If God knows the future (omniscient), can you change your destiny?


Kwa nini mungu amuandikie kiumbe kupotea?

Wakati ana uwezo wa kumuandikia kutopotea?

Si tunaambiwa mungu huyu ni "the most merciful"?

Sasa inakuwaje "the most merciful" amuandikie kiumbe wake kupotea kwa namna ambayo huyo kiumbe hawezi kuibadikisha? Wakati mungu huyu sna uwezo wa kumuandikia kiumbe ssipotee bila kupungukiwa kitu? Mungu gani mwenye roho mbaya ya kubania viumbe wake kama huyu?

Sasa kiumbe akipotea, kwa sababu kandikiwa kupotea na mungu kwa.namna.ambayo kiumbe huyo hawezi kuibadilisha, sikunya.hukumu.mungu atamhukumu kiumbe.huyu kwa kupotea?

Na kumpeleka motoni?

Hata kama mungu mqenyewe ndiye aliyemuandikia kupotea kwa namna ambayo kiumbe hawezi kuibadikisha?

Fikra hizi zina mantiki kweli?

Au ni fikra za kufikirika tu za kuhusu mungu asiyekuwepo?
 

kiranga unaongeaje na kutaja kitu ambacho hakipo!!!!?@
 

Bold-Utaonaje wakati unawaweka watu kwenye ignore list?
LET US DEBATE

I will prove it to you that HE exist.

TAKE ME OUT OF YOUR IGNORE LIST, SO THAT I CAN PROVE IT TO YOU.

GUYS, TELL THIS PERSON, TO DEBATE WITH ME.

I WANT TO PROVE THAT GOD DOES EXIST.
 

How does the opposite prove he does not exist?
 

kiranga unaongeaje na kutaja kitu ambacho hakipo!!!!?@

Hii ndio dawa yake. Safi sana mkuu.

Jamaa anaongea mwenyewe kama ameingiwa na fiendish spirit. Msaidieni huyo kiumbe, anako elekea sasa ni pabaya. especially mtu anapo anza kujiongelesha mwenyewe kama alivyo fanya hapa.
 

How does the opposite prove he does not exist?

Jamaa sasa anajiongelesha mwenyewe!!! Msaidieni, maana symptoms za kupoteza akili huwa zinaanzaga hivi.
 
Jamaa sasa anajiongelesha mwenyewe!!! Msaidieni, maana symptoms za kupoteza akili huwa zinaanzaga hivi.

Huwa tu najiuliza;

Hivi kama mtu akisema kuna mwizi amepita mtaani kwao saa kumi na moja alfajiri akiwa anakimbia halafu akadaiwa ushahidi akakosa sijui itakuwa huyo mwizi hayupo?

Sijui mtu unawezaje kuona unafikiri sawasawa halafu unafikia hitimisho la namna hii

Mara aseme anatafiti ili ajue kama Mungu yupo
Mara anasema hayupo
Mara anasema hajui kama yupo

Unaweza kumuweka kwenye kundi gani mtu wa aina hii?

Ndio maana hata naanza kuona mbinu yake ya kukuweka kwenye ignore list ni kukimbia tu kwakuwa hapo kuna mambo mawili
  • Anajua Mungu yupo ila anaamua tu kukataa kwa sababu ambazo anazijua yeye
  • Anaogopa yeye kuwa ndio njia ya kusababisha wengine kuona uwepo wa Mungu [japokuwa hili wameshaliona wengine ambao wamekuwa wakifuatilia mijadala mingi hapa
Kimsingi kwa wale ambao wanafuatilia mijadala hapa wanaweza kuona tu kuwa kuna woga mkubwa hapo na sio kingine,kama unaweza kuthibitisha jambo fulani ni ukweli au uongo ni kwanini uogope?
 
kiranga unaongeaje na kutaja kitu ambacho hakipo!!!!?@

Hujajibu maswali.

Kama ether haipo, kuuliza maswali yatakayohoji.uwapo wa ether si kuongelea kitu ambacho hakipo.

Naongelea imani ya kuwapo mungu, ambayo ipo.

Mungu huyu yuko logically inconsistent.

Huku ana rehema kuu, huku anawapangia viumbe wake.kupotea.

Mwenye rehema kuu hapangii viumbe wake kupotea.

Mwenye kupangia viymbe wake kupotea hana rehema kuu.

Which is which?

Mungu ana rehema kuu au hana rehema kuu?
 
Mtumishi:
Umesema inavyo takiwa tena ni kabisaa kweli.

Huyu kijana anamatatizo mengi sana. La kwanza ni pale anapo tumia assumptions kwamba watu hawaelewi nini anasema kwa kuchomeka sayansia huku wengine wakifahamu kuwa, neno alilo liweka au chomekeza halihusiani na mada na wala halijibu swali au saidia mada. Hilo ni kosa ambalo analifanya kila siku, sasa atakapo tambua tu, umesha mgundua na au unafahamu hilo kosa lake, teyari atakuweka kwenye ile group yake inayo ifanya roho yake ifurai "ignore list".

Pili huwa anajichaganya katika majibu yake ambayo hayo consistent. Mfano, Siku fulani alisema "I am allergic to faith", nikamtega kwa kuingiza assumption na kifananisha na faith. Akaingia mkenge na kusema in fact, faith huwa inatumika kidogo katika sayansia. Teyari hapo umesha poteza kesi yako, maana huwezi kusema huna na hutumii faith halafu baadae ukasema, aaah aah huwa naitumia kigodo. Mimi huwa nasoma posti huku nikiangalia wapi kuna kosa na wapi kuna walakini. Hii ndio mbinu ya debate ambayo inatumiwa sana na watu wanao fanya debate kila siku. Ni kupoint out your errors and mistake na kukurudishia mwenyewe. Kwa kufanya hivyo, mpinzani wako anakuwa frustrated na kupoteza mwelekeo.

Ndio maana na wale ndugu zetu wa kuleee kwa Jibril, wanachukia, maana mbinu nni ile ile ya kuonyesha wapi kuna makosa kwao, halafu unawaacha wanakutukanaaaweeee huku wakionyesha udhaifu wa imani yao.

Anyways, mtu ambaye alimuona mwizi na baadaye kushindwa kuprove kuwa kuli kuwa na mwizi, bado yupo maana siku moja, mwizi atarudi tena na kufanya mengine.

Madai yake menginie ya hayupo, sijui anafanya utafiti na au hajui ni jibu tosha kuwa yupo, ndio maana anakosa usingizi maana fikra zake zimefika ukingoni na kushindwa kutathmini kuhusu huyo Mungu. Yaani mtu akisema tu kuwa hakuna Mungu, elewa kuwa kuto kuwepo kwa Mungu ndio kukiri kuwa yupo. (1) Kwanini unamwita Mungu? Hivi kitu kisicho kuwepo huwa kinafahamika na kupewa jina? (2) Kwanini wanataka kupewa ushaidi wa kuwepo kwa Mungu? Ni nini hasa kinacho wanyima usingizi na kutaka ushaidi wa Mungu kuwepo? (3) Kama Mungu hayupo, kwanini unatumia time yako kuzungumzia? Ni kwasababu yupo, na hawana jinsi ya kufanya zaidi ya kuendelea kupagawa akili zao.

Yesu ni Mungu
 

IN RED: Sasa ndugu yenu ameamua kuongelea imani ambayo anadai huwa hana. Huu ni msiba wa kwanza.
IN BLUE: Sasa umesha mpa na sifa ya Mungu wako kuwa yupo logically ...Huu ni msiba wa pili.
IN GREEN. Teyari amesha anza na kumpa sifa huyu Mungu ambaye hayupo. Huu ni msiba wa Tatu.
IN ORANGE: Sasa Mungu anapangia watu rehema kama vile sayansi ina kitu kama "rehema" Msiba wa nne.

Si mnaona jinsi ambayo jamaa yenu anavyo jiweka kwenye hali mbaya kila siku.

Sasa Muulizeni swali moja tu:
Kwanini anataka kufahamu kama Mungu yupo?
 
You have not answered the original question.

Your question is absurd, since one cannot prove a negative.

I didn't ask you to prove anything,re read my question

By the way,if you know can not prove your claim,what make you say he does not exist?
Or you just assuming?
 
You have not answered the original question.

Your question is absurd, since one cannot prove a negative.

Signature yako uliyo kopia kwenye Biblia yetu inasema:
Proverbs 23:9 Speak not in the ears of a fool: for he will despise the wisdom of thy words.

Sasa Biblia inakuji nani ni huyo "fool"
Psalm 14:1 For the director of music. Of David. The fool says in his heart, "There is no God." They are corrupt, their deeds are vile; there is no one who does good.

Ndio raha ya Biblia, inakujibu wewe kitaratiiiib
 

hujanielewa yani namaanisha unawezaje kuhoji kitu ambacho hakipo mana hadi unahoji icho kitu kipo.....huwezi kuuriza kitu ambacho hakipo...
 
hujanielewa yani namaanisha unawezaje kuhoji kitu ambacho hakipo mana hadi unahoji icho kitu kipo.....huwezi kuuriza kitu ambacho hakipo...

Unaweza kuambiwa bia ya Safari inatibu UKIMWI.

Kitu hicho hakipo, kwa maana ya kwamba bia haitibu.

Mtu mwenye akili akiambiwa "bia ya Safari inatibu UKIMWI" atahoji.

Unaweza kuhoji kitu ambacho hakipo, kwa mantiki kabisa. Kwa sababu hakipo.
 
Mkuu kuhusu rebirth nina mashaka nayo. kwani our numbers are increasing duniani, kama tunazaliwa tena tungeendelea kuwa constant ama sijui kama nimekupata vizuri..<
 
Unaweza kuambiwa bia ya Safari inatibu UKIMWI.

Kitu hicho hakipo, kwa maana ya kwamba bia haitibu.

Mtu mwenye akili akiambiwa "bia ya Safari inatibu UKIMWI" atahoji.

Unaweza kuhoji kitu ambacho hakipo, kwa mantiki kabisa. Kwa sababu hakipo.

Unatumia wrong comparison katika fikra yako. Jifunze kufanya research.

Ukimwi :UPO:
Bia :IPO:
Mtu :YUPO:

Sasa hii inahusiana vipi kw kushindwa kuleta uthibitisho wa "negative god" unaye muamini na abudu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…