Idara ya Marine Parks: Mfano wa Serikali Inayojihujumu Yenyewe

Idara ya Marine Parks: Mfano wa Serikali Inayojihujumu Yenyewe

Mwingereza

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2014
Posts
1,115
Reaction score
2,771
Kwa wakazi wa Dar-es-Salaam masikini na tajiri, kwa muda mrefu , wamekuwa wakienda kwenye visiwa vya Mbudya na Bongoyo kwa ajili ya mapumziko ya masaa. Wanafunzi wengi sana kutoka kwenye vyuo wamekuwa wakimiminika kwa wingi siku za weekend kwa ajili ya mapumziko.

Gharama zilikuwa nzuri sana na Rafiki. Tsh. 3000 ndio kiwango ambacho watanzania wamekuwa wakitozwa. Ghafla gharama imeongezeka mara 4 (Tsh. 12,000). Kwa sasa Mtanzania yeyote kwenda Mbudya au Bongoyo ni mtihani. Wageni ndio kabisaaa Tsh. 40,000

Matokeo ya hizi gharama imekuwa mbaya sana. Wikendi iliyopita nilienda Mbudya na mdogo wangu, tukajikuta tuko watu 14. Kipindi cha nyuma kwa siku lile eneo, asubuhi hadi jioni hapakosekani watu 700 hadi 1000. Boti ilikuwa zinakuja na watu wengi sana, na pia kuwarudisha wengi. Kwa sasa, boti zinakuwa na trip moja au mbili

Kwa akili yangu hii ni Serikali kujihujumu yenyewe. Inapandisha gharama mara 4 na kujikosesha mapato ambayo yalikuwa ni ya uhakika. Wanafunzi wanategemea wazazi na boom ya chuo, hawawezi kujilipia hizi gharama kubwa. Mmachinga anayetaka kupumzika hata kwa siku moja, hawzi kumudu gharama.

Kwa mfano, Boti kwenda mbudya ni 10,000. Chakula 15,000 na Kiingilio ni Tsh. 12,000 jumla unalipa tsh. 37,000 au tuseme 40,000. Kwa watu hali ya chini, hii kodi ya chumba kwa mwezi. Na ndio maana Mbudya pamekauka. Wakushanya kiingilio wanalia sana, wanaomba watu wenye nguvu wafikishe hii kilio kwa wakubwa maana wanaumia sana
 
Win-Win situation inaonekana wingi wa watu haukua na faida kiuhifazi hivyo limefanywa kuokoa uhai wa mazingira, mazingira uhai wake ni bora kuliko hizo pesa za wahuni, when a destination becomes too cheap and for everyone kuna hatari yake ya kuondoa dhana ya mvuto ya sehemu yenyewe, aina ya uamuzi kama huo unafaa ili kuokoa hali ya eneo. Originally Mbudya and Bongoyo wasnt for everyone.

Boosterism saa ingine ndio madhara yake.

Wa apply sustainability approach.

Ukosefu wa wataalamu wa parameters za assessment ndio tatizo.

Managing supply and demand side.

Pricing inahitaji akili sana ikitumika kama technique ya kuregulate visitor flow kwenye destination.

How is self-sustainance working with bongoyo and mbudya? How much of the income generated goes back or is retained to maintain, ehnance, repair, rehabilitate or restoring the place?

Is there anything like going green campaign for these destinations, anything like participatory campaign to improve the environmental conditions of these places?

Is there anything like Responsible weeekend let's go Mbudya, Let's go Bongoyo. Where the domestic individuals, foreign nationals etc would each be voluntarily and responsibly assigned to plant at least one tree.

More so what about the education and intetpretation services for the visitors. Are there Visitor management Models or rather frameworks at these places?

NB: Let's go for sustainable mass tourism.

Only a piece of opinion.

I submit while i stand for additions,objections, comments, questions, etc.

Double G.
The wahuni do not sound well and squarelly inclussive.kindly ignore this word.
 
Win-Win situation inaonekana wingi wa watu haukua na faida kiuhifazi hivyo limefanywa kuokoa uhai wa mazingira, mazingira uhai wake ni bora kuliko hizo pesa za wahuni, when a destination becomes too cheap and for everyone kuna hatari yake ya kuondoa dhana ya mvuto ya sehemu yenyewe, aina ya uamuzi kama huo unafaa ili kuokoa hali ya eneo. Originally Mbudya and Bongoyo wasnt for one.

Boosterism saa ingine ndio madhara yake.

Wa apply sustainability approach.

Ukosefu wa wataalamu wa parameters za assessment ndio tatizo.

Managing supply and demand side.

Pricing inahitaji akili sana ikitumika kama technique ya kuregulate visitor flow kwenye destination.

How is self-sustainance working with bongoyo and mbudya? How much of the income generated goes back or is retained to maintain, ehnance, repair, rehabilitate or restoring the place?

Is there anything like going green campaign for these destinations, anything like participatory campaign to improve the environmental conditions of these places?

Is there anything like Responsible weeekend let's go Mbudya, Let's go Bongoyo. Where the domestic individuals, foreign nationals etc would each be voluntarily and responsibly assigned to plant at least one tree.

More so what about the education and intetpretation services for the visitors. Are there Visitor management Models or rather frameworks at these places?

NB: Let's go for sustainable mass tourism.

Only a piece of opinion.

I submit while i stand for additions,objections, comments, questions, etc.

Double G.
I second you.
 
