombea wa nafasi za uongozi kuwa wanatoka vyama vya kisiasa. Kabla ya hapo mgombea hakulazimishwa kuwa mwanachama wa chama cha kisiasa. Vipengele hivyo vya Katiba unaweza kuvisoma kwenye Katiba nenda http://www.tanzania.go.tz na utaiona Katiba na uvifuatilie.

Mabadiliko hayo ya vipengele vya Katiba yakapingana na kile kinachoitwa Haki za Msingi (Bill of Rights) ambapo mtu anayo haki ya kuchagua na kuchaguliwa akitimiza masharti fulani. Itafute hukumu nzima (google Mtikila Vs. Attorney General, Private Candidate"..

Thanks Mwkjj,

Ref: old articles hapa chini;

Article 21(1) provides:"Kila raia wa Jamhuri wa Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja, au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wanacnhi kwa hiari yao kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria"

Je, huyo mgombea binafsi alizingatia huo utaratibu uliowekwa na sheria? Anyway, sidhani kama kilikuwa ni kifungu kizuri kwa mgombea kukitumia katika claims zake kwani kinambana sana. Why, sababu tayari hizo taratibu zimesemwa mwanzo mbazo hazina favor kwake kutumia kifungu hiki.


Article 39 of the Constitution read:"Mtu hatastahili kuchaguliwa kushiriki kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kama:
(a) ametimiza umri wa miaka arobaini na
(b) anazo sifa za kumwezesha kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge au Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi”.

Again, kipengele (b), i doubt.

Article 67(1) of the Constitution:"Bila ya kuathiri masharti yaliyomo katika ibara hii, mtu yeyote atakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge endapo:
(a)........................................(imefutika)

(b) ni mwanachama wa chama anayetimiza masharti yote ya uanachama yaliyoelezwa katika katiba ya chama ………”

And “Chama” is defined in Article 151 to mean:… Chama Cha Mapinduzi kilichotajwa katika ibara ya 3(3) nay a (10) ya Katiba hii”.

The dominance of Chama Cha Mapundizi was abolished by an amendment to Article 10, introduced by Act No. 4 of 1992, with the advent of multiparty politics in Tanzania while Articles 20 and 21 remained intact.

Section 13 of Act No. 4 of 1992 amended Article 39 but retained paragraph (c) of the qualifications for a presidential candidate.

“(c) ni mwanachama na mgombe aliyependekezwa na chama cha
siasa”.[/
COLOR]


The new Article 21(1) now reads (2005 edition):

“Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 39 ya 47 na ya 67 ya Katiba hii nay a sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na nanchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria".

Ninachoona mimi, kilichofanyika hapa ni kuunganisha Article tatu kuwa moja (sijui ni kwa nini walifanya hivyo), lakini ujumbe ni ule ule.

Anyway, sina uzoefu sana.

Thanks.
 
Jamani, rufaa inapokatwa uamuzi uliotolewa unatiiwa kwanza. Mtu akihukumiwa kufungwa miaka mitano jela, anaenda kwanza lupango wakati kesi yake ya rufaa inasikilizwa. Hatusemi ati kwa vile anakata rufaa basi atoke nje asianze kutumikia kifungo cha awali.

Katika hili, seriikali ilitakiwa kwanza kutii uamuzi wa mahakama wakati inaendelea kukata rufaa, siyo kwamba haitii halafu inakata rufaa, sasa inakata rufaa ya nini wakati status quo is still maintaiened? Wangekata rufaa kama wangekuwa wametii uamuzi wa awali kwanza.

Hii reasoning mnayotumia si ingetumiwa na mamia ya watu ambao tayari wameanza kutumikia kifungo huku wakisubiri rufaa zao? Mfano mzuri ni Aden Rage alipohukumiwa kufungwa si alianza kutumikia kifungo hadi mahakama ya juu ilipotengua hukumu yake?
 
Jamani, rufaa inapokatwa uamuzi uliotolewa unatiiwa kwanza. Mtu akihukumiwa kufungwa miaka mitano jela, anaenda kwanza lupango wakati kesi yake ya rufaa inasikilizwa. Hatusemi ati kwa vile anakata rufaa basi atoke nje asianze kutumikia kifungo cha awali.

Katika hili, seriikali ilitakiwa kwanza kutii uamuzi wa mahakama wakati inaendelea kukata rufaa, siyo kwamba haitii halafu inakata rufaa, sasa inakata rufaa ya nini wakati status quo is still maintaiened? Wangekata rufaa kama wangekuwa wametii uamuzi wa awali kwanza.

