IBILIS Hufungwa Mwezi huu | Kwaninii Watu Hufanya Dhambi Wakati IBILIS Kafungiwa?

IBILIS Hufungwa Mwezi huu | Kwaninii Watu Hufanya Dhambi Wakati IBILIS Kafungiwa?

AL-USTADH

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2015
Posts
406
Reaction score
226
Amani iwe nanyi.

Ama baada ya salaam ningependa kuzungumzia mada tajwa hapo juu kama inavyosomeka kuwa ni kwa nini watu hufanya maasi (DHAMBI) wakati anayefanya watu watende dhambi huwa amefungwa kwa muda huu wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani...?.

IBILIS ni BABA WA MAASI yote unayoyaona yanatokea leo hii duniani, na ushahidi juu ya hili ni pale alipoweza kuwashawishi BABA YETU (ADAM) na MKEWE wakajikuta wakitenda dhambi bila ya wenyewe kujijua na hapo ndipo ilipotokea dhambi ya pili ; dhambi ya kwanza ilitokea pale IBILIS alipomuasi MUNGU WETU na akalaaniwa na akafukuzwa mbinguni na kuahidi atawasimamia WANA WA ADAM kila upande kuhakikisha anaingia nao MOTONI na baada ya hapo ndipo ikafata dhambi ya pili ya kuwashawishi ADAM NA MKEWE kutenda dhambi bila ya kujijua na kusababisha nao pia kufukuzwa mbinguni na kuja duniani ambapo iliandikwa kuwa mwanaume atakula kwa JASHO na mwanamke atazaa kwa UCHUNGU na kujikuta wakiwa MAADUI wenyewe kwa wenyewe kutokana na dhambi zao walizozitenda.

Kizazi baada ya kizazi ikawa vinatenda dhambi juu ya dhambi isipokuwa wale ambao wamesimama upande wa MUNGU, hao pekee ndio hukaa kwenye MSTARI japokuwa nao pia hujikuta wakiteleza na kuanguka kwenye MATOPE ila hunyanyuka haraka na kujisafisha tofauti na wengine ambao huanguka kwenye MATOPE na kuendelea kukaa hapo hapo huku wakiendelea kuyachezea MATOPE pasina kujali.

IBILIS NA SHETANI.

Kama nilivyokwisha sema kuwa IBILIS NI BABA WA MAASI ambaye alikuwa mwenyewe hapo mwanzo lakini baada ya hapo akapata wafuasi, akaendelea kupata kundi na jeshi la kutosha la kufanya kazi moja tu ambayo wala hakuificha aliiweka wazi kabisa kuwa ni kuwakusanya WENZA wa kuingia nao kwenye MOTO WA MILELE na kazi hii hufanywa na MASHEITWAAN wa KIBINADAM na MAJINI ikiwa lengo lao ni hili ; moja tu la kuingia nao MOTONI.

Mashetani wapo wa aina mbili wapo katika MAJINI NA WATU, nikimaanisha kuwa majini na watu wote wameumbwa kwa lengo la kumuabudu MUUMBA WETU sasa wote hawa (MAJINI NA WATU) wanapoasi na kuacha LENGO KUU ambalo ni kumuabudu MUNGU na kufanya mambo ya kumchukiza MUNGU KUPINDUKIA ndipo huingia kwenye sifa hii ya USHEITWAAN ambapo kazi yao KUU inakuwa ni KUMUASI MUNGU na kushawishi wengine pia kufanya MAASI na kumuasi MUNGU.

IBILIS ni kama RAIS ambaye ana jeshi lake sasa RAIS anaposafiri si kwamba eti na jeshi lake linaondoka HAPANA jeshi linabaki na kazi huwa zinaendelea kama kawaida na ndio maana unaweza kuona japo IBILIS amefungwa ndani ya MWEZI MTUKUFU lakini unaweza kujiuliza, kama IBILIS amefungwa mbona bado watu wanatenda dhambi ?, jeshi limebaki katika MAJINI NA WATU, hivyo kama ni mmoja kati ya wenye kufanya MAASI KUPINDUKIA basi juwa kuwa nawe ni mmoja kati ya WANAJESHI na WAFUASI WA IBILIS ambapo japo KIONGOZI hayupo lakini kazi za mikono yake zinaendelea kufanywa kama kawaida.

NAFSI YA MTU NA USHETANI.

Kila nafsi ndani yake imeumbiwa SHETANI ambaye humuamrisha kufanya MAASI na ndio maana mtu anapofanya MAASI utasikia akiambiwa "ISHINDE NAFSI YAKO BWANA" nadhani mmeshasikia hii kauli, na hii ni kwa sababu nafsi yoyote ile imeumbiwa SHETANI ndani yake kwa hiyo tunatakiwa kwanza kupambana na nafsi kwa sababu NAFSI ni kama MTOTO MCHANGA ukiiachia nayo inaendelea tu kutenda MAOVU siku zote ila ukiikataza nayo huacha ni kama MTOTO MCHANGA ukimuachia aendelee KUNYONYA bila ya kumkataza/kumuachisha basi ataendelea KUNYONYA hata awe na umri gani nafsi nayo ni hivyo hivyo kwa sababu nafsi imeumbiwa SHETANI ndani yake.