Ukweli ni kuwa mtoa mada utafute kanuni ya zamani na mpya usome vizuri tumeingia huko Mbudya Mara nyingi. Hakunaga tozo la 3000 huko umetoa wapi.

Kisiwa hicho ni Reserve tofautisha na Kunduchi beach Kuna kitu kinaitwa carrying capacity watu wakiwa wengi kelele nyingi,mmomonyoko zaidi,utupaji taka zaidi,uhalifu zaidi. Uthibiti huo unatuhakikishia Wala Bata usalama/watalii.

Mtoa mada rejea sera ya Tanzania ni Utalii endelevu/ Low number of visitors,High yield,sustainable environment. Mazingira kwanza sio pesa kwanza.

Visiwa vya Dar vikimomonyoka nyumba zote Kawe, Mbezi beach, Kunduchi zitapata mawimbi makali kwani visiwa hivyo ni Kama bumps kuzuia kasi ya mawimbi.

Thamani ya rasilimali kwenye fukwe hizo zinategemea usalama wa kisiwa hiki. Hatutaki Mbudya iwe Kama Mombasa beach wageni wengi mataka mengi. Hatma kisiwa mnakitumia miaka kumi pesa mmepata ila kisiwa kinachoka. Hatutaki hayo.

Big up mlioongeza tozo kupunguza watu. Mbudya imepata heshima yake.
 
tafiti ya siku moja haiwezi kukufanya kuja na hitimisho chief..Endelea kufanya utafiti angalau mwaka mzima baada ya kupanda kwa gharama hizi then ndo uje na hitimisho
 
... niko huku wilaya ya Tanganyika magharibi mwa nchi Chief.
Ni visiwa viko Baharini karibu kabisa na jiji la Dar es Salaam, takribani km 10 kutoka ufukweni. Huwa viko kama vinne au vitano hivi. Vinafikika kwa urahisi zaidi kwa boti kutokea Slipway, Masaki
 
Kwa wakazi wa Dar-es-Salaam masikini na tajiri, kwa muda mrefu , wamekuwa wakienda kwenye visiwa vya Mbudya na Bongoyo kwa ajili ya mapumziko ya masaa. Wanafunzi wengi sana kutoka kwenye vyuo wamekuwa wakimiminika kwa wingi siku za weekend kwa ajili ya mapumziko.

Gharama zilikuwa nzuri sana na Rafiki. Tsh. 3000 ndio kiwango ambacho watanzania wamekuwa wakitozwa. Ghafla gharama imeongezeka mara 4 (Tsh. 12,000). Kwa sasa Mtanzania yeyote kwenda Mbudya au Bongoyo ni mtihani. Wageni ndio kabisaaa Tsh. 40,000

Matokeo ya hizi gharama imekuwa mbaya sana. Wikendi iliyopita nilienda Mbudya na mdogo wangu, tukajikuta tuko watu 14. Kipindi cha nyuma kwa siku lile eneo, asubuhi hadi jioni hapakosekani watu 700 hadi 1000. Boti ilikuwa zinakuja na watu wengi sana, na pia kuwarudisha wengi. Kwa sasa, boti zinakuwa na trip moja au mbili

Kwa akili yangu hii ni Serikali kujihujumu yenyewe. Inapandisha gharama mara 4 na kujikosesha mapato ambayo yalikuwa ni ya uhakika. Wanafunzi wanategemea wazazi na boom ya chuo, hawawezi kujilipia hizi gharama kubwa. Mmachinga anayetaka kupumzika hata kwa siku moja, hawzi kumudu gharama.

Kwa mfano, Boti kwenda mbudya ni 10,000. Chakula 15,000 na Kiingilio ni Tsh. 12,000 jumla unalipa tsh. 37,000 au tuseme 40,000. Kwa watu hali ya chini, hii kodi ya chumba kwa mwezi. Na ndio maana Mbudya pamekauka. Wakushanya kiingilio wanalia sana, wanaomba watu wenye nguvu wafikishe hii kilio kwa wakubwa maana wanaumia sana
Maskini starehe waachie wenyewe, unataka kustarehe alafu unawaza elfu 40. Watu wanalipa villa ucku mmoja milioni 9 mpaka 10. Tujifunze kula urefu wa kamba zetu ukiona huwezi nunua suruali moja laki na kuendelea usiende mlimani city, nenda kariakoo ambapo utanunua suruali kwa elfu 20.
Pia kumbuka kuna kitu kinaitwa sustainable tourism. Ambayo ni chini ya udhamini UN Environent program. Ambayo lengo lake ni kujaribu kwa kadili inavowezekana kupunguza social and environmental impacts. Na kwa visiwani hapa wanajikita zaidi kwenye uharibifu wa mazingira. Badala ya kupokea watalii mia 7 wanapokelewa mia kwa gharama kubwa.
Lengo ni kupata kidogo kidogo kwa muda mrefu, kuliko kupata kingi kwa muda mfupi. Ukitafakari utagundua huo ndo mkakati. Destination nyingi zinajaribu kuweka gharama za juu ili ku avoid overcrowded tourist.
 
tafiti ya siku moja haiwezi kukufanya kuja na hitimisho chief..Endelea kufanya utafiti angalau mwaka mzima baada ya kupanda kwa gharama hizi then ndo uje na hitimisho
Kuna mazingira yanalazimu mkuu
 
Watanzania ndivyo walivyo ndugu yangu, yeye NI bora apewe laki tano kwa mkupuo kuliko laki moja ya kila siku. Sio akili ni matope.
 
Back
Top Bottom