Idadi kubwa ya members wa JF inaonesha wanapishana sana na moja kati ya hizi KKK.3

Idadi kubwa ya members wa JF inaonesha wanapishana sana na moja kati ya hizi KKK.3

ANGALIZO; Tunapojivunia yakuwa tu "Great Thinker" hatunabudia pia kuwa makini katika uandishi, usomaji, na uhesabuji hasa juu ya Lugha yetu ya Taifa (Kiswahili).

Kwenye msafara wa Mamba na Kenge wapo.
 
Hili nimepata kuendelea kuliona kupitia ndani ya majukwaa (forums) ya humu JF, na linakua kwa kasi ya ajabu kadiri siku, miezi na miaka inavyojongea.

Kuna baadhi ya watu humu utakuta kama anajua Kusoma, basi hajui Kuandika, au kama anajua Kuandika basi hajui Kuhesabu au Kusoma.

Mwanzoni kipindi cha nyuma, nilidhani pengine ni mtu tu, anaweza kosea bahati mbaya katika uandishi (typing error) ila kumbe sivyo.
Mfn. Utakuta panapohitajika "r" mtu anaandika "l" au neno "Kuonesha" utakuta mtu tena na elimu yake ya kutosha tokea shule ya msingi mpaka anapata kazi anaandika au kutamka "Kuonyesha".
Au unaweza kuta panapohitajika herufi kubwa mtua anaandika ndogo.
Na hili ni kwa upande wa Lugha yetu ya Taifa (Kiswahili), upande wa Lugha nyingine nahofu kuliongelea maana hata mimi si mjuzi nazo.

Kwa anayebisha au wale wepesi wakuulizia neno "SOURCE", anza na hoja za wachangiaji humu humu....!

ANGALIZO; Tunapojivunia yakuwa tu "Great Thinker" hatunabudia pia kuwa makini katika uandishi, usomaji, na uhesabuji hasa juu ya Lugha yetu ya Taifa (Kiswahili).

Kwa kuanzia tuanze na wewe hapo kwenye RED.
 
Nitakuwa nimekosea kama nikisema na wewe ni wale wale?

Lipi neno sahihi kati ya "kuonesha" na "kuonyesha"?

kama umeshindwa kutofautisha kati ya mwenye ulemavu wa kuona na mwenye makengeza basi si makosa yangu. Ila siwezi KUKUONYA, ila naweza KUKUONESHA.
 
Kuna baadhi ya watu humu utakuta kama anajua Kusoma, basi hajui
Kuandika, au kama anajua Kuandika basi hajui Kuhesabu au Kusoma.

Hivi wewe mtoa mada,ulifikiria kweli?Inawezekana vipi mtu ajue kuandika halafu asiweze kusoma?..

jibu hapa ni rahisi tu. Kama wewe hapa umejua kusoma ila hujui kuandika. Asiweze kusoma = Hasiweze kusoma. Jipime uone wapi panakufaa.
 
kama umeshindwa kutofautisha kati ya mwenye ulemavu wa kuona na mwenye makengeza basi si makosa yangu. Ila siwezi KUKUONYA, ila naweza KUKUONESHA.

Haya bana. Wapo walioanzisha mpaka thread juu ya matumizi ya haya maneno:

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-lugha/125825-kuonesha-au-kuonyesha.html


https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-lugha/101110-tofauti-kati-ya-onesha-na-onyesha.html

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-lugha/27556-ni-onesha-au-onyesha.html

Neno "kuonyesha" nimefundishiwa tokea nikiwa shule ya msingi kuwa ni sahihi.

Bado siamini kuwa wewe upo sahihi na mwalimu wangu wa primary alikuwa wrong.

I'm sure Dingswayo, Chamoto, Nyani Ngabu Gaijin, Mathias Byabato Tukufu, Ntaramuka, Maamuma "watatuonyesha" njia.

Ni "maonyesho" au "maonesho" ya mavazi?
 
Last edited by a moderator:
Haya bana. Wapo walioanzisha mpaka thread juu ya matumizi ya haya maneno: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-lugha/125825-kuonesha-au-kuonyesha.html

Neno "kuonyesha" nimefundishiwa tokea nikiwa shule ya msingi kuwa ni sahihi.

Bado siamini kuwa wewe upo sahihi na mwalimu wangu wa primary alikuwa wrong.

I'm sure Dingswayo, Chamoto, Nyani Ngabu Gaijin "watatuonyesha" njia.

Ni "maonyesho" au "maonesho" ya mavazi?