Sasa hata IBILIS anapofungwa, hapa mtu huwa anashindwa na nafsi yake na kushindwa kuikataza na kuizuia katika kufanya MAASI sasa ukiona upo kwenye hali hii au kundi hili basi juwa wazi kuwa nawe ni mmoja kati ya waliopo chini ya UTAWALA wa IBILIS japo RAIS hayupo lakini kazi za mikono yake huendelea kufanyika pasina kipingamizi na wala sio kazi za mikono yake huendelea kufanyika pasina kipingamizi na wala sio kipindi cha kumsingizia IBILIS eti ndio anakushawishi LA HASHA hapa ni wewe na nafsi yako na wala sio IBILIS kwa sababu ndani ya MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAAN IBILIS hufungwa MINYORORO na MALAAIKA WA MUNGU na ndio maana unapoisha mwezi huu basi IBILIS huwa anaachiliwa na huwa anarudi kwa HASIRA mno na ndio maana utaona watu wakitenda MAASI/MAOVU kwa kasi mno tofauti na alivyokuwa amefungwa hapo kabla.

Ukiona upo kwenye MAASI ndani ya MWEZI HUU basi juwa wazi kuwa MOYO WAKO umeota KUTU na umezidiwa na IBILIS kwa kupigwa MUHURI NA IBILIS na ndio maana unaona MKUU hayupo lakini MTUMISHI unatumikia kama kawaida na kuendelea kufanya kazi za MKUU hata kama yeye hayupo............kwa mfano wa haraka haraka chukulia tu kama vile unaendesha BAISKELI kisha ukanyonga itategemea ulikuwa unanyonga kwa kiasi gani, utaweza kuona hata kama utaacha kunyonga pedeli lakini BAISKELI utakuta inaendelea tu kutembea katika spidi ambayo ulikuwa unainyongea itategemea ulikuwa ukinyonga kwa spidi kiasi gani BAISKELI hiyo.Hii ni sawa na mfano wa IBILIS kuwa, hata kama AMEFUNGWA inategemea ulikuwa ni MFUASI WAKE kwa kiasi gani na ndio maana unakuta hata kama YEYE HAYUPO lakini MTUMISHI unaendelea kutumikia kwa kutenda MAASI/MADHAMBI kama kawaida pasina kujali uwepo wa MKUU AU LAA.

Hivyo, kwa kuweza kujua tatizo ni KWA NINI WATU HUTENDA MADHAMBI WAKATI MSHAWISHI KAFUNGWA tunaweza kujua kuwa kumbe ni NAFSI ZETU wenyewe na wala sio sababu ni IBILIS, hivyo kaa chini utafakari na ujaribu kuizuia nafsi yako kama unavyomzuia MTOTO MCHANGA KUNYONYA, kama utamuachia aendelee KUNYONYA basi ataendelea tu pasina kuacha mpaka pale utakapo muachisha mwenyewe au aidha kama utaizuia na kuweza kupambana na kuishinda nafsi yako basi MUNGU nae atakuonyesha NJIA kwa sababu alishasema MUNGU kuwa, anamuongoza MTU kule MTU anapotaka mwenyewe kwenda kama ukitaka kwenda KULIA basi MUNGU atakufanyia wepesi na atakuongoza katika NJIA HIYO unayotaka kwenda, na pia ukitaka kwenda KUSHOTO pia atakufanyia wepesi na atakuongoza pia katika NJIA HIYO unayotaka kwenda.

Nawatakia kila la heri.
 
Amani iwe nanyi.

Ama baada ya salaam ningependa kuzungumzia mada tajwa hapo juu kama inavyosomeka kuwa ni kwa nini watu hufanya maasi (DHAMBI) wakati anayefanya watu watende dhambi huwa amefungwa kwa muda huu wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani...?.

IBILIS ni BABA WA MAASI yote unayoyaona yanatokea leo hii duniani, na ushahidi juu ya hili ni pale alipoweza kuwashawishi BABA YETU (ADAM) na MKEWE wakajikuta wakitenda dhambi bila ya wenyewe kujijua na hapo ndipo ilipotokea dhambi ya pili ; dhambi ya kwanza ilitokea pale IBILIS alipomuasi MUNGU WETU na akalaaniwa na akafukuzwa mbinguni na kuahidi atawasimamia WANA WA ADAM kila upande kuhakikisha anaingia nao MOTONI na baada ya hapo ndipo ikafata dhambi ya pili ya kuwashawishi ADAM NA MKEWE kutenda dhambi bila ya kujijua na kusababisha nao pia kufukuzwa mbinguni na kuja duniani ambapo iliandikwa kuwa mwanaume atakula kwa JASHO na mwanamke atazaa kwa UCHUNGU na kujikuta wakiwa MAADUI wenyewe kwa wenyewe kutokana na dhambi zao walizozitenda.