Hii reasoning mnayotumia si ingetumiwa na mamia ya watu ambao tayari wameanza kutumikia kifungo huku wakisubiri rufaa zao? Mfano mzuri ni Aden Rage alipohukumiwa kufungwa si alianza kutumikia kifungo hadi mahakama ya juu ilipotengua hukumu yake?
Nafurahia reasoning yako M'kijiji. Lakini brother, tutambue tofauti kati ya kesi za jinai na kesi za madai. Utekelezaji wa maamuzi katika kesi hizo vilevile hutofautiana. Hukumu ya kesi ya jinai huanza kutekelezwa mara moja kwa kumwadhibu mkosaji na mkosaji ana haki mbili: kukata rufaa au kuomba bail pending appeal.Kwa upande wa kesi za madai, hukumu ikitolewa, utekelezaji unaanza vilevile mara moja ila aliyeshindwa naye ana haki ya: kukata rufaa na kuiomba mahakama kusitisha utekelezaji hadi rufaa itakaposikilizwa (stay of execution). Ahsante, Lazaros
 
Lazaro, unasahau kitu kimoja, hii sii kesi ya madai au ya jinai (not a civil or criminal case) ni kesi ya Kikatiba. Tukirudi hata kwenye kesi ya madai, mahakama inaposema fulani amlipe x kwa kumchafulia jina, yule x halazimiki kuanza kulipa mara moja kama anampango wa kukata rufaa na polisi hawawezi kwenda kukamata mali yake kutekeleza hiyo hukumu. Lakini katika muda uliopo mawakili wake n.k watatoa notice kwa mahakama kuwa wana nia ya kukata rufaa na hivyo hiyo hukumu isitekelezwe pending the appeal process.

Turudi kwenye kesi ya Kikatiba. Ikitokea kesi ambayo hukumu yake inasema "hukumu ya kifo ni kinyume na Katiba kwa sababu inapingana na kipengele kinachosema Kila mtu ana haki ya kulindwa maisha yake n.k" halafu kesho yake kuna hukumu ya mtu kunyongwa je mtu yule anyongwe wakati mahakama inasema sheria inayohalalisha hukumu ya kifo ni kinyume cha Katiba? Tukiangalia ibara ya 30:5 jibu ni ndiyo, kwa sababu ingawa mahakama imesema sheria hiyo ni kinyume na Katiba, sheria hiyo bado ina nguvu na inapaswa kufuatwa.

Tatizo lake ni kuwa hukumu ya Kikatiba haina ulazima wa injunction ya kuizuia serikali nk kutii amri ya mahakama (hata kama ni mahakama ya chini) pending appeal. Kwenye kesi ya kifo, je tukiamua kumuua huyu mtu baada ya hukumu kutolewa na kabla ya rufaa kumalizwa, itakapokuja mwishoni (kwenye mahakama ya rufaa) ikakubaliana na mahakama ya chini kuwa kweli sheria ile ni kinyume na Katiba.. tutawezaje kuhalalisha kitendo hicho cha sisi kama jamii kumuua mtu wakati tumeambiwa na mahakama kuwa ni kinyume na Katiba tangu kabla hatujamuua?
 
...Turudi kwenye kesi ya Kikatiba. Ikitokea kesi ambayo hukumu yake inasema "hukumu ya kifo ni kinyume na Katiba kwa sababu inapingana na kipengele kinachosema Kila mtu ana haki ya kulindwa maisha yake n.k" halafu kesho yake kuna hukumu ya mtu kunyongwa je mtu yule anyongwe wakati mahakama inasema sheria inayohalalisha hukumu ya kifo ni kinyume cha Katiba? Tukiangalia ibara ya 30:5 jibu ni ndiyo, kwa sababu ingawa mahakama imesema sheria hiyo ni kinyume na Katiba, sheria hiyo bado ina nguvu na inapaswa kufuatwa.

Tatizo lake ni kuwa hukumu ya Kikatiba haina ulazima wa injunction ya kuizuia serikali nk kutii amri ya mahakama (hata kama ni mahakama ya chini) pending appeal. Kwenye kesi ya kifo, je tukiamua kumuua huyu mtu baada ya hukumu kutolewa na kabla ya rufaa kumalizwa, itakapokuja mwishoni (kwenye mahakama ya rufaa) ikakubaliana na mahakama ya chini kuwa kweli sheria ile ni kinyume na Katiba.. tutawezaje kuhalalisha kitendo hicho cha sisi kama jamii kumuua mtu wakati tumeambiwa na mahakama kuwa ni kinyume na Katiba tangu kabla hatujamuua?

Injuction ipo.

Ibara ya 30 (5) inaipata Mahakama Kuu nguvu ya kupitia uhalali wa Sheria, Judicial Review, japo haisemi wazi wazi, kama sio lolote, kuhusu nguvu za Mahakama kutoa uamuzi wa papo kwa papo wa ku guarantee haki za Kikatiba. Uko sawa hapo

Lakini Katiba ikisimama peke yake sio msumeno, sio self-executing. Ndio maana husikii mtu kaenda jela kwa kuvunja Katiba, ila sheria zilizopo kwa mujibu wa Katiba. Kwa kuwa Katiba ikisimama yenyewe huwa sio msumeno na haina meno, yani sio self-executing, huwa zinaandikwa sheria za kutekeleza matakwa ya Katiba, Implementing Legislation au Proclamation Statutes, kama baadhi ya wataalam wa Tanzania wanavyoziita.

Implementing Legislation ya Ibara ya 30 (5) ya Katiba inaipa Mahakama Kuu uwezo wa kutoa agizo la ku guarangee haki. Wewe umeliita hilo agizo injuction.

BASIC RIGHTS AND DUTIES ENFORCEMENT ACT, 1994-33, Section 13 (3)

Power of High Court in Decisions


The power of the High Court under this Act shall include the power to make all such orders as shall be necessary and appropriate to secure the enjoyment by the applicant of the basic rights, freedoms and duties under the provisions of sections 12 to 19 of the Constitution should the court come to the conclusion that such basic rights freedoms or duties have been unlawfully denied or violated or that grounds exist for their protection by an order.
 
Kuhani.. ibara ya 30:5 ndivyo ambavyo ingesomeka isipokuwa pale inaposema kuwa mahakama ikiamuru kitu hicho kitu hakitakuwa hadi Bunge libadili sheria hiyo au muda upite. Kimsingi kama Mahakama inasema haki fulani imevunjwa (haki ya kuchaguliwa) tulitarajia kuwa amri hiyo ya mahakama iwe na nguvu. Lakini kutokana na kipengele hicho cha katiba hilo halitokei. Na hapo ndio tunauliza nani anaweza kuilazimisha serikali kutii amri ya mahakama kama Katiba yenyewe haisemi serikali inapaswa kutii amri ya mahakama wakati inapanga rufaa?
 
Wakati unasubiri rufaa ya kesi ya Kikatiba maana yale Kesi haijaisha.

Kama Lizy alivyoelezea, Mahakama Kuu inaweza kuwa imekosea. Hawawezi kuanza kuchapisha Vitabu vipya vya Katiba wakati kesi iko katikati ya Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa!

Mimi tatizo langu sio sana kile kipindi cha giza between the rufaa's and the courts. Tatizo langu ni kile kipindi cha giza wakati tunasubiri Serikali ibadilishe Sheria ambayo Mahakama imeona ni batili lakini imeambiwa na Katiba isithubutu kutamka ni batili.

Kile kipindi pale ndio tatizo langu. Not so much the time between the appeals. Kwa sababu pale kesi haijaisha.

Unanielewa ?
 
Wakati unasubiri rufaa ya kesi ya Kikatiba maana yale Kesi haijaisha.

Kama Lizy alivyoelezea, Mahakama Kuu inaweza kuwa imekosea. Hawawezi kuanza kuchapisha Vitabu vipya vya Katiba wakati kesi iko katikati ya Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa!

Mimi tatizo langu sio sana kile kipindi cha giza between the rufaa's and the courts. Tatizo langu ni kile kipindi cha giza wakati tunasubiri Serikali ibadilishe Sheria ambayo Mahakama imeona ni batili lakini imeambiwa na Katiba isithubutu kutamka ni batili.

Kile kipindi pale ndio tatizo langu. Not so much the time between the appeals. Kwa sababu pale kesi haijaisha.

Unanielewa ?

Kuhani nadhani tuko upande mmoja. Mimi tatizo langu ni hilo je Mahakama inapotangaza kipengele au sheria fulani ni kinyume na Katiba na serikali inapanga kukata rufaa, je sheria au kipengele hicho kiendelee kutumika? Jibu la kipengele cha 30:5 ni kuwa ndiyo sheriia au kipengele hicho bado kina nguvu na hatuna budi kukitii.
 
