IGP Sirro afanya mabadiliko: ACP Wankyo Nyigesa arudishwa Makao Makuu kupisha Uchunguzi, ACP Mwampakale awa RPC Kagera

IGP Sirro afanya mabadiliko: ACP Wankyo Nyigesa arudishwa Makao Makuu kupisha Uchunguzi, ACP Mwampakale awa RPC Kagera

Polisi kuna shida ya nidhamu. Utomvu wa nidhamu kwa askari wadogo kama mauaji kule Mtwara ni kielelezo cha hali halisi huko juu. Hili la Wankyo ni tukio la aibu mno kijeshi!

Ni dhamira ya kutaka madaraka ya mkuu wa jeshi la Polisi! Hii case inaweza kumuweka pabaya mno huyu RPC.

Nafikiri toka Sirro alalamike kuwa wapo makamanda waliona wao walifaa kuliko yeye na hili la juzi, ni muhimu hili Jeshi litazamwe upya kurudisha nidhamu. Ni jeshi muhimu mno na kilelezo cha ulinzi wa Taifa lolote!

Hapa tupa kule unampenda Sirro au humpendi, Jeshi lina mipaka yake ya nidhamu. Ni hatari mtu wa cheo kile kuongea vile hadharani! Kesho akisema anatamani Urais? Hatari! Hatari! Hatari!

Mungu ibariki Tanzania [emoji1241]
 
Kwa jinsi ulivyo na ulivoandika hufai kuwa staff wa jf umedhihirisha uwezo wako Mdogo wa kutafakari na kung'amua Mambo pia ujuhi umuhimu wa kukaa kimya ili usionekane mjinga
umeamua tu kunisakama ila hoja huna , halafu unapaswa kufahamu kwamba sijawahi kuhofia madongo duni kama hayo yako
 
Polisi kuna shida ya nidhamu. Utomvu wa nidhamu kwa askari wadogo kama mauaji kule Mtwara ni kielelezo cha hali halisi huko juu. Hili la Wankyo ni tukio la aibu mno kijeshi...
Sirro hastahili hiyo heshima kutokana na ukweli unaoufahamu
 
Pole zake ACP Wankyo, waswahili wanasema kama ipo, ipo tu!

Binafsi sijaona kosa la Wankyo kiasi cha kuanza kufanyiwa uchunguzi mitaani na mitandaoni wamejaa vibaka kibao bado wanatapeli watu, kwanini hao ndio wasiwafanyie uchunguzi?

After all, ikumbukwe kuwa wakati wa sherehe za kuagana kama hizo watu huwa wanakunywa pombe, hivyo kutoa kauli kama hizo ni jambo la kawaida kabisa hivyo Siro alipaswa kuwa mvumilivu wa kauli kama hizo!
 
Huyu afande ana akili nyingi Sana, hakutaka kwenda Kagera. Alijua akim- provoc Mkuu wake, obviously atapelekwa makao makuu. Pale ndo atajijenga na Kisha ndoto zake zitatimia.

Hivi mnapajua Kagera?! Waache waende hao waliotoka Rukwa labda watapata nafuu.

Mawazo binafsi.
Subiri kina masifa wenye mkoa wao watakujibu😀
 
Taarifa zilizopo ni kwamba RPC KAGERA ambaye ametoka Pwani na kupelekwa mkoa Kagera ndugu Wankyo nadhani kauli ya jana ya kuhitaji ukuu wa Jeshi la Polisi imemuungiza matatani hii imeonesha hana nidhamu ya hali ya juu ndani ya jeshi hivyo basi staff officer aliyepo mkoa wa Rukwa ameteuliwa kuwa kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Kagera na Wankyo amepelekwa makao makuu ya jeshi mkoani DODOMA ambapo ni mji mkuu wa tanzania.

Ikumbukwe kuwa kauli aliyotoa jana kiutendaji ndani ya jeshi la polisi huku akijuwa mkuu wake wa kazi yupo na anafanya kazi hakustahili kusema kuwa mkuu wake wa kazi anafanya kazi ila yeye akipewa ukuu wa jeshi anaweza kufanya vizuri zaidi hii imeonesha kuwa nafasi aliyeteuliwa na amri jeshi mkuu hatoshi kuliongoza jeshi hivyo basi kwa kuwa jeshi huongozwa kwa nidhamu ya hali ya juu ndiyo maana mabadiliko hayo yamefanyika ili akae makao makuu ajifunze nidhamu pamoja na kuandika vipeperushi mabalimbali vinavyolihusu jeshi la polisi.

Pia soma: Wankyo Nyigesa RPC Kagera: Natamani kuwa IGP, aliyepo hajafanya makosa lakini mimi nitafanya mazuri zaidi

WENYE MADARAKA kumbukeni VYEO ni Kama KOTI kuna KUVAA na KUVUA
 
nani amuwajibishe yule anaetaka kutawala miaka kumi mbele bila kidhibiti cha uchafuzi😄😄


hii inchi ukiwa na katucheo kubali msujudiaji mambo ya uropokaji sasa unafanana na Assistant officer😄😄
 
Taarifa zilizopo ni kwamba RPC KAGERA ambaye ametoka Pwani na kupelekwa mkoa Kagera ndugu Wankyo nadhani kauli ya jana ya kuhitaji ukuu wa Jeshi la Polisi imemuungiza matatani hii imeonesha hana nidhamu ya hali ya juu ndani ya jeshi hivyo basi staff officer aliyepo mkoa wa Rukwa ameteuliwa kuwa kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Kagera na Wankyo amepelekwa makao makuu ya jeshi mkoani DODOMA ambapo ni mji mkuu wa tanzania.

Ikumbukwe kuwa kauli aliyotoa jana kiutendaji ndani ya jeshi la polisi huku akijuwa mkuu wake wa kazi yupo na anafanya kazi hakustahili kusema kuwa mkuu wake wa kazi anafanya kazi ila yeye akipewa ukuu wa jeshi anaweza kufanya vizuri zaidi hii imeonesha kuwa nafasi aliyeteuliwa na amri jeshi mkuu hatoshi kuliongoza jeshi hivyo basi kwa kuwa jeshi huongozwa kwa nidhamu ya hali ya juu ndiyo maana mabadiliko hayo yamefanyika ili akae makao makuu ajifunze nidhamu pamoja na kuandika vipeperushi mabalimbali vinavyolihusu jeshi la polisi.

Pia soma: Wankyo Nyigesa RPC Kagera: Natamani kuwa IGP, aliyepo hajafanya makosa lakini mimi nitafanya mazuri zaidi

Kumekucha kumekucha wacha aende huko akakoroge chai na kalamu utamtukanaje mkunga na uzazi ungalipo?
 
Back
Top Bottom