Kizazi baada ya kizazi ikawa vinatenda dhambi juu ya dhambi isipokuwa wale ambao wamesimama upande wa MUNGU, hao pekee ndio hukaa kwenye MSTARI japokuwa nao pia hujikuta wakiteleza na kuanguka kwenye MATOPE ila hunyanyuka haraka na kujisafisha tofauti na wengine ambao huanguka kwenye MATOPE na kuendelea kukaa hapo hapo huku wakiendelea kuyachezea MATOPE pasina kujali.

IBILIS NA SHETANI.

Kama nilivyokwisha sema kuwa IBILIS NI BABA WA MAASI ambaye alikuwa mwenyewe hapo mwanzo lakini baada ya hapo akapata wafuasi, akaendelea kupata kundi na jeshi la kutosha la kufanya kazi moja tu ambayo wala hakuificha aliiweka wazi kabisa kuwa ni kuwakusanya WENZA wa kuingia nao kwenye MOTO WA MILELE na kazi hii hufanywa na MASHEITWAAN wa KIBINADAM na MAJINI ikiwa lengo lao ni hili ; moja tu la kuingia nao MOTONI.

Mashetani wapo wa aina mbili wapo katika MAJINI NA WATU, nikimaanisha kuwa majini na watu wote wameumbwa kwa lengo la kumuabudu MUUMBA WETU sasa wote hawa (MAJINI NA WATU) wanapoasi na kuacha LENGO KUU ambalo ni kumuabudu MUNGU na kufanya mambo ya kumchukiza MUNGU KUPINDUKIA ndipo huingia kwenye sifa hii ya USHEITWAAN ambapo kazi yao KUU inakuwa ni KUMUASI MUNGU na kushawishi wengine pia kufanya MAASI na kumuasi MUNGU.

IBILIS ni kama RAIS ambaye ana jeshi lake sasa RAIS anaposafiri si kwamba eti na jeshi lake linaondoka HAPANA jeshi linabaki na kazi huwa zinaendelea kama kawaida na ndio maana unaweza kuona japo IBILIS amefungwa ndani ya MWEZI MTUKUFU lakini unaweza kujiuliza, kama IBILIS amefungwa mbona bado watu wanatenda dhambi ?, jeshi limebaki katika MAJINI NA WATU, hivyo kama ni mmoja kati ya wenye kufanya MAASI KUPINDUKIA basi juwa kuwa nawe ni mmoja kati ya WANAJESHI na WAFUASI WA IBILIS ambapo japo KIONGOZI hayupo lakini kazi za mikono yake zinaendelea kufanywa kama kawaida.

NAFSI YA MTU NA USHETANI.

Kila nafsi ndani yake imeumbiwa SHETANI ambaye humuamrisha kufanya MAASI na ndio maana mtu anapofanya MAASI utasikia akiambiwa "ISHINDE NAFSI YAKO BWANA" nadhani mmeshasikia hii kauli, na hii ni kwa sababu nafsi yoyote ile imeumbiwa SHETANI ndani yake kwa hiyo tunatakiwa kwanza kupambana na nafsi kwa sababu NAFSI ni kama MTOTO MCHANGA ukiiachia nayo inaendelea tu kutenda MAOVU siku zote ila ukiikataza nayo huacha ni kama MTOTO MCHANGA ukimuachia aendelee KUNYONYA bila ya kumkataza/kumuachisha basi ataendelea KUNYONYA hata awe na umri gani nafsi nayo ni hivyo hivyo kwa sababu nafsi imeumbiwa SHETANI ndani yake.

Sasa hata IBILIS anapofungwa, hapa mtu huwa anashindwa na nafsi yake na kushindwa kuikataza na kuizuia katika kufanya MAASI sasa ukiona upo kwenye hali hii au kundi hili basi juwa wazi kuwa nawe ni mmoja kati ya waliopo chini ya UTAWALA wa IBILIS japo RAIS hayupo lakini kazi za mikono yake huendelea kufanyika pasina kipingamizi na wala sio kazi za mikono yake huendelea kufanyika pasina kipingamizi na wala sio kipindi cha kumsingizia IBILIS eti ndio anakushawishi LA HASHA hapa ni wewe na nafsi yako na wala sio IBILIS kwa sababu ndani ya MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAAN IBILIS hufungwa MINYORORO na MALAAIKA WA MUNGU na ndio maana unapoisha mwezi huu basi IBILIS huwa anaachiliwa na huwa anarudi kwa HASIRA mno na ndio maana utaona watu wakitenda MAASI/MAOVU kwa kasi mno tofauti na alivyokuwa amefungwa hapo kabla.

