IGP: Ajali ya Shabiby Tunduma trafic aliyewahi kupiga faini bus lolote la Shabiby kuanzia Sep 2024 hadi sasa awasiliane nami

Ni mbinu yake kuyumbisha mjadala, lengo tutumie muda mwingi kumuuliza ana maanisha nini tuache kuhoji tabia za hao madereva na boss wao kuhonga traffic
Mkuu shida si madereva. Shida ni mfanyabiashara na mbunge pia. Ao askari watamwajibishaje?. Nyerere alikataa haya mambo kuwa Kama wewe ni mfanya biashara Kaa pembeni fanya biashara yako kihalali lipa Kodi. Sasa mtu anafanya biashara alafu ana mamlaka pia. Askali wakipiga faini wanaonywa na wakati mwingine wanaamishwa mpaka vituo vya kazi
 
Haya mambo ndiyo yananifanya nataka kuwa kiongozi yaani kuna watu wanajikuta miungu watu. Aisee
 
Hawa madereva wa mabasi hawana tofauti na magaidi na hawana tofauti na mmiliki wa gorofa la kariakoo.

Kuna wakati natoka mwanza kuja Dar nipo na abood tukanusurika na ajali kibaigwa nikaenda mbele kugombana na dereva basi likasimama ajabu abiria wote ndani ya basi walinyamaza kimya Kama mazombie na abiria mmoja akawa anamtetea dereva.
Kichekesho kingine dada niliekuwa nae Siti ya jirani hakunichangamkia Tena 😁 aliniona mkorofi .
 
Ktk bus nilikua napata amani kusafiri nalo ni haya mabus ya Shabiby..ila sasa ndo hivi tena
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…