Ifahamu Premier League Production | Uzalishaji wa Ligi Kuu

Ifahamu Premier League Production | Uzalishaji wa Ligi Kuu

isajorsergio

Platinum Member
Joined
Apr 22, 2018
Posts
4,143
Reaction score
6,560
Premier League, ligi kuu soka ya Uingereza ikifahamika vyema hapo awali kama BPL kabla ya mabadiliko mnamo mwaka 2015 toka BPL iliyokuwa ikiuza kupitia chapa ya Barclays Premier League chini ya mkataba wa udhamini kutoka kampuni maarufu inayoshughulika na masuala ya kiuchumi, fedha, uwekezaji na mabenki - Barclays. 2015 urasimishaji uliipatia uhuru ligi kuu hii na kutengeneza chapa ya upekee isiyohitaji ununuliwaji. Ni muda sasa duniani kote kumekuwa kukishuhudiwa urushwaji wa matangazo ya kandanda kupitia televisheni na redio, matangazo murua yenye muonekano ang'avu, sauti imara na ubunifu wa upekee.


Premier League 4.jpg

Chapa ya Premier League katika mitindo na muonekano tofauti.


Premier League hapo awali haikuwa na nguvu kama chapa na ndio maana baada ya mkataba wa muungano baina ya PL na Barclays, Premier League iliamua kuanza kutengeneza picha yake yenyewe katika jamii. Ubinifu akinifu kutoka kwa taasisi, kampuni na wabunifu mbalimbali ndio waliowezesha kutengeneza chapa unayoishuhudia kila wiki. Ni ushirika baina ya DesignStudio wale waliokuletea chapa za Airbnb, Deliveroo, GAP na Treatwell na DixonBaxi waandaaji chapa na mifumo ya picha mchocheo 'Graphics System' unazoziona leo, kuanzia maneno ya ufunguzi (Opening Titles), picha mchocheo (Graphics), video mchocheo (Animations), bao zenye kukutanisha timu (Hand Shake Boards), masuala ya uchapaji (Printing Collateral) na tiketi (Tickets).


PL_01.gif

Bao za kukutanisha timu.


DesignStudio vs DixonBaxi.jpg

Ushirika baina ya DesignStudio na DixonBaxi.

Ubunifu huu ulizingatia desturi, asili na kutofungamana baina ya PL na vilabu. Ndio mwanzo wa rangi zilizotanabaishwa kuwa za 'kike' na wafuasi wengi wa kandanda ulemwenguni lakini muda ulivyojongea uhalisia ukabaki mahala pake, na sasa ni wazi mvuto umezidi kuipa dili mbalimbali PL. Amewahi kueleza Bw. Maxence Melo
"...English Premium League kabla ya changes ikiwa inaitwa Barclays wao walibadili kabisa hadi rangi zao. Watu walijiapiza hawataangalia EPL wengine wakidai ni rangi za kike!" - @Maxence Melo


PL_13.jpg

Mfumo wa machapisho ya Premier League.


Je Premier League Production ufanyaje kazi? - Premier League Production ni shirika linalohusika moja kwa moja katika shughuli za uaandaji, uchakataji na urushaji matangazo kwa ushirikiano mkubwa na IMG kupitia PLP. Mechi 380, Magazine Shows na Televisheni inayorusha vipindi na matangazo 24/7 ikiwa inasaidiwa na vituo washirika. Urushaji wa matangazo umefikia ubora 4KHD, huku PLP ikiwa nyuma ya teknolojia ya VAR Live (Checking) inayoandaliwa moja kwa moja kutoka Stockley Park - IMG Studios.

Premier League Production husimamia uchukuaji maudhui katika viwanja 20 kwa kutumia ungamuaji wa IP Networks, Nevion VS 902, Nevion nSure FCS 1000 Plus kwa uchache, hapa urushwaji uanza kuendelezwa kupitia VideoIPath - Management and Orchestration hadi kuingia ndani ya jengo lenye ghorofa tatu IMG Studios. Kabla ya kufika IMG Studios, PLP hutumia wastani wa kamera 15 katika kila kiwanja wakati wa uchukuaji maudhui mubashara. Kamera nyingi zinazotumika ni Arri, GoPro, Leica na Pentax.


