TheDealer naona unaenda kimapepe sana,please try hata kucopy huko marekani kampuni kama yako hiyo wanavyofanya...come open nd be professional....
Unaweza kufund projects za max capital kiasi gani?Za sekta zipi hasa?Usije kisanii namna na slang za "Ova"...piece of BS!
Taja jina la kmpuni yenu,web link yenu,portifolio za kmapuni mlizofund na zimefanikiwa ngapi...na jee are u guys nice to work with?
Hii ni partnership,kuwe na mutual respect na sio unakuja hapa na kusema leteni idea,mtu hajui who are u...
Kajipange vizuri mzee and stop being dellusional
Hawa watu meshindwa kuwaelewa mewatumia idea yangu kupitia email yangu ila baadae nilipotaka kulog in kwenye email yangu nilitaarifiwa kwamba gmail wamegundua kuna shughuli zinaendelea kwenye email yangu zisizo za kawaida na mpaka sasa meshindwa kulog in kwenye email yangu. Hawa watu sidhan kama ni wema
Same ideas but different goals, so don't give up, biashara inahitaji confidance, don't be scare to loose.
Mwaka 2009 nikiwa nilikuwa na idea's yangu, ya ki technology, wakati huo nipo nchini Ireland, idea hio matumaini yangu kama ningefanikiwa ningekuwa bilinear, idea ile niliwasiliana na manufacturer in China wanitengezee one sample kwanza, Ikisha tutafanya contract nikifanikiwa kwa ajili ya kuingiza katika soko la ulaya,
wakaniambia ita ni cost dola 2000, nikawambia sawa, baadaye wakanitumia email kuwa wanataka dola 32,000 Nikaona hawa wanataka mchezo mchafu, na ile idea walinambia ni new technology so lazima waifainyie kazi, mimi nikawambia sawa wanifanyie lakini sikuwa na pesa za kutosha, baada ya muda wale jamaa manufacturer kila nikipiga simu hawapokei na wakipokea wanakata,nikasema nishatiwa changa la macho.
My goal ilikuwa nipeleke katika competition katika mambo ya wataalam, na nilikuwa naa mini inaweza kupita. Kwani ilikuwa ni new idea ya ki technology.
Samahani Lakini Naweza kutuma idea yangu kwa email..mkakaa kimya huku mkiifanyia kazi..
Au Nikiwapa mnaweza sema hiyo tulishaipata na kuifanyia kazi kumbe loh
Na mengineyo kama hayo..
Nazungumzia hivyo kwa sababu kuna mwenzangu (rafiki yangu sana sana) tulitaka kuanzia biashara based on agrubusiness Mi nikawa na idea na fursa za masoko ila kufinance yeye kwa 80% sasa wakati tukiwa katika kukaribia kuanza project kama wiki moja sasa tuanze akaniambia ameibiwa hela kwenye MPESA yake yaani kuna rafiki yake aliazima simu kumbe anajua passwors yake ni mwaka wa kuzaliwa akachukua hela yote kisha akatoweka mpaka leo..
Kumbe jamaa ni mwongo hakuibiwa wala nini ila alichukua ile hela akatuma kwao waanze ile project na kweli ikaanza sasa Mungu si athuman nlikuwa nafahamiana na mdogo wake siku tukakutana facebook aliponisimulia nilisikitika sana sana sana.
Nimetoa mfano huo labda naomba unieleweshe hapo Nikikupa idea yangu idea yangu hiyo italindwaje?? (Kiswahili kumenishinda kidogo namna ya kuuliza)
labda nijaribu kwa kiingereza How my idea will it be protected??
Aiseeee.......usitake kutumia JF kama kokoro la kutupia kila kitu!
Wee kama huna idea ya business tuliza mshono! Waache wenzako waje!
The Dealer mimi nina idea lakini lazima tukutane na kuwekeana mkataba wa kutoitumia au kuiuza kwingine kwa kuchangia gharama za kisheria baina yetu; Ukiwa tayari nifahamishe
Mwaka 2009 nikiwa nilikuwa na idea's yangu, ya ki technology, wakati huo nipo nchini Ireland, idea hio matumaini yangu kama ningefanikiwa ningekuwa bilinear, idea ile niliwasiliana na manufacturer in China wanitengezee one sample kwanza, Ikisha tutafanya contract nikifanikiwa kwa ajili ya kuingiza katika soko la ulaya,
wakaniambia ita ni cost dola 2000, nikawambia sawa, baadaye wakanitumia email kuwa wanataka dola 32,000 Nikaona hawa wanataka mchezo mchafu, na ile idea walinambia ni new technology so lazima waifainyie kazi, mimi nikawambia sawa wanifanyie lakini sikuwa na pesa za kutosha, baada ya muda wale jamaa manufacturer kila nikipiga simu hawapokei na wakipokea wanakata,nikasema nishatiwa changa la macho.
My goal ilikuwa nipeleke katika competition katika mambo ya wataalam, na nilikuwa naa mini inaweza kupita. Kwani ilikuwa ni new idea ya ki technology.
Pole sana, hii inatokea sana kwa matapeli wa idea za watu lakini kuna company nzuri pia kama bright ideas ya UK hao unawapa idea wanaangalia kama haijatoka bado duniani, wanakuambia utoe let's say £450 inategemea na idea yako halafu ikipita una shauriwa uwe na lawyer mnasaini mikataba na wanaifanyia kazi, lakini hapa naona hajajieleza vizuri
Hebu Nipe maelekezo hapa uk wapi pa kupeleka ideas?
Zipo kampuni nyingi ambazo unaweza kupeleka idea yako lakini watakula hela, ila kama una idea nzuri jaribu patent office (IPO) hao wataangalia kama idea yako ipo au haijawahi tengenezwa UK ukisajili itakuwa yako kwa miaka 20, lakini itakuwa public kwa muda wa miezi 18 watu kuiona baada ya kuisajili, hapo utashika Patent attorney (awe amesajiliwa) na kama idea yako itaibiwa baada ya kusajili unaweza kuipeleka kesi mahakamani hapo mahakama itaamua either kupata haki yako au la.
Hii ni kwa UK tu