Mimi tatizo langu ni hilo je Mahakama inapotangaza kipengele au sheria fulani ni kinyume na Katiba na serikali inapanga kukata rufaa, je sheria au kipengele hicho kiendelee kutumika? Jibu la kipengele cha 30:5 ni kuwa ndiyo sheriia au kipengele hicho bado kina nguvu na hatuna budi kukitii.

Hakiendelei kutumiaka. Ndio kile kitu kinaitwa stay of execution.

BASIC RIGHTS AND DUTIES ENFORCEMENT ACT, 1994-33, Section 14 (3)

Appeals


Notwithstanding the provisions of the Civil Procedure Code or of any other law to the contrary, where in proceedings under this Act which do not involve continuos breach or personal injuries, the Government files a notice of intention to appeal against any decision of a court the notice shall, when entered, operate as a stay of execution upon the decisions sought to be appealed against.


Sasa hiyo ni kuhusu rufaa. Ambayo mimi sioni tatizo kwa sababu katika ya rufaa na counter-rufaa kesi haijaisha. Yani ule uamuzi wa Mahakama ya Chini sio final. Achana na rufaa. Ukianza kuingiza suala la rufaa hapa unadhoofisha argument na ku obscure uzito wa concern yetu. Kwa sababu kesi bado haijaisha, ndio maana huwezi kusema definitively kwamba sheria ni batili.

Turudi kwenye Ibara ya 30 (5), situation ambapo hakuna rufaa ila tunasubiri Serikali ifute Sheria batili.

Hapo ndio kuna swali. Inakuwaje, kwa mujibu wa ibara ya 30 (5), wakati tunasubiri sheria batili ibadilishwe -uamuzi ambao haujapingwa kwa rufaa - na Serikali inajishaua kubadilisha sheria, kwa nini sheria batili inakuwa bado iko in force?
 
Hakiendelei kutumiaka. Ndio kile kitu kinaitwa stay of execution.

BASIC RIGHTS AND DUTIES ENFORCEMENT ACT, 1994-33, Section 14 (3)

Appeals


Notwithstanding the provisions of the Civil Procedure Code or of any other law to the contrary, where in proceedings under this Act which do not involve continuos breach or personal injuries, the Government files a notice of intention to appeal against any decision of a court the notice shall, when entered, operate as a stay of execution upon the decisions sought to be appealed against.


Sasa hiyo ni kuhusu rufaa. Ambayo mimi sioni tatizo kwa sababu katika ya rufaa na counter-rufaa kesi haijaisha. Yani ule uamuzi wa Mahakama ya Chini sio final. Achana na rufaa. Ukianza kuingiza suala la rufaa hapa unadhoofisha argument na ku obscure uzito wa concern yetu. Kwa sababu kesi bado haijaisha, ndio maana huwezi kusema definitively kwamba sheria ni batili.

Turudi kwenye Ibara ya 30 (5), situation ambapo hakuna rufaa ila tunasubiri Serikali ifute Sheria batili.

Hapo ndio kuna swali. Inakuwaje, kwa mujibu wa ibara ya 30 (5), wakati tunasubiri sheria batili ibadilishwe -uamuzi ambao haujapingwa kwa rufaa - na Serikali inajishaua kubadilisha sheria, kwa nini sheria batili inakuwa bado iko in force?

My friend that is what is called a million dollar question. Kwa sababu sasa hivi ukitokea uchaguzi (kama ulivyotokea wa Tunduru (kabla ya rufaa kukatwa) na ule wa Kiteto, katika sehemu zote mbili Tume ya Uchaguzi haijaruhusu wagombea huru kwa sababu wanasema Bunge bado halijatii amri ya mahakama na hivyo sheria inayotaka wagombea kuwa wanachama wa chama cha kisiasa bado kutumika licha ya sheria hiyo kuamuriwa mara mbili sasa kuwa ni kinyume na Katiba, na serikali haijakata rufaa na rufaa haijamalizwa.

Kimsingi binafsi naamini kama ilivyo katika mambo mengine, wagombea huru wangeruhusiwa wakati serikali inajisua sua kukata rufaa. Kama serikali itashinda rufaa basi waliochaguliwa wanapoteza nafasi zao na kama chaguzi mpya zitafanyika. Lakini tunaweza vipi kuitii sheria ambayo mahakama imesema ni sheria kinyume na Katiba?
 
Back
Top Bottom