Ukiona upo kwenye MAASI ndani ya MWEZI HUU basi juwa wazi kuwa MOYO WAKO umeota KUTU na umezidiwa na IBILIS kwa kupigwa MUHURI NA IBILIS na ndio maana unaona MKUU hayupo lakini MTUMISHI unatumikia kama kawaida na kuendelea kufanya kazi za MKUU hata kama yeye hayupo............kwa mfano wa haraka haraka chukulia tu kama vile unaendesha BAISKELI kisha ukanyonga itategemea ulikuwa unanyonga kwa kiasi gani, utaweza kuona hata kama utaacha kunyonga pedeli lakini BAISKELI utakuta inaendelea tu kutembea katika spidi ambayo ulikuwa unainyongea itategemea ulikuwa ukinyonga kwa spidi kiasi gani BAISKELI hiyo.Hii ni sawa na mfano wa IBILIS kuwa, hata kama AMEFUNGWA inategemea ulikuwa ni MFUASI WAKE kwa kiasi gani na ndio maana unakuta hata kama YEYE HAYUPO lakini MTUMISHI unaendelea kutumikia kwa kutenda MAASI/MADHAMBI kama kawaida pasina kujali uwepo wa MKUU AU LAA.

Hivyo, kwa kuweza kujua tatizo ni KWA NINI WATU HUTENDA MADHAMBI WAKATI MSHAWISHI KAFUNGWA tunaweza kujua kuwa kumbe ni NAFSI ZETU wenyewe na wala sio sababu ni IBILIS, hivyo kaa chini utafakari na ujaribu kuizuia nafsi yako kama unavyomzuia MTOTO MCHANGA KUNYONYA, kama utamuachia aendelee KUNYONYA basi ataendelea tu pasina kuacha mpaka pale utakapo muachisha mwenyewe au aidha kama utaizuia na kuweza kupambana na kuishinda nafsi yako basi MUNGU nae atakuonyesha NJIA kwa sababu alishasema MUNGU kuwa, anamuongoza MTU kule MTU anapotaka mwenyewe kwenda kama ukitaka kwenda KULIA basi MUNGU atakufanyia wepesi na atakuongoza katika NJIA HIYO unayotaka kwenda, na pia ukitaka kwenda KUSHOTO pia atakufanyia wepesi na atakuongoza pia katika NJIA HIYO unayotaka kwenda. Hivyo ni wewe mwenyewe ndio wa kuchagua ni NJIA GANI unayotaka kwenda aidha ni KUSHOTO au KULIA MUNGU atakuongoza vyema huko unapotaka kuelekea.TUMUOMBE MUNGU ATUONGOZE KATIKA NJIA ILIYONYOKA SOTE IN SHAA ALLAH, AMEN.

NAWATAKIA KILA LA HERI.
 
jamaa fanya practical ndogo kabisa.... inua baiskeli matairi juu then zungusha peda sanaaaaaaa afu achia, then jiulize why tyre inazunguka wakati peda siizungushi.......????
 
jamaa fanya practical ndogo kabisa.... inua baiskeli matairi juu then zungusha peda sanaaaaaaa afu achia, then jiulize why tyre inazunguka wakati peda siizungushi.......????

Mkuu labda kama upeo wako wa kufkiri utakuwa umefika mwisho hapo sawa ila kama utafkiri kwa KINA basi jibu la swali lako tayari lipo hapo juu kiongozi, TATIZO UELEWA TU.

Na hata wee mwenyewe umeshajijibu yani ni jibu ambalo umeligeuza swali lenye jibu ndani yake labda kwa kukusaidia tu kutokana na jibu la swali lenye jibu lako ndani yake ni kwa sababu umeshasema kuwa ULIZUNGUSHA SANAAAAAA, sasa ukifkiri kwa KINA basi tayari jibu utakuwa nalo kiongozi.

KARIBU.
 
Maelezo yako yanataja kuwa IBLIS aliasi akafukuzwa mbinguni.ADAM na HAWA pia waliasi wakafukuzwa mbinguni.SWALI:Mbona Adam na Hawa walionekana na Iblis haonekani?

Jibu:Adam na Hawa waliumbwa waishi duniani.Hawakuwahi kuishi mbinguni.Walikuwa wanaishi ktk Bustani ya Edeni.Walipoasi walifukuzwa kutoka bustanin na Mungu akaweka Upanga wa MOTO na makerub mlango wa kuingilia bustan ili wasiingie tena.Wakaanza kuishi mashariki ya Bustani.Bustani ya edeni ilikuwa na mito ambayo ipo hapa duniani hadi leo. SOMA Mwanzo sura 2 na ya 3.
 
Jesus is mentioned many times than Muhammad in the Qur'an..

Its a fact, no offense intended..
 
Kote nimekuelewa ila umekuja kuniacha hoi na kuharibu uliposena majini pia waliumbwa wamuabudu Mungu na wakati majini yote nu jeshi lililoasi pamoja na ibilisi na kwahiyo wanasubiri hukumu yao,ila hiyo ya shetani kufungwa minyororo kila mwezi wa ramadhani ili watu wasitende dhambi ndio kwnza naiskia leo hii kwa maana shetani kwnn afungwe huo mwezi na miezi mingine aachiliwe inamaana kama Mungu wenu anawapenda wanadamu wake kwnn asimfunge siku zote?

Kwa sababu kama ndio mwezi wa watu kumrudia mola wao basi haina haja ya toba katika maisha ya wanadamu maana toba ni upendeleo tuliopewa na Mungu ili kumrudia ndio maana sisi kwa dini yetu maisha yetu hutakiwa kuishi kwa toba na kufunga mara kwa mara na kuomba ili kuushinda mwili maana mwili ndio hututia katika majaribu kwasababu ya tamaa zake ndio maana hatunaga mwezi maalumu wa toba kinachotakiwa ni kwmba tuwe wasafi siku zote katika maisha yetu kwa maana shetani yupo kazini siku zote na wala hana likizo kwa maana anajua muda wake wa kuangamia umekaribia sana sasa pasipo kuwaharibu watu lengo lake halitatimia, ikiwa yeye ndo mkuu wa madhambi yote na anajeshi lake ni kwann asiamrishe farasi wake wawe wanatulia kipindi hiki?

Maana katika hayo huwezi kumfunga mkuu wao ukaacha jeshi lake linaendelea kuteketeza watu maana kuendelea kwa dhambi kipindi hiki ni kwamba shetani bado yupo na anatenda kazi zake kama kawaida kwahyo msiseme malaika wa Mungu hushuka na kumfunga minyororo shetani huku dhambi zinaendelea inakuwa haileti mantiki, maana katika sisi tunajua kuwa shetani alikuwa ni mkuu wa malaika na alikuwa ni kiongozi wa sifa kwhyo alivyoasi akatupwa na jeshi lake la malaika waliomuasi Mungu na hao malaika ndio hayo majinni.

Kwahiyo ushauri wangu ni kwmba bwana Ostadhi kwa dini yenu sishangai lakini waambie tu waumini wako wajitahd kutenda mema maisha yao yote angalau wanaweza kupata rehma kwa mola wao. Na sisi dini yetu nishauri kwamba shetani yupo kazini siku zote hana weekend, saa wala likizo kwhiyo tujitahd kuomba toba ya kwl na kufunga mara kwa mara maana hatuna mwezi maalumu labda kwa wenzetu wa roman na anglicana lakini madhehebu mengne hasa ya kipentecoste hatunaga mwezi maalumu sisi hufunga kila roho mtakatifu anavyotusukuma kufanya hivyo kwa lengo maalumu mfano kuombea wengine,na mambo mengine.

Ndio maana kama jambo ni gumu huweza kufunga hata siku 3 kavu bila kula wala kunywa chochote ili kuusulubisha mwili na tamaa zake na roho kuwa na nguvu maana tunapoambiwa mbinguni hakitaingia chenye nguvu haimaanishi nguvu za mwili kwa maana mwili haufai kitu pasipo roho bali ni nguvu za roho yako kwa maana ukiushinda mwili na tamaa zake lazma roho yako iwe na nguvu za kuuongoza mwili lakini mwili ukiwa na nguvu kuliko roho kwako dhambi itakuwa ni ibada kwa maana tamaa na machukizo yote hutokana na mwili.

Japo naskia yapo madhehebu hufunga masaa sijui 6 au hufunga huku wanakunywa maji au wanakula tuu pasipo maji hio ni juu yao ila kwa mimi ninaamini kufunga kuzuri ni masaa 12 makavu, 24, 36 n.k kulingana na Roho mtakatifu atakavyokuwa anakutia nguvu na pasipo huyo roho huwezi kufunga hivyo kwa maana bado utakuwa na tamaa za mwili hvyo tunatakiwa toba ya kweli, kufunga, kuomba, matendo mema na roho mtakatifu tutaweza kumshinda huyo ibilisi na kuishi maisha matakatifu.
 
Maelezo yako yanataja kuwa IBLIS aliasi akafukuzwa mbinguni.ADAM na HAWA pia waliasi wakafukuzwa mbinguni.SWALI:Mbona Adam na Hawa walionekana na Iblis haonekani?

Mkuu labda unamaanisha walionekana na nani kiongozi ?, na pia ukae ukikumbuka kuwa IBILIS pamoja na ADAM wote ni viumbe lakini kuwa kwao viumbe si sawa kuwa wote wameumbwa kwa kitu kimoja HAPANA, tunapotazama suala la UUMBWAJI ni kwamba ADAM aliumbwa kwa UDONGO lakini IBILIS hakuumbwa kwa UDONGO IBILIS aliumbwa kwa MOTO na hii labda ndio sababu ya yeye kutokuonekana na pia inategemea hakuonekana na nani ni BINADAM TU ndio hawakuweza kumuona ila MALAIKA NA MUNGU wanamuona kama kawaida ila kwa macho ya KIBINADAM ndio huwezi kumuona labda pale atakapotaka mwenyewe umuone kwa minajili maalum.


Jibu:Adam na Hawa waliumbwa waishi duniani.Hawakuwahi kuishi mbinguni.

Mkuu una uhakika na unachokinena toka kinywani mwako kiongozi...?.


