Kkimondoa
JF-Expert Member
- May 31, 2014
- 4,453
- 4,933
Wana JF naomba kujuzwa, kwa anayefaham kiwango cha fimbo, anachotakiwa kuchapwa mwanafunzi pindi anapofanya kosa shuleni? Maana huku kwetu st kayumba naona kumchapa mwanafunzi imekua fashion..utakuta kijana anachapwa hadi anaichukia shule.
Natanguliza shukran wana jamvi
wewe kama ni mzazi tumia busara kwenye sana kwenye hilo swala. Maana unaweza kusimama upande wa mwanao kumbe ni mkorofi sana shuleni. Na mzazi ukisha kuwa unamtetea hivyo mwanao unamtengenezea mazingira ya kufeli maana utakuwa unaanzisha mgogoro na walimu. Maana jua uki anza mgogoro na mwalimu mmoja ni sawa na kuingia mgogoro na staff nzima, yaani ni kama polisi ukikosana na mmoja basi unapata shida na wote. Na atakaye umia hapo ni mwanao maana hao hao walimu ndio wana dhamana ya mwanao kitaaluma ukiwatibua ni rahisi sana kumfelisha mwanao hata kumuandikia ripoti chafu baraza la mtihani ambayo itamfelisha
ushauri fuatilia kosa la mwanao lililo sababisha achapwe ili ujue chanzo. Coz unaweza kumtetea kumbe kosa lake lilikuwa la kufukuzwa shule ila mwalimu kaona amuadhibu yaishe,halafu mtoto akaja kwako kukueleza uongo utakao mlinda yeye ili aonekane hana hatia. so tumia busara tu kwa hli ili usimuumize mwanao kitaaluma achana na hao wanao jifanya wanasheria poli wakati hawana hakika na wanacho kueleza maana nao wamesikia mitaani . Kuhusu idadi ya viboko kwa mujibu wa sheria visizidi 6 kwa kosa kubwa . Na zaidi ni mtoto kurudishwa nyumbani hadi hapo bodi ya shule itakapo kaa,