IGP afuta kikosi kazi cha wakaguzi wa leseni za udereva kutokana na ongezeko la ajali

IGP afuta kikosi kazi cha wakaguzi wa leseni za udereva kutokana na ongezeko la ajali

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Camilius Wambura ametangaza kukifuta kikosi chote cha wakaguzi wa leseni za magari na watahini wa leseni na kuunda tume ya uchunguzi ili kuchunguza namna kikosi hicho kilivyokuwa kinatoa leseni kutokana na ongezeko la ajali za barabarani ambazo nyingi zimetokana na uzembe wa madereva.

#ITVUpdates

View attachment 2525701
Ukimaliza mafunzo ya udereva mkaguzi anapewa laki moja ili akupitishe.Usipotoa hiyo hela hutestiwi na leseni hupati
 
IGP kujishuhulisha na driving licenses inajionyesha ni jinsi gani nchi yetu imepotea mambo mengi, IGP pls fanya yafuatayo;TRA waondolewe kwenye kutoa hizi licenses, hizi leseni zitolewe na municipalities ambazo zitaunganishwa kwa systems moja (mapato yake ni mali ya municipalities)

Ruhusu private driving schools ziwe zinatoa mafunzo kwa madereva watarajiwa;mitihani ya kuandika kuhusu alama za barabarani, sheria na controls ifanyike chini ya traffic officer's including wa driving test(controlling na observations)viwe ndivyo vipimo muhimu, Traffic officer's kwenye mabarabara yetu wapunguzwe ili kuwa na polisi wengi wa ku patrol mitaani
 
Shida ni kwamba kuna watu tunahitaji leseni na hatujaweza kupata zaidi ya wiki sasa kisa igp kafuta hicho kikosi kazi....yani kweli nchi nzima tunashindwa kupata leseni kisa kuna wakaguzi wamefanya mambo ya hovyo kwenye kazi zao...kwa nn wengine tuadhibiwe kwa ujinga wa watu mliowaajiri wenyewe walioshindwa kufuata weledi wao....hii nchi ya ajabu sana

Mimi mwenyewe nasubiri leseni week ya pili sasa 🥲
 
Back
Top Bottom