PL_03.jpg

Maudhui yafikapo IMG wataalamu mbalimbali uanza uchakataji na urushaji wa matangazo hayo mubashara. Uchakataji huu wa maudhui uzingatia kanuni na muongozo ya chapa husika PL. Kwa kutumia muundo uliondaliwa tayari na DesignStudio na DixonBaxi.


DixonBaxi Premier League Guide 001.jpg

Muonekano wa muongozo kabla ya kuchanganywa na maudhui kutoka uwanjani.


DixonBaxi Premier League 010.jpg

Muundo wa muda kabla ya kuchanganywa na maudhui kutoka uwanjani.


DixonBaxi Premier League.jpg

Muongozo mkuu wa yapi yafanyike wakati wa uchakataji na urushaji matangazo.


PL Trans.png

Uchanganyaji picha hufanyika.


Baada ya uchanganyaji maudhui.

Premier League Broader Visual.jpg



DixonBaxi Premier League 004.jpg



DixonBaxi Premier League 005.jpg



Leicester Premier League.jpg

PLP na IMG zimekuwa nyuma ya ligi nyingine vilevile. La Liga, Bundesliga na Seria A zimekuwa zikiishirikisha PLP na IMG kusaidia mambo baadhi katika mifumo ya urushaji matangazo.
 
Duh...makala yAko haijaeleweka..umetumia kiswahili cha google
 
Professionalism at its finest!

Uzi mzuri sana umeuleta, mimi ni shabiki mkubwa wa ligi kuu ya England. Ila uzi huu uliponivutia zaidi ni kuhusiana na mambo ya Graphic Design ndani yake.

Kwa miaka karibu mitano nafanya Graphic Design ni moja ya sekta kubwa sana duniani hususani kipindi hiki mitandao ikitumika kwa kasi. Makampuni na biashara nyingi zinawekeza nguvu kubwa kuzalisha machapisho ya kuvutia kupakia kwenye kurasa zao za kijamii wakishirikiana na wabunifu wenye uwezo mkubwa katika sekta.

Kwa Tanzania hii ni sekta inayokua sana kwa kasi ila haina wateja wengi kama inavyostahili: Graphic Designer wengi nchini hawapewi kazi wanazostahili, wengi wanaishia ku-design vipeperushi tu vya sherehe na tafrija mbalimbali.

Ni makampuni machache nchini yametoa fursa kwa wabunifu wa hapa nchini, pia kukosekana kwa wateja ndiyo kunaifanya sekta kufa pia taratibu.

Tukibaki hapahapa kwenye soka, viwango na ubunifu wa wabunifu wanaopewa nafasi ni mdogo sana. Ukipitia page za timu kubwa kama Simba SC na Yanga SC unaweza kujiuliza maswali mengi ni aina gani ya Graphic Designer Ruvu Shooting FC watakuwa naye! Ukipitia page za TFF pia na aina ya machapisho yao utajua safari ni ndefu kufikia kutoa ubora stahiki.

Hii ni moja ya sekta inayochukuliwa poa na wengi na serious na wachache.

Ukitaka kujua ubunifu umeisaidia EPL ni katika branding, sasa hivi hiyo logo yao ukiiona bila maandishi unajua tu ni logo ya EPL. So hapa katika branding wamefaulu.

Juzujuzi Simba SC nao walifanya rebranding logo yao ila bado niliona kitu walichokipata hakikna ubora kulingana na brand ya Simba SC. Graphic Designer wachache wali-shout kuonyesha evidence kuwa Simba aliyewekwa kwenye logo alitolewa tu kwenye Adobe Stocks na kupachikwa.

