Silly
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 569
- 180
Hapa kuna barabara ambalo kimsingi linahudumia watu wengi, na kwa wengi sana limekuwa ni msaada mkubwa kwa kuwawezesha watu kufika Buhongwa bila ya ulazima wa kupita mjini kati.
Siku za hivi karibuni linatumika sana hata na magari makubwa na ukweli ni kwamba litakuwa ni msaada mkubwa sana kuepusha msongamano usio wa lazima kuwezesha kuingilia Buhongwa hadi ukanda wa mashariki mwa mji - (Igoma au Nyamongolo).
Zimekuwepo tetesi za siku nyingi zinazohusu hili barabara na majuzi wakati wanafanya upimaji barabara limeonekana kuhitaji mita 50 na tayari vigingi vimewekwa kuonyesha mipaka.
Hapa pia watu wengi wamesogea kupisha ujenzi huu. Swali ni lini kazi itaanza huku na je route ya hili barabara ni ipi maana Sahwa ya Chini na Juu zote zinaonekana kuwa na mahitaji makubwa.
Je ni lini Serikali itatujali sisi watumiaji wa hili barabara na wengine wengi ambao ni wahitaji.
Siku za hivi karibuni linatumika sana hata na magari makubwa na ukweli ni kwamba litakuwa ni msaada mkubwa sana kuepusha msongamano usio wa lazima kuwezesha kuingilia Buhongwa hadi ukanda wa mashariki mwa mji - (Igoma au Nyamongolo).
Zimekuwepo tetesi za siku nyingi zinazohusu hili barabara na majuzi wakati wanafanya upimaji barabara limeonekana kuhitaji mita 50 na tayari vigingi vimewekwa kuonyesha mipaka.
Hapa pia watu wengi wamesogea kupisha ujenzi huu. Swali ni lini kazi itaanza huku na je route ya hili barabara ni ipi maana Sahwa ya Chini na Juu zote zinaonekana kuwa na mahitaji makubwa.
Je ni lini Serikali itatujali sisi watumiaji wa hili barabara na wengine wengi ambao ni wahitaji.