Walikuwa wanaishi ktk Bustani ya Edeni.Walipoasi walifukuzwa kutoka bustanin na Mungu akaweka Upanga wa MOTO na makerub mlango wa kuingilia bustan ili wasiingie tena.Wakaanza kuishi mashariki ya Bustani.Bustani ya edeni ilikuwa na mito ambayo ipo hapa duniani hadi leo. SOMA Mwanzo sura 2 na ya 3.

Haya yote ni mapokeo tu kiongozi hivyo siwezi kukupinga kwa vile ulivyopokea kwa upande wako ndugu.
 
Jesus is mentioned many times than Muhammad in the Qur'an..

Its a fact, no offense intended..


Yes, ni kweli kabisa NABII ISSA ametajwa mara nyingi ndani ya QUR'AN kuliko alivyotajwa NABII MUHAMMAD ametajwa mara 4 au 5 tu kwa jina ila NABII ISSA ametajwa zaidi ya mara 25 na pia MTAKATIFU MARYAM ametajwa si chini ya mara 32 kuliko alivyotajwa kwenye BIBLIA na pia QURAN imeshushwa kwa NABII MUHAMMAD hivyo hakukuwa na sababu ya kumtaja repeatedly, zaidi ni ametajwa kwa ishara YAA AYUHAA.
 
yesu alifunga kwa siku 40.


Ni kweli kabisa mkuu unenayo ila wale wanaomfata naona hawafanyi kabisa kama afanyavyo yeye sasa sijui wanamfata kwa kufanya mambo mengine na mengine wanabagua sidhani kama ndivyo mafundisho yanavyosema hivyo...?.
 
Amani iwe nanyi.

Ama baada ya salaam ningependa kuzungumzia mada tajwa hapo juu kama inavyosomeka kuwa ni kwa nini watu hufanya maasi (DHAMBI) wakati anayefanya watu watende dhambi huwa amefungwa kwa muda huu wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani...?.

IBILIS ni BABA WA MAASI yote unayoyaona yanatokea leo hii duniani, na ushahidi juu ya hili ni pale alipoweza kuwashawishi BABA YETU (ADAM) na MKEWE wakajikuta wakitenda dhambi bila ya wenyewe kujijua na hapo ndipo ilipotokea dhambi ya pili ; dhambi ya kwanza ilitokea pale IBILIS alipomuasi MUNGU WETU na akalaaniwa na akafukuzwa mbinguni na kuahidi atawasimamia WANA WA ADAM kila upande kuhakikisha anaingia nao MOTONI na baada ya hapo ndipo ikafata dhambi ya pili ya kuwashawishi ADAM NA MKEWE kutenda dhambi bila ya kujijua na kusababisha nao pia kufukuzwa mbinguni na kuja duniani ambapo iliandikwa kuwa mwanaume atakula kwa JASHO na mwanamke atazaa kwa UCHUNGU na kujikuta wakiwa MAADUI wenyewe kwa wenyewe kutokana na dhambi zao walizozitenda.

Kizazi baada ya kizazi ikawa vinatenda dhambi juu ya dhambi isipokuwa wale ambao wamesimama upande wa MUNGU, hao pekee ndio hukaa kwenye MSTARI japokuwa nao pia hujikuta wakiteleza na kuanguka kwenye MATOPE ila hunyanyuka haraka na kujisafisha tofauti na wengine ambao huanguka kwenye MATOPE na kuendelea kukaa hapo hapo huku wakiendelea kuyachezea MATOPE pasina kujali.

IBILIS NA SHETANI.

Kama nilivyokwisha sema kuwa IBILIS NI BABA WA MAASI ambaye alikuwa mwenyewe hapo mwanzo lakini baada ya hapo akapata wafuasi, akaendelea kupata kundi na jeshi la kutosha la kufanya kazi moja tu ambayo wala hakuificha aliiweka wazi kabisa kuwa ni kuwakusanya WENZA wa kuingia nao kwenye MOTO WA MILELE na kazi hii hufanywa na MASHEITWAAN wa KIBINADAM na MAJINI ikiwa lengo lao ni hili ; moja tu la kuingia nao MOTONI.

Mashetani wapo wa aina mbili wapo katika MAJINI NA WATU, nikimaanisha kuwa majini na watu wote wameumbwa kwa lengo la kumuabudu MUUMBA WETU sasa wote hawa (MAJINI NA WATU) wanapoasi na kuacha LENGO KUU ambalo ni kumuabudu MUNGU na kufanya mambo ya kumchukiza MUNGU KUPINDUKIA ndipo huingia kwenye sifa hii ya USHEITWAAN ambapo kazi yao KUU inakuwa ni KUMUASI MUNGU na kushawishi wengine pia kufanya MAASI na kumuasi MUNGU.