Katika Branding, Simba SC walipaswa kwenda mbele zaidi na kuwakimbia wazawa, wangewapa kazi wabunifu kutoka nje naamini wangepata kitu kizuri sana kuitambulisha Club yao. Bila shaka walimtumia Graphic Designer wa timu ambaye uwezo wake ni mdogo sana ukilinganisha na quality Simba SC wanayostahili.

Ngoja niishie hapa bila shaka sijatoka nje ya mada ila pongezi kwako kwa kutusogezea huu uzi.
 
Professionalism at its finest!

Uzi mzuri sana umeuleta, mimi ni shabiki mkubwa wa ligi kuu ya England. Ila uzi huu uliponivutia zaidi ni kuhusiana na mambo ya Graphic Design ndani yake.

Kwa miaka karibu mitano nafanya Graphic Design ni moja ya sekta kubwa sana duniani hususani kipindi hiki mitandao ikitumika kwa kasi. Makampuni na biashara nyingi zinawekeza nguvu kubwa kuzalisha machapisho ya kuvutia kupakia kwenye kurasa zao za kijamii wakishirikiana na wabunifu wenye uwezo mkubwa katika sekta.

Kwa Tanzania hii ni sekta inayokua sana kwa kasi ila haina wateja wengi kama inavyostahili: Graphic Designer wengi nchini hawapewi kazi wanazostahili, wengi wanaishia ku-design vipeperushi tu vya sherehe na tafrija mbalimbali.

Ni makampuni machache nchini yametoa fursa kwa wabunifu wa hapa nchini, pia kukosekana kwa wateja ndiyo kunaifanya sekta kufa pia taratibu.

Tukibaki hapahapa kwenye soka, viwango na ubunifu wa wabunifu wanaopewa nafasi ni mdogo sana. Ukipitia page za timu kubwa kama Simba SC na Yanga SC unaweza kujiuliza maswali mengi ni aina gani ya Graphic Designer Ruvu Shooting FC watakuwa naye! Ukipitia page za TFF pia na aina ya machapisho yao utajua safari ni ndefu kufikia kutoa ubora stahiki.

Hii ni moja ya sekta inayochukuliwa poa na wengi na serious na wachache.

Ukitaka kujua ubunifu umeisaidia EPL ni katika branding, sasa hivi hiyo logo yao ukiiona bila maandishi unajua tu ni logo ya EPL. So hapa katika branding wamefaulu.

Juzujuzi Simba SC nao walifanya rebranding logo yao ila bado niliona kitu walichokipata hakikna ubora kulingana na brand ya Simba SC. Graphic Designer wachache wali-shout kuonyesha evidence kuwa Simba aliyewekwa kwenye logo alitolewa tu kwenye Adobe Stocks na kupachikwa.

Katika Branding, Simba SC walipaswa kwenda mbele zaidi na kuwakimbia wazawa, wangewapa kazi wabunifu kutoka nje naamini wangepata kitu kizuri sana kuitambulisha Club yao. Bila shaka walimtumia Graphic Designer wa timu ambaye uwezo wake ni mdogo sana ukilinganisha na quality Simba SC wanayostahili.

Ngoja niishie hapa bila shaka sijatoka nje ya mada ila pongezi kwako kwa kutusogezea huu uzi.

Graphics design mzuri yuko Yanga. Nenda ukacheki kwenye page utagundua kitu.
 
Graphics design mzuri yuko Yanga. Nenda ukacheki kwenye page utagundua kitu.
Sure mkuu, hapo nakubaliana nawe kazi yake anaifanya vizuri. Yupo simple na anatoa kitu kinachoeleweka.

Nimepitia page ya Simba kwenye poster ya kikosi chao cha leo utajua ni jinsi gani Graphic Designer wao ni wa kawaida. Ameweka details nyingi zisizo na msingi, kwa mfano kaweka jezi watakayovaa leo Simba kuwa ni Red: hivi ni nani asiyejua Simba yuko HOME hivyo atavaa jezi nyekundu!?

So mpaka hapo unajua tu ni aina gani ya mtu waliye naye.
 
Professionalism at its finest!