Kiswahili sanifu ni 'kuonyeshwa' litokalo na neno la tendo 'onyesha'. Hata hivyo neno 'onesha' inatumiwa pia na baadhi ya watu katika lahaja zao na hivyo kuonekana kwao kuwa ni sahihi.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Haya bana. Wapo walioanzisha mpaka thread juu ya matumizi ya haya maneno:

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-lugha/125825-kuonesha-au-kuonyesha.html


https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-lugha/101110-tofauti-kati-ya-onesha-na-onyesha.html

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-lugha/27556-ni-onesha-au-onyesha.html

Neno "kuonyesha" nimefundishiwa tokea nikiwa shule ya msingi kuwa ni sahihi.

Bado siamini kuwa wewe upo sahihi na mwalimu wangu wa primary alikuwa wrong.

I'm sure Dingswayo, Chamoto, Nyani Ngabu Gaijin Justin Byabato, Tukufu, Ntaramuka, Maamuna, "watatuonyesha" njia.

Ni "maonyesho" au "maonesho" ya mavazi?

mkuu, maneno yote yapo sahihi, ila inategemea unalitumia wapi ili lilete maana sahihi iliyokusudiwa.
 
Last edited by a moderator:
Kiswahili sanifu ni 'kuonyeshwa' litokalo na neno la tendo 'onyesha'. Hata hivyo neno 'onesha' inatumiwa pia na baadhi ya watu katika lahaja zao na hivyo kuonekana kwao kuwa ni sahihi.

Nakubaliana na uliyosema kwenye ile thread nyingine kuwa neno "onesha" linatumika zaidi Zanzibar kuliko bara.

Huku Bara wengi wanatumia zaidi neno "onyesha"
 
mkuu, maneno yote yapo sahihi, ila inategemea unalitumia wapi ili lilete maana sahihi iliyokusudiwa.

Nimecheki Revised Edition ya Concise English-Swahili Dictionary (Kamusi ya Kiingereza - Kiswahili) iliyoandikwa na R.A Snowxall and H.B. Mshindo na kuchapishwa na Oxford University Press, Dar Es Salaam, mwaka 2002.

Waandishi hao wametafsiri neno "show" kama "kuonyesha", "Maonyesho", "kujionyesha"

Pia wametafsiri neno "shown" kama "onyesha" na kulitolea mfano wa "onyesha mfano".

Katika tafsiri zote mbili hawakughusia kabisa neno "kuonesha" au "onesha"

Unaweza kusema kuwa waandishi hao wametafsiri kimakosa?

Kwa mfano, nikiandika kesho ITV "wataonyesha" Champions League live nitakuwa nimekosea?

cc. Dingswayo
 
Katika kamusi yangu ya Johnson and Madam iliyochapishwa mara ya kwanza mwaka 1939 inasema hivi:

1. Onya: cause to see, show, display.[e.g nilimwonya njia].
1-1. Onyesha: Cause to see, demonstrate, show, point out, make clear, exhibit, place on view. [e.g. nilimwonyesha njia]
Note: the simple Cs form onesha is never used

2. Onya: warn, admonish, reprove. [e.g. Nilimwonya asiende]

Kwa hiyo sio kwamba denoo49 hajui matumizi ya herufi kubwa na ndogo katika uandishi pekee lakini pia hajui Kiswahili sanifu licha ya kujileta hapa na kujipa kuwasusuika wengine kwa makosa yote hayo mawili

Hawa wanaodhani neno sahihi ni "onesha" kwa kulinganisha na kazi ya jicho ya kuona, wanasahau kuwa Kiswahili ni lugha iliyoanza kimatamshi na sio kisarufi hivyo watu kutumia maneno yaliyokuwa rahisi kutamka licha ya kuwa kisarufi hayapo sahihi

Hao ndio wanaotaka mtu aseme "mtoto kamshindwa" badala ya "mtoto kamshinda" na "mtoto kaibwa" badala ya "mtoto kaibiwa"

Katika Kiswahili sio kila neno linafuata kanuni za sarufi

CC: EMT
 
mleta mada mwenye KKK kwake ni tatizo,kwa hiyo kajisema mwenyewe.
 
Hili nimepata kuendelea kuliona kupitia ndani ya majukwaa (forums) ya humu JF, na linakua kwa kasi ya ajabu kadiri siku, miezi na miaka inavyojongea.

Kuna baadhi ya watu humu utakuta kama anajua Kusoma, basi hajui Kuandika, au kama anajua Kuandika basi hajui Kuhesabu au Kusoma.

Mwanzoni kipindi cha nyuma, nilidhani pengine ni mtu tu, anaweza kosea bahati mbaya katika uandishi (typing error) ila kumbe sivyo.
Mfn. Utakuta panapohitajika "r" mtu anaandika "l" au neno "Kuonesha" utakuta mtu tena na elimu yake ya kutosha tokea shule ya msingi mpaka anapata kazi anaandika au kutamka "Kuonyesha".
Au unaweza kuta panapohitajika herufi kubwa mtua anaandika ndogo.
Na hili ni kwa upande wa Lugha yetu ya Taifa (Kiswahili), upande wa Lugha nyingine nahofu kuliongelea maana hata mimi si mjuzi nazo.

Kwa anayebisha au wale wepesi wakuulizia neno "SOURCE", anza na hoja za wachangiaji humu humu....!

ANGALIZO; Tunapojivunia yakuwa tu "Great Thinker" hatunabudia pia kuwa makini katika uandishi, usomaji, na uhesabuji hasa juu ya Lugha yetu ya Taifa (Kiswahili).
Tuko pamoja mkuu.
 
Katika kamusi yangu ya Johnson and Madam iliyochapishwa mara ya kwanza mwaka 1939 ..

Asante Gaijin. Mleta mada aje na authorities. Siyo anajisemea tuu.

I was a bit worried kuwa nimekuwa nikiandika kimakosa for all those years.

Ila hiyo dictionary yako ya mwaka 1939 imenimaliza kabisa. Bado ipo sokoni?
 
Last edited by a moderator:
Nimecheki Revised Edition ya Concise English-Swahili Dictionary (Kamusi ya Kiingereza - Kiswahili) iliyoandikwa na R.A Snowxall and H.B. Mshindo na kuchapishwa na Oxford University Press, Dar Es Salaam, mwaka 2002.

Waandishi hao wametafsiri neno "show" kama "kuonyesha", "Maonyesho", "kujionyesha"

Pia wametafsiri neno "shown" kama "onyesha" na kulitolea mfano wa "onyesha mfano".

Katika tafsiri zote mbili hawakughusia kabisa neno "kuonesha" au "onesha"

Unaweza kusema kuwa waandishi hao wametafsiri kimakosa?

Kwa mfano, nikiandika kesho ITV "wataonyesha" Champions League live nitakuwa nimekosea?

cc. Dingswayo

Hivi watu wanajua hata kuna tovuti ya BAKITA?

Hivi vipande hapa chini nimevitoa huko huko kwenye tovuti ya BAKITA.

Baraza la Kiswahili la Taifa huandaa na kutoa machapisho yanayoonyesha kazi mbalimbali. Baadhi ya machapisho ni:

Bofya hapa kwenda kwenye huo ukurasa.

BAKITA hushiriki kwenye maonyesho mbalimbali ya Vitabu ili kutangaza kazi, na bidhaa za BAKITA yakiwemo machapisho. Maonyesho hayo ni pamoja na:

Bofya hapa kwenda kwenye huo ukurasa.

Na bofya hapa kwenda kwenye ukurasa wa nyumbani wa BAKITA.

Kamusi za TUKI, ile ya Kiswahili-Kiingereza na ile ya English-Swahili, zote zina neno "onyesha".

Hata ile ya Kiswahili sanifu ya OXFORD, iliyochapishwa mwaka 2012 na yenye maneno yasiyopungua 224, 000 na ambayo ina maneno mengi ya Kimvita, nayo ina neno "onyesha".
 
Kiswahili hicho.

'"Mkoa wa Kinondoni wa kipolisi umefanikiwa kuwakamata watu sita wanaoshukiwa kuwa ni majambazi kufuatia operesheni tofauti zinazoendelea mkoani humo."

Ni dhahiri kuwa haiwezekani kuwakamata majambazi kufuatia operesheni inayoendelea mkoani humo. Kimantiki inawezekana kuwakamata majambazi kutokana na operesheni inayoendelea mkoani humo."

Jifunze Kiswahili Uwafunze na wengine - Kolamu - mwananchi.co.tz
 
002..JPG



Hawa jamaa lazima watakuwa wanakosea kila mwaka.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
002..JPG



Hawa jamaa lazima watakuwa wanakosea kila mwaka.

Umenifanya nikacheki tafsiri ya neno "exhibition".

Neno hilo limetafsiriwa kama "maonyesho", "uonyeshaji"
 
Back
Top Bottom