IBILIS ni kama RAIS ambaye ana jeshi lake sasa RAIS anaposafiri si kwamba eti na jeshi lake linaondoka HAPANA jeshi linabaki na kazi huwa zinaendelea kama kawaida na ndio maana unaweza kuona japo IBILIS amefungwa ndani ya MWEZI MTUKUFU lakini unaweza kujiuliza, kama IBILIS amefungwa mbona bado watu wanatenda dhambi ?, jeshi limebaki katika MAJINI NA WATU, hivyo kama ni mmoja kati ya wenye kufanya MAASI KUPINDUKIA basi juwa kuwa nawe ni mmoja kati ya WANAJESHI na WAFUASI WA IBILIS ambapo japo KIONGOZI hayupo lakini kazi za mikono yake zinaendelea kufanywa kama kawaida.

NAFSI YA MTU NA USHETANI.

Kila nafsi ndani yake imeumbiwa SHETANI ambaye humuamrisha kufanya MAASI na ndio maana mtu anapofanya MAASI utasikia akiambiwa "ISHINDE NAFSI YAKO BWANA" nadhani mmeshasikia hii kauli, na hii ni kwa sababu nafsi yoyote ile imeumbiwa SHETANI ndani yake kwa hiyo tunatakiwa kwanza kupambana na nafsi kwa sababu NAFSI ni kama MTOTO MCHANGA ukiiachia nayo inaendelea tu kutenda MAOVU siku zote ila ukiikataza nayo huacha ni kama MTOTO MCHANGA ukimuachia aendelee KUNYONYA bila ya kumkataza/kumuachisha basi ataendelea KUNYONYA hata awe na umri gani nafsi nayo ni hivyo hivyo kwa sababu nafsi imeumbiwa SHETANI ndani yake.

Sasa hata IBILIS anapofungwa, hapa mtu huwa anashindwa na nafsi yake na kushindwa kuikataza na kuizuia katika kufanya MAASI sasa ukiona upo kwenye hali hii au kundi hili basi juwa wazi kuwa nawe ni mmoja kati ya waliopo chini ya UTAWALA wa IBILIS japo RAIS hayupo lakini kazi za mikono yake huendelea kufanyika pasina kipingamizi na wala sio kazi za mikono yake huendelea kufanyika pasina kipingamizi na wala sio kipindi cha kumsingizia IBILIS eti ndio anakushawishi LA HASHA hapa ni wewe na nafsi yako na wala sio IBILIS kwa sababu ndani ya MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAAN IBILIS hufungwa MINYORORO na MALAAIKA WA MUNGU na ndio maana unapoisha mwezi huu basi IBILIS huwa anaachiliwa na huwa anarudi kwa HASIRA mno na ndio maana utaona watu wakitenda MAASI/MAOVU kwa kasi mno tofauti na alivyokuwa amefungwa hapo kabla.

Ukiona upo kwenye MAASI ndani ya MWEZI HUU basi juwa wazi kuwa MOYO WAKO umeota KUTU na umezidiwa na IBILIS kwa kupigwa MUHURI NA IBILIS na ndio maana unaona MKUU hayupo lakini MTUMISHI unatumikia kama kawaida na kuendelea kufanya kazi za MKUU hata kama yeye hayupo............kwa mfano wa haraka haraka chukulia tu kama vile unaendesha BAISKELI kisha ukanyonga itategemea ulikuwa unanyonga kwa kiasi gani, utaweza kuona hata kama utaacha kunyonga pedeli lakini BAISKELI utakuta inaendelea tu kutembea katika spidi ambayo ulikuwa unainyongea itategemea ulikuwa ukinyonga kwa spidi kiasi gani BAISKELI hiyo.Hii ni sawa na mfano wa IBILIS kuwa, hata kama AMEFUNGWA inategemea ulikuwa ni MFUASI WAKE kwa kiasi gani na ndio maana unakuta hata kama YEYE HAYUPO lakini MTUMISHI unaendelea kutumikia kwa kutenda MAASI/MADHAMBI kama kawaida pasina kujali uwepo wa MKUU AU LAA.

Hivyo, kwa kuweza kujua tatizo ni KWA NINI WATU HUTENDA MADHAMBI WAKATI MSHAWISHI KAFUNGWA tunaweza kujua kuwa kumbe ni NAFSI ZETU wenyewe na wala sio sababu ni IBILIS, hivyo kaa chini utafakari na ujaribu kuizuia nafsi yako kama unavyomzuia MTOTO MCHANGA KUNYONYA, kama utamuachia aendelee KUNYONYA basi ataendelea tu pasina kuacha mpaka pale utakapo muachisha mwenyewe au aidha kama utaizuia na kuweza kupambana na kuishinda nafsi yako basi MUNGU nae atakuonyesha NJIA kwa sababu alishasema MUNGU kuwa, anamuongoza MTU kule MTU anapotaka mwenyewe kwenda kama ukitaka kwenda KULIA basi MUNGU atakufanyia wepesi na atakuongoza katika NJIA HIYO unayotaka kwenda, na pia ukitaka kwenda KUSHOTO pia atakufanyia wepesi na atakuongoza pia katika NJIA HIYO unayotaka kwenda. Hivyo ni wewe mwenyewe ndio wa kuchagua ni NJIA GANI unayotaka kwenda aidha ni KUSHOTO au KULIA MUNGU atakuongoza vyema huko unapotaka kuelekea.TUMUOMBE MUNGU ATUONGOZE KATIKA NJIA ILIYONYOKA SOTE IN SHAA ALLAH, AMEN.

NAWATAKIA KILA LA HERI.

inategemea anayemfunga ibirisi ana guvu ya kumfunga??
 
Hakuna Ibilisi anayepotosha watu, bali watu wanapotoka kutokana na sumu kuu mbwalimbali. Watu wanapotoka kutokana na
  • Ujinga- Kushindwa kufahamu vitu kwa uhalisia vilivyo. Hii dunia tunayoishi ni dunia tofauti na unavyoiona. Kwa mtu mwenye akili duni anaweza kutumia akili yake kuhukumu hali au kiumbe au being yoyote nje yake. Mfano kusema shetani amenishawishi, hakuna anayekushawishi, bali kutokana na ujinga wako wa kushindwa kufahamu uhalisia wa jambo unajikuta unakosea kutenda yaliyosahihi. Mfano mtu anaiba, ni kutokana na ujinga kushindwa kujua chanzo cha kupata pesa kihalali, pia kutokana na uzembe wa kutenda majukumu na kufanikiwa, hakuna sauti kutoka kwa kiumbe wa nje yake iliyokuwa inaongea naye bali ni yeye alivyotumia akili yake vibaya na kufanya maamuzi mabaya.
  • Mazoea yasiyo sahihi. Mwanadamu ana asili hii ya kuwa akizoea jambo au hali anakuwa anaiona ni ya kawada. Mtu kazoea kutembea na wake za watu au na wanawake wengi basi anajikuta anaizoea ile tabia na kusema anashawishiwa na ibilisi wakati ni yeye mwenyewe ndiye aliyeweka uhalisia huo na kuuelewa.
  • Tamaa - Kila mwanadamu anapenda kuwa na furaha. Hakuna mwanadamu asiyependa kuwa na furaha. Lakini wanadamu wanatofautiana kuelewa maana ya furaha ni nini. Wengi hutafuta furaha nje yao na ndio maana wanakosea. Lengo la maisha ni kuwa na furaha, lakini tunapaswa kuitafuta furaha ya halali. Furaha isiyomuumiza mwanadamu, mnyama wala mazingira yanayotuzunguka. Kama mtu anaona ni raha kuzini, tatizo sio ibilisi alimshawishi bali kutokana na ujinga, mtu kutokujua chanzo cha furaha basi anajikuta anatafuta furaha kimakosa. Anatumia mwili na hisia zake kutafuta furaha, na kusahau kuwa huu mwili tunauacha hapa hapa duniani na raha zitokanazo na mwili huu hazidumu. Tamaa ni mbaya kama ni tamaa ambayo inaadhiri.
  • Pia kuna Hasira, Wivu, kushindwa kujitambua, kushindwa kufahamu akili na hisia zetu zilivyo n.k

Nadhani kwa upande wangu na uelewa wangu kuwa hamna Ibilisi bali sisi ndio Ibilisi na Malaika. Mwanadamu anaweza akawa ibilisi au malaika. Ni kutokana na kujitambua na kufahamu anatakiwa afanye nini na kwanini. Ibilisi ni fumbo na sio kama lijitu ambalo linakushawishi. Maisha yanataka tujifunze na tujitambue.

Hata kama huu ni mfungo wa Ramadhan, watu wapo ambao wanajichunga kipindi hiki na wanajitahidi kuacha yasiyostahili, lakini mwezi huu ukiisha bado wapo watakaoendelea na mazoea yao kwani hawafahamu chanzo cha mazoea mabaya yao nini bali wanalaumu Ibilisi ambaye hata hajawahi kuwaandikia mahali au kuongea nao kuwashawishi mabaya. Na pia bado maovu yapo mwezi huu kwani watu wapo walioshindwa kufahamu kwa udhani uhalisia upo wapi.


Kama hujui tiba na chanzo cha ugonjwa utaendelea kujitibu kwa dawa za matumaini lakini bado hujauondoa ugonjwa. Kuuondoa ugonjwa lazima ufahamu chanzo cha ugonjwa ambacho ndicho chanzo kikuu cha uhalisia na kujua ni jinsi gani ya kuikitibu.

Ramadhan Kareem, ni mchango wangu tu.

 
kwanini wamemfunga mwezi huu tu?
kama wamemfunga ina maana wanamfuga kwa hiyo wanaongoza maisha yako
eti watu wanatenda maasi baada ya mwezi mtukufu kwa sababu ibilisi ameachiliwa hakuna kitu kama hicho...
 
Sasa ibilisi afungwe kuna maana gani ya kufunga?Sawa sawa umpe mwanafunzi mtihani ambao hauna maswali.
 
Kwanini afungwe mwezi huu tu?

Ile mingine vipi hakamatiki?

Kama miezi mingine hakamatiki malaika wanao mkamata hawana uwezo.

Kafungwa kawekwa Gereza gani ?
 
Back
Top Bottom