Uzi mzuri sana umeuleta, mimi ni shabiki mkubwa wa ligi kuu ya England. Ila uzi huu uliponivutia zaidi ni kuhusiana na mambo ya Graphic Design ndani yake.

Kwa miaka karibu mitano nafanya Graphic Design ni moja ya sekta kubwa sana duniani hususani kipindi hiki mitandao ikitumika kwa kasi. Makampuni na biashara nyingi zinawekeza nguvu kubwa kuzalisha machapisho ya kuvutia kupakia kwenye kurasa zao za kijamii wakishirikiana na wabunifu wenye uwezo mkubwa katika sekta.

Kwa Tanzania hii ni sekta inayokua sana kwa kasi ila haina wateja wengi kama inavyostahili: Graphic Designer wengi nchini hawapewi kazi wanazostahili, wengi wanaishia ku-design vipeperushi tu vya sherehe na tafrija mbalimbali.

Ni makampuni machache nchini yametoa fursa kwa wabunifu wa hapa nchini, pia kukosekana kwa wateja ndiyo kunaifanya sekta kufa pia taratibu.

Tukibaki hapahapa kwenye soka, viwango na ubunifu wa wabunifu wanaopewa nafasi ni mdogo sana. Ukipitia page za timu kubwa kama Simba SC na Yanga SC unaweza kujiuliza maswali mengi ni aina gani ya Graphic Designer Ruvu Shooting FC watakuwa naye! Ukipitia page za TFF pia na aina ya machapisho yao utajua safari ni ndefu kufikia kutoa ubora stahiki.

Hii ni moja ya sekta inayochukuliwa poa na wengi na serious na wachache.

Ukitaka kujua ubunifu umeisaidia EPL ni katika branding, sasa hivi hiyo logo yao ukiiona bila maandishi unajua tu ni logo ya EPL. So hapa katika branding wamefaulu.

Juzujuzi Simba SC nao walifanya rebranding logo yao ila bado niliona kitu walichokipata hakikna ubora kulingana na brand ya Simba SC. Graphic Designer wachache wali-shout kuonyesha evidence kuwa Simba aliyewekwa kwenye logo alitolewa tu kwenye Adobe Stocks na kupachikwa.

Katika Branding, Simba SC walipaswa kwenda mbele zaidi na kuwakimbia wazawa, wangewapa kazi wabunifu kutoka nje naamini wangepata kitu kizuri sana kuitambulisha Club yao. Bila shaka walimtumia Graphic Designer wa timu ambaye uwezo wake ni mdogo sana ukilinganisha na quality Simba SC wanayostahili.

Ngoja niishie hapa bila shaka sijatoka nje ya mada ila pongezi kwako kwa kutusogezea huu uzi.

Umeeleza kwa uzuri Forgotten tasnia ya picha mchocheo (Graphic Design) na ubunifu haipewi kipaumbele katika taifa na imekuwa ikionekana na ni 'For Fun Work' hali inayopelekea watu kuwashusha designers. Huwezi kuamini ni vilabu, vyombo vya habari, kampuni, taasisi, na mashirika machache yenye kutumia ubunifu kuongoza chapa zao.

Nakumbuka baada ya uzinduzi wa nembo ya simba niliwahi kumuuliza mbinifu na mwanateknolijia mmoja toka Colombia mbona sioni 'Branding Palette' namna hiyo logo itavyohusika katika masuala mbalimbali? Alinijibu if unaona kuna tatizo ulitakiwa kutatua mapema kabla ya kukufikia. Lakini ni wangapi walipata taarifa ya tenda?

Bado Tanzania ubunifu katika aspect za graphic design na audiovisuals zimelalia 2D, 3D na Enfo... Inaonyesha wabunifu wengi wapo 1990.

All in all! Forgotten tunaweza build something! If interested.
 
Hawa jamaa kila kitu kipo poa..

Graphics✓✓

Presenters kina Steve Bower✓✓

Commentetors✓✓

Picture quality✓✓


EPL tamu sana
Graphics - Presenters - Commentators - Technicians and co. Wapo chini ya Premier League Production.
 
Mkuu endelea kudadavua zaidi, mfano naweza kuuliza swali je?

Hawa DSTV wananunua LIVE GAME kutoka kwenye IMG STUDIO?
DStv hununua haki za matangazo Premier League Production (PLP) ambayo imepewa idhini na Premier League. PLP yenyewe inashirikiana na IMG Studios kiutendaji. Sio tu DStv bali televisheni zote zinazouza maudhui. Ni sawa na Ligu Kuu kuwa na kitengo au taasisi iliyochini yake inayofahamika kama Ligi Kuu Productions ambayo yafaa kusimamia maudhui. uzarishaji. uchakataji na usambazaji kwa Azam TV, GoTV, Startimes, Wasafi and co. katika packages tofauti, kwa sasa anayefanya hivyo ni Azam Productions anayegawa Azam TV inayosambaza maudhui kupitia Azam Sports Channels.

TFF, TPLB na Ligu Kuu zinatakiwa kujitenga kiutendaji katika ligi na kufanya uwekezaji wa masuala kama haya! Hasa katika masuala maudhui yafaa uwekezaji kutoka TFF na TPLB na washirika/wadhamini kuwekeza ndani ya taasisi ya Ligi Kuu kufanikisha haya.
 
DStv hununua haki za matangazo Premier League Production (PLP) ambayo imepewa idhini na Premier League. PLP yenyewe inashirikiana na IMG Studios kiutendaji. Sio tu DStv bali televisheni zote zinazouza maudhui. Ni sawa na Ligu Kuu kuwa na kitengo au taasisi iliyochini yake inayofahamika kama Ligi Kuu Productions ambayo yafaa kusimamia maudhui. uzarishaji. uchakataji na usambazaji kwa Azam TV, GoTV, Startimes, Wasafi and co. katika packages tofauti, kwa sasa anayefanya hivyo ni Azam Productions anayegawa Azam TV inayosambaza maudhui kupitia Azam Sports Channels.

TFF, TPLB na Ligu Kuu zinatakiwa kujitenga kiutendaji katika ligi na kufanya uwekezaji wa masuala kama haya! Hasa katika masuala maudhui yafaa uwekezaji kutoka TFF na TPLB na washirika/wadhamini kuwekeza ndani ya taasisi ya Ligi Kuu kufanikisha haya.

Ahsabte mkuu kwa jibu lako saf nimekupata ipasavyo kabsa.

Hakika wewe ni balaaa kwenye hili swala la PL
 
Umeeleza kwa uzuri Forgotten tasnia ya picha mchocheo (Graphic Design) na ubunifu haipewi kipaumbele katika taifa na imekuwa ikionekana na ni 'For Fun Work' hali inayopelekea watu kuwashusha designers. Huwezi kuamini ni vilabu, vyombo vya habari, kampuni, taasisi, na mashirika machache yenye kutumia ubunifu kuongoza chapa zao.

Nakumbuka baada ya uzinduzi wa nembo ya simba niliwahi kumuuliza mbinifu na mwanateknolijia mmoja toka Colombia mbona sioni 'Branding Palette' namna hiyo logo itavyohusika katika masuala mbalimbali? Alinijibu if unaona kuna tatizo ulitakiwa kutatua mapema kabla ya kukufikia. Lakini ni wangapi walipata taarifa ya tenda?

Bado Tanzania ubunifu katika aspect za graphic design na audiovisuals zimelalia 2D, 3D na Enfo... Inaonyesha wabunifu wengi wapo 1990.

All in all! Forgotten tunaweza build something! If interested.
Pamoja mkuu, ntakucheki PM tuzungumze kwa upana zaidi.
 
Umenifungua macho. Mimi nilijua kuna kampuni tofauti iliyoingia ubia na premier league ndio inaandaa matangazo then hawa dstv wananunulia kwao.
 
Back
Top Bottom