ICC yambana Bensouda kesi ya Kenyatta

ICC yambana Bensouda kesi ya Kenyatta

Bensouda alikuwa anategemea ushirikiano kutoka serikali ya Kenya ambayo inaongozwa na huyo huyo Uhuru Kenyatta.

Binafsi sidhani kama Uhuru hana hatia lakini pia sidhani kama kuna ushahidi wa kutosha kumpata na hatia mahakamani kwa sababu ya mambo kama witness tampering n.k.

Sasa amini uhuru hana hatia, wenye hatia ni raila na kibaki
 
Navyojua ICC kuna mwendesha mashitaka na majaji...labda huyo alopewa amri ni mwendesha mashitaka (Chief Prosecutor) mimi namkumbuka Ocampo..alimaliza muda wake...aliye m replace simjui jina...

Mahakama ziko very complicated...watu wanafungwa wasio na hatia...wengine wanaachiwa huru wakiwa na makosa...kuna tofauti kati ya haki na sheria...

Kuna dada mmoja anatokea moja ya nchi za eastern Europe alikuwa anasimulia kuhusu mshitakiwa mmoja sijiu Serbia sijui wapi..naye alikuwa kwenye moja ya mahakama The Hague...unaambiwa jamaa liko mahabusu lakini likipelekwa mahakamani linatumia ishara ambazo zinawaumiza mashaidi kwani ndizo walizokuwa wanatumia wakati wanawachinja...kuna siku shaidi kama hakufa basi alizimia mahakamani baada ya jamaa kuonyesha hiyo ishara...

Na cha kusikitisha hilo lishitakiwa linapelekewa flowers likiwa mahabusu na followers wake...haya mambo si unajua hata Hitler ana wafuasi...sasa victims wanaon ni upuuzi...maana jamaa alikuwa ndani lakini anakula good time...case haiamuliwi...mashaidi wanakufa kwa uzee...

Ndio maana wananchi wanaamuaga kuchukua sheria mkononi...
Ona sasa Egypt...Jeshi si limemuachia huru Mubarak...wa Egypt wamefura...cha kufanya hawana...nadhani wanatamani wangemtia moto tu....

Baada ya Ocampo ndo Bensouda
 
nyumba kubwa, Adharusi, Nyani Ngabu,
CJ wa Tz mohamed chande na fatou bensouda walikuwa 2 finalists kwenye process ya kumrithi ocampo.

Wakuu wa AU ndiyo walioamua kum-support mama bensouda kwa hiyo cj mohamed chande akarudi kuendelea na kazi yake Tz.

Now can u imagine mahusiano ya Tz na Ky yangekuwaje with mohamed chande as ICC chief prosecutor huku akimfuatilia Uhuri Kenyatta na Wiliam Ruto?

Tungeshaletewa jeshi hadi arusha
 

Kenya yupo Bensouda pia


 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom