isajorsergio
Platinum Member
- Apr 22, 2018
- 4,143
- 6,560
- Thread starter
-
- #21
Hapana ni kitengo au taasisi iliyopewa dhamana ya masuala haya na kitengo hichi PLP kikaongeza nguvu na IMG kuhakisha mambo yanakuwa sawa.Umenifungua macho. Mimi nilijua kuna kampuni tofauti iliyoingia ubia na premier league ndio inaandaa matangazo then hawa dstv wananunulia kwao.
Na kuongeza tu..DStv hununua haki za matangazo Premier League Production (PLP) ambayo imepewa idhini na Premier League. PLP yenyewe inashirikiana na IMG Studios kiutendaji. Sio tu DStv bali televisheni zote zinazouza maudhui. Ni sawa na Ligu Kuu kuwa na kitengo au taasisi iliyochini yake inayofahamika kama Ligi Kuu Productions ambayo yafaa kusimamia maudhui. uzarishaji. uchakataji na usambazaji kwa Azam TV, GoTV, Startimes, Wasafi and co. katika packages tofauti, kwa sasa anayefanya hivyo ni Azam Productions anayegawa Azam TV inayosambaza maudhui kupitia Azam Sports Channels.
TFF, TPLB na Ligu Kuu zinatakiwa kujitenga kiutendaji katika ligi na kufanya uwekezaji wa masuala kama haya! Hasa katika masuala maudhui yafaa uwekezaji kutoka TFF na TPLB na washirika/wadhamini kuwekeza ndani ya taasisi ya Ligi Kuu kufanikisha haya.
Safi sana kwa kuongeza kitu muhimu sana, ni kweli SkySports na BT Sports hufanya uzalishaji wenyewe pia talksports kwa upande wa redio ndani ya Uingereza.Na kuongeza tu..
Kwa United Kingdom Skysport na BT wanafanya production wenyewe..lakini maeneo mengine mengi especially Africa na Asia tunapokea hayo matangazo ya PLP..
Unachokiona LaLiga ni Intel True View (Virtual Reality) ni mfumo unaorahisisha kuona mengi kwa mfumo wa 3D na 4D zinazochakatwa vyema kwa kutumia Camera Arrays zinazokuwa zimefungwa pembe 38 juu ya uwanja zikiendeshwa vilivyo na nyaya na kukuletea 3D view ya 360 Degrees. Intel Team yenyewe uhusika katika uzalishaji kivyake na uzigawa videos hizi hapo hapo kwa team ya LaLiga Live hii inatokana na mkataba baina ya LaLiga na Intel. Kwa upande Premier League mhusika wa masula haya ni EA Sports, sema binafsi naona ni kama outdated one.Ila kwa upande wangu naonaga LALIGA wanafanyaga kitu cha ziada sana ambacho EPL hawafanyi.
Kuna ile picha inacheza sekunde 2 tatu then inakuwa paused halafu ikiwa imeganda vile vile kamera inazungushwa pande zote ili mtazamaji ujionee vizuri mazingira ya goal labda, au namna walivyokosa nk.
Kingine wanavyoonesha kila kuonesha picha isiyo live kwenye positiona atakayochezea kwenye uwanja halisi.
Halafu mkuu nina swali kidogo, hivi wanaocontrol VAR wapo pale pale uwanjani au eneo tofauti?
Mkuu nimekunyoshea mkono. Umenifungua macho kuhusu hiyo 3D na 4D kuhusu hizo camera zinazofungwa katika pande zote za uwanja ili kupata virtual reality.Unachokiona LaLiga ni Intel True View (Virtual Reality) ni mfumo unaorahisisha kuona mengi kwa mfumo wa 3D na 4D zinazochakatwa vyema kwa kutumia Camera Arrays zinazokuwa zimefungwa pembe 38 juu ya uwanja zikiendeshwa vilivyo na nyaya na kukuletea 3D view ya 360 Degrees. Intel Team yenyewe uhusika katika uzalishaji kivyake na uzigawa videos hizi hapo hapo kwa team ya LaLiga Live hii inatokana na mkataba baina ya LaLiga na Intel. Kwa upande Premier League mhusika wa masula haya ni EA Sports, sema binafsi naona ni kama outdated one.
View attachment 1670996
View attachment 1670997
View attachment 1670998
View attachment 1670999
View attachment 1671000
Picha kwa hisani ya engadget.
Kwanza! Katika swali lako la pili, post yako ya kwanza nitaaeleza kama ifuatavyo namna VAR inaongozwa. VAR inaongozwa kwa kanuni mbili tofauti maeneo mengi. 1. VAR inaweza kuongozwa tokea sehemu moja ambayo inaweza kukusanya matokeo katika viwanja mbalimbali mfano, wakati wa Kombe La Dunia - Urussi 2018 mfumo wa VAR na maamuzi yote yalitokea jijini Moscow ndani ya chumba maalumu VOR - Video Operation Room ndani ya International Broadcast Centre (IBC).Sasa nikuulize swali dogo. Kwa mfano kama bongo tunaamua kutumia VAR kwenye ligi yetu, je itabidi kule azam tv kitengo cha kuchanganya picha na ku-replay, referees ndio wahusike na kazi hiyo badala ya azam wenyewe? Najua umenielewa.
Azam TV wao watafanya kazi ya kufikisha maudhui kama yanavyoonekana, yafikapo VOR, VAR Team inashirikiana na wataalamu wa Azam Productions kufanya marejeo (ex. Russia 2018) au/pia inawezekana waamuzi kujitegemea endapo wamepewa mafunzo ya kuendesha na kurudia matukio kupitia mfumo huu wa teknolojia (ex. Premier League VAR).Sasa nikuulize swali dogo. Kwa mfano kama bongo tunaamua kutumia VAR kwenye ligi yetu, je itabidi kule azam tv kitengo cha kuchanganya picha na ku-replay, referees ndio wahusike na kazi hiyo badala ya azam wenyewe? Najua umenielewa.