Ifahamu Al Ahly watakaomenyana naSsimba SC

Ifahamu Al Ahly watakaomenyana naSsimba SC

1.Thamani ya kikosi cha Al Ahly ni Tsh Billion 89.3 huku thamani ya washambuliaji tu ikiwa ni Billion 50.3 wakati kikosi kizima cha simba sc kina thamani ya Bilion 1...Je Beki Sergi Wawa,Juko wanaweza kuzuia Washambuliaji hawa wenye thamani ya Billion 50 wasifunge magoli 5?

2.Klabu ya Al Ahly imecheza fainali ya CAF mara 2 mfululizo.Mwaka jana walicheza fainali na Esperance ya Tunisia na kushindwa na mwaka 2017 walicheza fainali na Wydad casablanca na kushindwa pia mwaka 2015 walicheza nusu fainali na mwaka 2014 walibeba taji la shirikisho na mwaka 2013 na 2012 walibeba taji la CAF mara 2 mfululizo wakati huo huo klabu ya simba hii ndio mara yao ya kwanza kushiriki michuano ya CAF ndani ya miaka 5..

3. Al Ahly ndio klabu ya pili yenye mafanikio zaidi kwenye michuano ya kimataifa duniani wakiwa nyuma ya Real Madrid yenye mataji 26 huku Al Ahly wakiwa na mataji 24.

4.Al Ahly ndio timu pekee inayoongoza kuwa na mataji mengi ya CAF champions league wakiwa na mataji 8 na rekodi ya makombe 4 ya African super cup.

5.Klabu ya Al Ahly imemsajili msimu huu kiungo mshambuliaji Hussein El shahaat kutoka klabu ya Al ain kwa rekodi ya ada ya uhamisho ya dollar 4.5 Million.El shahaat anatoka Al ain akiwa amecheza michezo 33 na kufunga mabao 15 na kutoa assists 17....Binafsi kwenye mchezo kati ya Al ahly na Vita club huyu player El shahaat nilimtizama alisumbua sana ni mbunifu na mara nyingi hutembea na mpira vigumu kupokonywa.

6.Al Ahly imemsajili mchezaji Mohamed mahmoud kutoka klabu ya Wadi degla kwa Dollar 1.5 Million .Kinda Mohamed anatanabaisha ya kuwa vilabu vya Hoffenheim,Fc Basel na Ajax vilimtaka lakini alivitolea nje licha ya mchezaji wa liverpool Mo salah kumshauri akubali kwenda basel lkn mohamed alikataa na kwenda klabu ya ndoto yake Al Ahly.

7.Al Ahly imemchukua kwa mkopo mchezaji wa timu ya Huddesfield inayoshiriki ligi kuu uingereza Ramadan sobhi.

8.Al Ahly ina wachezaji tishio kama El shahaat,sobhi,walid,marwan na Al ahly wanasifika kucheza pasi fupi fupi na kwa kasi.

9.Al Ahly ndio klabu yenye mashabiki wengi Africa na ni klabu yenye mashabiki wenye amsha amsha na makelele mara nyingi sana vilabu vikienda Misri huchachawa na makelele na amsha amsha za mashabiki na hupelekea kufungwa idadi kubwa ya magoli ..Al ahly kwa lugha ya kiswahili humaanisha taifa hivyo klabu ya Al ahly ni kama timu ya taifa huko misri na ndio maana ina wanachama na mashabiki wengi mno

View attachment 999930

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu utaua watu kwa pressure
 
Haya sasa kikosi cha Mwarabu ndio hichoooooo!!

Kazi kwenu wale mnaojiita Nguvu moja maana kipigo nakiona kiileeee. 💃💃💃
 
Nawakubali sana mashabiki wao muda wote kushangilia na kuimba wimbo wa timu kama wamechukua ubingwa
 
Kama pesa inacheza real Madrid wasingekuwa na hali ngumu, pia kikosi cha 89 billion je kwenye mashindano ya CAF wanapata kiasi gani kama wakichukua kombe?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama pesa inacheza real Madrid wasingekuwa na hali ngumu, pia kikosi cha 89 billion je kwenye mashindano ya CAF wanapata kiasi gani kama wakichukua kombe?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna mahali duniani zawadi ya kombe itakidhi mahitaji ya uendeshaji wa klabu nzima. Ila unapochukua kombe unajiweka kwenye mazingira mazuri zaidi ya kupata mikataba minono itayoboresha uchumi wa klabu. Usitegemee kurudisha pesa ya usajili kupitia kuchukua kombe. It only works kwa hizi timu ndogo maybe Simba au Yanga maana wao bajeti yao sio ya kutisha sasa inapotokea wakabeba hilo kombe kwao ni kama wameagana na umaskini.
 
Hakuna mahali duniani zawadi ya kombe itakidhi mahitaji ya uendeshaji wa klabu nzima. Ila unapochukua kombe unajiweka kwenye mazingira mazuri zaidi ya kupata mikataba minono itayoboresha uchumi wa klabu. Usitegemee kurudisha pesa ya usajili kupitia kuchukua kombe. It only works kwa hizi timu ndogo maybe Simba au Yanga maana wao bajeti yao sio ya kutisha sasa inapotokea wakabeba hilo kombe kwao ni kama wameagana na umaskini.
Lakini mbona wanatumia pesa nyingi sana inawalipa kweli?

Sent from my SM-G610F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom