IGP mshawishi Rais Samia akuruhusu utumie japo 50% ya bilioni 125 kuboresha makazi ya Askari NCHINI. Uchaguzi ni tendo la siku moja

IGP mshawishi Rais Samia akuruhusu utumie japo 50% ya bilioni 125 kuboresha makazi ya Askari NCHINI. Uchaguzi ni tendo la siku moja

Resilience

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2023
Posts
1,096
Reaction score
4,948
IGP upo katika kipindi ambacho serikali inakuhitaji kuliko wakati wowote. Watangulizi wako pamoja na wewe mmekuwa mkiomba bajeti ya kuboresha makazi ya askari bila mafanikio kwa miaka mingi. Lakini kila inapofika kipindi cha uchaguzi watu wale wale wasiokuwa na fedha ya kukusaidia kuboresha makazi ya watumishi wako utangaza na kupitisha mabilioni ya fedha kukutumia uwasaidie kwenye tendo la kisiasa.

Skiatai kwamba uchaguzi ni gharama ila naamini askari anachohitaji si fedha anahitaji jambo ambalo linampa hadhi na furaha. Mimi kwa mtizamo wangu, askari angependa kulea familia yake kama wanavyolea watumishi wengine wa bandari, TAkukuru, TRA na taasisi nyingine. Makazi ya watumishi wa taasisi nilizotaja yanaakisi fikra na mnunurisho ndani ya miyoyo yao na miyoyo ya familia zao. Makazi hayo yanawapa faragha na kuwafanya wawe na amani makazini.

Nakubali kwamba yapo maeneo askari wana makazi bora ikiwemo baadhi ya miji kama Dar, ila pia yapo makazi duni yaliyojengwa na mkoloni; naamini pia zipo familia za askari wanaishi chumba na sebule hata katika miji mikubwa.

Niwapongeze wapiganaji hawa kwa kuheshimu kiapo chao lakini nitumie fursa hii na jukwaa letu kuwafikirisha zaidi viongozi wa jeshi letu pamoja na viongozi wa kisiasa.

Mhe. Rais ameingia kusaka bilioni 125 kama mlivyoomba. Sijui fedha hizo mmesema zinakwenda kusaidia nini ila niwaombe pamoja na vipaombele vyote mlivyompa , kama kipaombele cha nyumba za askari siyo sehemu ya mkakati wenu kusimamia uchaguzi mtakuwa mmekosea sana.

Nikipiga mahesabu hizi fedha endapo mtawalipa posho sidhani kama kuna askari wa chini atalipwa jumla ya laki tano kwa chaguzi zote mbili yaani 2024 na 2025. Ila mkifanya maamuzi kwamba mnawanyima wengi posho mnawapatia wachache makazi I hope hii itasaidia hao wachache na watoto wao lakini pia itawasaidia wapiga kura kuepukana na treatment zisizo na staha kwa sababu mtu mwenye furaha ya nafsi utoa huduma yenye kiwango.

Viongozi wa jeshi la polisi, kupitia tafakuri hii; trudini kwa mama mkamwombe awape japo 50% ya fedha za uchaguzi mkarabati miundombinu ya makazi ya wale askari wadogo wanaokwenda kusimamia uchaguzi.

Bilioni 62 kwa mikoa tuseme kumi ni sawa na kutenga kiasi cha bilioni sita za ukarabati na ujenzi kwa kila mkoa.

Ni mimi mtetezi wa walinzi wetu; kambale wa Mwanza ahsanteni
 
Askari ni masikini akafeli la Saba tu,kazi yake Ni kumlinda ntawala ili amnyonye na kumtawala masikini mwenzake.

Askari afanye kazi Kama robot no question eti amri ya mkubwa. Yaani aliye program majeshi ana akili kubwa mno .wewe mlinde mwanaume mwenzako akunyonye damu
 
Tuwekee kapicha basi ka hizo nyumba za masoja tuone iivyochakaa
 
Hivi uwa ni lazima kuishi kwenye zile nyumba aseee...ila wenye Kisanga ni askari magereza wale jamaa wana nyumba mbayaaa sija wahi ona ..rejea pale butimba zile nyumba zilifaa wakae mifugo
 
Hivi uwa ni lazima kuishi kwenye zile nyumba aseee...ila wenye Kisanga ni askari magereza wale jamaa wana nyumba mbayaaa sija wahi ona ..rejea pale butimba zile nyumba zilifaa wakae mifugo
Lipo tatizo la kifikra la kuunganisha umaskini na uzalendo . This is wrong perception

Wanasiasa wazalendo hakuna anayeishi maisha ya tabu na dhiki; wazalendo wetu askari wapo kwenye maisha ambayo hata ndugu wakiomba kuja kuwatembelea wanaogopa.

Good thing ni kwamba kizazi cha sasa naona wameamua kwa dhati kutoishi kwenye makazi duni na wengi walioamua kwenda kupangisha wamefanikiwa kujenga na wana mahusiano mazuri na wananchi kwa sababu wanaishi kwenye jamii.

Usipoishi na wananchi ukaona hadha na furaha zao ni vigumu kuyajua matatizo yao. Natamani bilioni kadhaa zipelekwe zikalete aman kwenye nafsi za hawa watoto wetu.

Naamini ujumbe huu kama Mwenyenzi Mungu aishivyo unakwenda kuwaondoa baadhi ya walinzi wetu kwenye maisha ya kulaza watoto sebuleni na kwenda kuwaruhusu sasa watoto hao kuishi kwa hadhi ya kazi za baba zao.

Mwenyenzi fungua Miyoyo na macho ya watu hawa waweze kujiuliza wao wakiambiwa waishi au wapeleke familia zao kwenye hizi nyumba watapeleka? Je kama awatapeleka, wanaamini wao wanatofauti na haw a wadogo na watoto wao? Ongea na viongozi hawa waeleze kiu ya wapiganaji walio chini yao
 
Polisi ni mbwa wa watawala!
Wapo very loyal kwa wamiliki wao. HaijLishi wanatendewa maovu gani.
Mbwa halali usiku ili mmiliki wake awe salama!
 
Askari wawe upande wa haki, nikimaanisha wasimamie haki,kipindi hicho cha uchaguzi,hii itafanya umuhimu wao uonekane.Kuna chama huwa kinawatumia tu,na mwishowe hawawajali,wanabaki kuwasimanga majukwaani,kua ni wala rushwa.
 
Bora askari je walimu wa shule za misingi au secondary ambao wanawakilishwa na Waziri mkuu naibu waziri mkuu hahahaha vituko nyumba wanazokaa. Kwanza tu vaa ya waalimu ya kimasikini masikini. Nikiwa rais mimi waalimu kima cha chini mshahara ni mil 5.
 
Sijui kwann wakoloni waliwajengea askari wa kiafrika nyumba za bati fully suit mchana joto kama jiko la mchina usiku baridi hadi umande unadondokea shuka
 
Kuna ka-nchi mpinzani aliwahi sema hivyo kabla ya Uchaguzi, kilichotokea mnakijua , nimesahau jina la nchi huko West Africa.
 
Ndiyo maana wanakomaa kulinda jezi zao. Kuna mdau alitoa hoja hiyo. Misoto wanayopitia malipo ni kutokuruhusu kutinga nguo zinazofanana na zao.

Kuhusu hoja naunga mkono, binafsi mambo ya uchaguzi kama tungekuwa tunafanya kwa haki sioni hata gharama ya bilioni kumi kutumika.

Tatizo hadaa nyingi sana na kukuza mambo.
 
Ni muhimu kuwaheshimu watu wote kwa ujumla wake.
Wapo askari wenye akili nzuri na weledi kama ilivyo kwenye profession nyingine.
Hawa askari ni watu muhimu sana kwenye jamii kama wakijielewa. Changamoto kubwa kwao ni kwa kuwa vipato halali ni duni kwa sababu tu ya umasikini wa nchi na hivyo rushwa kuwa ndiyo chanzo kikuu cha mapato kwa walio wengi ili wapate maisha Bora.
Hili hali haiwahusu askari tu, ila kwa sababu wao ni wawezeshaji wa wanasiasa kutawala (ulinzi) lawama huenda kwao kutoka kwa makundi hasimu.
Bottom line ni kwa askari kuwa mwadilifu, kutenda haki na heshima yake itakuwa kubwa kuliko mwananchi mwingine yeyote. Katika nchi yoyote, askari yupo juu kama anajielewa. Sababu ya kupeleka watu wetu JKT ilikuwa kuwafanya wawe raia wenye kujielewa katika kutetea nchi yao (uzalendo).
Hata hivyo, uzalendo ni kipenda na kuipigania nchi yako, siyo serikali au viongozi (serikali na viongozi ni tofauti na nchi. Kuna changamoto ya wengi kushindwa kutofautisha ).
 
Leo nilikwenda kula burudani kwenye beach hotels za Bagamoyo, nikaoneshwa nyumba za askari polisi.

Hakika hawa watu wanateseka. Wanaishia kwenye nyumba mbovu zilizojaa nyufa yaani magofu kabisa.
 
Back
Top Bottom